Sunday 12 November 2017

Lema Atoa Ushauri Kuhusu ‘Wabunge Wa Lipumba’



Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.



Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Godbless Lema amemshauri Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai kutumia busara kuwaondoa bungeni wabunge nane walioingia bungeni kuziba nafasi za wabunge nane waliokuwa wamevuliwa uanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) Julai 24, mwaka huu.

Lema ametoa ushauri huo kupitia mtandao wake wa kijamii ikiwa ni siku chache tu baada ya Mahakama Kuu kutengua uamuzi wa
kufukuzwa kwa Wabunge 8 na Madiwani 2 wa CUF mpaka pale shauri la msingi litakaposikilizwa.

“Mh Spika anapaswa kuzingatia kwa busara uamuzi uliotolewa na mahakama kwa kuwaondoa wale Wabunge wa Lipumba ndani ya Bunge na kuwarejesha Wabunge halali sasa, mpaka hapo haki itakaposhinda zaidi,”ameandika Lema.

Wabunge hao nane walivuliwa uanachama Julai 24 na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi, CUF linaloongozwa na Prof. Lipumba kwa madai ya utovu wa nidhamu yakiwemo kukisaliti chama hicho na Tume ya Uchaguzi (NEC) kuteua wabunge wengine kutokana na uamuzi huo na kuchukua nafasi zao maramoja.

clouds stream