Sunday, 1 October 2017
Mbunge Chadema Aweka Hadharani Ushahidi Madiwani Walivyonunuliwa

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari ameweka hadharani ushahidi wa rushwa waliyopewa waliokuwa
madiwani wa Chadema ambao wamejiuzulu kwa madai ya kumuunga mkono Rais Magufuli na kuhama chama hicho.
Nassari ambaye aliambatana na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema walitoa ushahidi huo mbele ya waandishi wa habari na kueleza kuwa wataukabidhi katika mamlaka husika leo ikiwemo Taasisi ya Kupambana na Kuzuia Rushwa (Takukuru) na katika
taasisi nyingine.
Katika ushahidi wa video uliorekodiwa viongozi kadhaa wakiwemo Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alexander Mnyeti pamoja
Mkurugenzi Mtendaji wa (H) Meru Christopher Kazeri wamesikika wakiwashawishi madiwani kuhama na baadhi waliahidiwa
wangelipwa posho za vikao vyao vilivyobaki hadi 2020 na kukamilishwa miradi yao.
Miongoni mwa makubaliano hayo ni kuwa wapewe fedha na kupata ajira na kukamilishwa miradi yote ya maendeleo waliyoahidi ikiwa ni pamoja na wengine kubadilishiwa makazi pamoja na diwani mmoja kusaidiwa gharama za kufanikisha harusi.
“Tutafikisha ushahidi huu katika ofisi za TAKUKURU Dar es Salaam kwa ajili ya kuukabidhi kwa Mkurugenzi Valentino Mlowola,”amesema.
Hatahivyo wakati Nassari akitoa ushahidi huo hadharani, madiwani 10 wa Chadema tayari wameshapokelewa ndani ya CCM huku wengine wakiwa wamepinga vikali kuhama chama hicho kwa sababu ya rushwa.
Aidha Nassari amesema ameamua kutoa ushahidi huo sasa kwa sababu alikuwa akiendelea kukusanya ushahidi wa kutosha.
“Mimi sina tatizo kwa mtu mmoja kuhama chama kwa utashi wake, ila kuhama kwa njia za kushawishiwa kwa rushwa ndiyo kitukibaya sana na ninataka Rais Magufuli achukue hatua dhidi ya jambo hili ili asihusishwe na uovu huu,” ameongeza.
Professor Jay Afunguka Machungu Ya Kubomolewa Nyumba

Mbunge wa Mikumi (Chadea), Joseph Haule ‘Professor Jay’ ametumia mitandao yake ya kijamii kueleza machache na uchungu
aliousikia kuhusiana na kubomolewa kwa nyumba za wananchi huko Mbezi Kimara ikiwemo nyumba yake.
Professor Jay ameandika yafuatayo;
“Mimi ni mmoja wa wahanga wa hili zoezi la kubomolewa nyumba zetu huku Mbezi Kimara Tarehe 29/9/ 2017. Jana (juzi) nikiwa
katika majukumu jimboni Mikumi Majira ya saa kumi mbili hivi jioni, nilitaarifiwa kwamba, watu wa Tanroads wakiwa
wameambatana na grader mbili na magari mawili ya polisi (defenders) yenye askari waliokuwa na silaha mbalimbali za moto
walikuwa wanabomoa nyumba yangu, sijawahi kuumia kiasi hiki.
“Nimesikitishwa sana jinsi Tanroads wanavyoweza kujichukulia maamuzi bila ya kujali mhimili muhimu wa Mahakama wametoa
maagizo gani. Na taratibu zilizotumiwa kubomoa nyumba yangu bila ya mimi na Tanesco kupewa taarifa saa kumi na mbili jioni
(haukuwa muda wa kazi). Poa kubomoa nyumba huku Umeme ukiwa unawaka ni kitendo ambacho kwanza kina hatarisha maisha
ya wabomoaji wenyewe, maisha ya familia yangu pamoja na majirani zangu, LIMENISIKITISHA zaidi.
Nasema hivi kwasababu Tanesco wamenipigia simu baada ya masaa 24 au zaidi baada ya zoezi la kubomoa nyumba kufanyika
kunitaarifu kuja kukata Umeme kabla ya ubomoaji huo, pindi nilipo waambia kwamba mbona nyumba IMESHABOMOLEWA kabisa
na sijaweza kuokoa kitu chochote na hata hiyo meter yenu mnayoiulizia mkaitafute kwenye kile kifusi cha nyumba yangu
kilichokusanywa kwa pamoja na watu wa Tanroads. Tanesco walishangazwa sana kuvunjwa nyumba yangu kwa taratibu hizo.
Lakini naamini kila kitu kinatokea kwa sababu maalum. Nimejifunza kumtegemea Na kumshukuru Mungu kwa kila jambo. Na hili
ni moja ya mitihani ya hapa duniani. Nimepokea na kumsikiliza Mungu ana mipango gani juu yetu katika familia yangu mbeleni.
Tumelipokea na Naamini tutashinda.”
Subscribe to:
Posts (Atom)


