Sunday, 14 May 2017

Korea Kaskazini: Kombora jipya lina uwezo wa kubeba nyuklia

Gwaride la kijeshi lililofanywa na Korea Kaskazini hivi karibuni

Gwaride la kijeshi lililofanywa na Korea Kaskazini hivi karibuni

Korea Kaskazini imedai kwamba kombora la masafara marefu ililolifanyia majaribio siku ya Jumapili ni kombora jipya linaloweza kubeba kichwa cha nyuklia .

Kombora hilo lililorushwa lilienda anagani urefu wa kilomita 2,000 na kusafiri kilomita 700 kabla ya kuanguka katika bahari Magharibi mwa Japan.

Korea Kaskazini ilisema siku ya Jumatatu ni jaribio la uwezo wa kombora jipya.

Jeshi la Korea Kusini limesema kuwa haliweza kuthibitisha madai hayo ya Korea Kaskazini. kuruka angani, hatua ambayo ni muhimu katika utengenezaji wa makombora ya masafa marefu kulingana na kituo cha habari cha Yonhap.

Majaribio ya mara kwa mara ya makobora ya masafa marefu yanayofanywa na taifa hilo yanakiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa na yamesababisha wasiwasi miongoni mwa jamii ya kimataifa pamoja na Marekani.

Marekani na Japan zimetaka kufanyika kwa mkutano wa dharura katika baraza la usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne.

Shirika la habari la Korea Kaskazini KCNA limesema Jumatatu kwamba jaribio la kombora jipya la masafa marefu la Hwasong 12 lilifanyika kama ilivyopangwa.

Limesema kuwa jaribio hilo lililenga kuonyesha kwamba kombora hilo jipya lina uwezo wa kubeba kichwa cha Nyuklia.

Trump atakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo na James Comey

Donald Trump ametakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkuu wa FBI James Comey

Donald Trump ametakiwa kusalimisha kanda za mazungumzo yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkuu wa FBI James Comey

Wabunge wandamizi nchini Marekani wamemtaka rais Donald Trump kusalimisha mazungumzo yoyote yaliorekodiwa kati yake na aliyekuwa mkurugenzi wa shirika la FBI James Comey aliyemfuta kazi.

Kiongozi wa Democrats katika bunge la seneti Charles Schumer alionya kuwa uharibifu wa kanda hizo utakuwa uvunjaji wa sheria.

Naye Seneta wa Republican Lindset Graham alisema kuwa Ikulu ya Whitehouse inahitaji kuwa wazi kuhusu iwapo kulikuwa na kanda zozote za rekodi za mazungumzo hayo au la.

Matamshi hayo yanajiri baada ya bwana Trump kusema katika mtandao wake wa Twitter matamshi yanayoonekana kuwa vitisho kwa mkuu huyo wa zamani wa FBI.

Alimuonya Comey wiki iliopita dhidi ya kuzungumza na vyombo vya habari akisema natumai hakuna rekodi za mazungumzo yetu.

Ikulu ya Whitehouse haijathibitisha wala kukana kuwepo kwa kanda hizo.

Bwana Schumer pia alionya kwamba masenata wa chama cha Democrats watakataa kumuunga mkurugenzi mpya wa FBI hadi pale mtaalam atakapochaguliwa kuchunguza hatua ya Urusi kuingilia maswala ya Marekani katika uchaguzi uliopita.

FBI inachunguza madai hayo pamoja na ushirikiano wa Urusi na kampeni ya rais Trump.

Rais Trump amekana uhusiano wowote na anasema bwana Comey amemhakikishia kwamba hachunguzwi.

Anasema kuwa alimpiga kalamu bwana Comey kwa sababu alikuwa ameshindwa kufanya kazi vizuri.

Wanachama wa Democrats wameshutumu Trump kwa kumfuta kazi Comey ili kujaribu kusitisha uchunguzi wa FBI.

Wafungwa 12 wapigwa risasi Papua New Guinea

Mwaka 2016 inadaiwa kuwa wafungwa walivamia lango kuu la gereza hilo

Mwaka 2016 inadaiwa kuwa wafungwa walivamia lango kuu la gereza hilo

Maafisa wa magereza nchini Papua New Guinea, wamewapiga risasi na kuwauwa wafungwa 17, ambao walivunja gereza na kutoroka siku ya Ijumaa.

Polisi wamewatia mbaroni wafungwa watatu, huku wakiendelea kuwasaka wengine 50 ambao bado hawajulikani waliko tangu kutokea kwa kisa hicho katika gereza la Buimo katika mji wa Lae.

Polisi wanasema kuwa, wengi wa wafungwa waliotoroka walikuwa wahalifu sugu.

Idara ya usalama nchini humo imewatahadharisha raia kuwa macho na watoe taarifa kwa vyombo vya usalama pindi wakiwaona wafungwa hao.

Gereza hilo la Buimo huwa na msongamano mkubwa wa wafungwa na uchafu na mwaka jana wafungwa 12 waliuawa baada ya kujaribu kutoroka.

clouds stream