Thursday 9 November 2017

Aliyedaiwa Kununua Nyumba Za Lugumi Akamatwa Na Polisi



Moja ya nyumba hizo za Lugumi.



Mtu aliyedaiwa kujitokeza leo na kufanikiwa kununua nyumba mbili za Mfanyabiashara, Said Lugumi, Dkt. Luis Shika amekamatwa na Jeshi la Polisi baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya fedha kama yalivyo masharti ya mnada. Mnada huo sasa unarudiwa tena muda huu.

Awali mtu huyo aliyefika mnadani hapo akiwa amevaa suruali, shati, tai na makobazi (sandals) alidaiwa kufanikiwa kununua nyumba hizo mbili za Mfanyabiashara, Said Lugumi zilizopo Mbweni, Jijini Dar es Salaam kwa Shilingi Bilioni 1.1 na Shilingi Milioni 900 kupitia kampuni ya udalali ya Yono.

Nyumba hizo zinauzwa kwa njia ya mnada kufuatia deni alilokuwa akidaiwa Lugumi na Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambapo katika mnada wa awali nyumba hizo zilikosa wateja kutokana na bei yake kuwa juu sana.


Dkt. Luis Shika.

clouds stream