Sunday 12 November 2017

Mgomo Mabasi Mikoani Wanukia, Wananchi Waaswa Kutokata Tiketi




Taswira nzima ya mabasi yaendayo Mikoani na Nchi Jirani katika Kituo cha Ubungo.



Chama cha Wamiliki wa Mabasi yaendayo Mikoani na Nchi Jirani Tanzania (TABOA), kimewataka wananchi kutokata tiketi za kusafiri kwa siku ya kesho, Jumanne, kufuatia mgomo wa mabasi hayo.

Katibu Mkuu wa TABOA, Enea Mrutu amesema hayo kupitia Mkutano Mkuu Maalum wa TABOA na kudai kuwa maamuzi ya mgomo huo ni katika kuwashinikiza wabunge kutopitisha sheria kandamizi dhidi ya wamiliki wa mabasi.

Amesema sheria hiyo ni kandamizi kwakuwa inashindwa kutofautisha kosa la mmiliki wa basi na dereva.

“Tunaomba radhi wateja wetu wote kwa kuwanyima huduma lakini kimsingi sheria hiyo ndiyo inayowanyima huduma,” amesema.

Ameongeza kuwa vita yao kubwa ni sheria ambayo haikutenganisha makosa baina ya dereva na mmiliki wa chombo husika na kupelekea kumfunga mmliki kwa kosa linalomhusu dereva.

“Tulisema sheria hiyo ibainishe makosa ili kosa linalomhusu dereva liende kwa dereva na lile linalomhusu mmiliki liende kwa mmiliki lakini wenzetu hawakusikia hivyo tumesema watu wasikate tiketi na Jumanne ndio mwisho wa kutoa huduma,” amesisitiza.

clouds stream