Saturday, 10 October 2015

Magufuli awanadi Ridhiwani, Kawambwa mkoani Pwani


Magufuli awanadi Ridhiwani, Kawambwa mkoani Pwani

Tarehe October 10, 2015

Mgombea wa Urais kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo jimbo la Chalinze Ndugu Ridhiwani Kikwete.
Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli ameipongeza wilaya ya Bagamoyo kufuatia kugulika kwa gesi ambayo itasaidia kukuza uchumi hapa nchini wakati akiwanadi wanasiasa Ridhiwani Kikwete pamoja na Shukuru Kawambwa.
Akizungumza katika mikutano yake ya kampeni iliyofanyika katika majimbo ya Chalinze na Bagamoyo Magufuli alibanisha kuwa ugunduzi wa gesi hiyo itasaidia ujenzi wa viwanda katika serikali yake.
Kwa upande mwingine Magufuli  alisema serikali yake anatarajia iwe ya viwanda ili kutoa fulsa ya ajira kwa vijana ambao wamekuwa hawana kazi mara baada ya kumaliza masomo yao.

Mgombea urais TLP, afunguka Mrema kumnadi Magufuli


Mgombea urais TLP, afunguka Mrema kumnadi Magufuli


Tarehe October 9, 2015
Mgombea urais kupitia chama cha TLP Macmillan Lyimo.
Mgombea urais kupitia chama cha TLP Macmillan Lyimo amefunguka kufuatia Mwenyekiti wa chama chake cha TLP Augustine Mrema kumnadi mgombea wa Chama cha Mapinduzi Dkt.John Pombe Magufuli wakati naye pia ni mgombea urais. Akizungumza na kituo kimoja cha redio Lyimo amesema kwamba hayo ni maamuzi yake binafsi na kwamba kauli hiyo haijatolewa na mkutano wowote wa chama, bali ni maoni binafsi akisisitiza kuwa alilofanya Mrema si jipya wa la ajabu.
“Hili jambo siyo la ajabu, hata Marekani, Colin Powell alitangaza kumuunga mkono Obama licha ya kuwa chama tofauti pia uamuzi wake haunipi shida. Amesema Macmillan Lyimo
Alipoulizwa mahusiano kati yake na mwenyekiti huyo, Lyimo amesema kuwa mahusiano ndani ya chama hicho ni mazuri na hakuna ugomvi wowote.
Akizungumzia kampeni za uchaguzi pamoja na wagombea urais Lyimo amesema yeye ndiye atakayeshinda urais mwaka huu, na kamwe Rais hatoki CCM.
Mwenyekiti wa chama cha Siasa cha TLP Augustino Mrema akiwa na mgombea urais wa CCM Dkt,John Pombe Magufuli.

Mosore ageuka Mbogo NCCR-Mageuzi, agoma kung’oka

Mosore ageuka Mbogo NCCR-Mageuzi, agoma kung’oka

Tarehe October 9, 2015
Makamu Mwenyekiti wa NCCR- Mageuzi (Bara), Leticia Ghati Mossore.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi Leticia Mosore amegeuka mbogo kufuatia kugoma kuong’olewa madarakani kama ilivyotangazwa na Mwenyekiti wa chama hicho James Mbatia hivi karibuni.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam Mosore amepinga vikali madai ya mwenyekiti wa chama hicho James Mbatia kwamba anatumika na chama cha Mapinduzi kwa ajili ya kukibomoa chama chao ambacho ni mshirika mkubwa wa umoja wa katiba ya wananchi UKAWA.
Mosore amesema kwamba madai ya kutumika hayana ukweli wowote ukilinganisha na madai yake kwamba chama chao kimepewa majimbo machache pamoja na Mwenyekiti wake kuonekana anaegemea sana katika kutekeleza majukumu ya ukawa na kukitelekeza chama cha NCCR-Mageuzi.

Katika hatua nyingine Mosore amemshangaa Mbatia kusema kuwa ametumika wakati yeye aliteuliwa ubunge wa viti maalumu na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akihoji ni kipi zaidi alicho kifanya hadi kufikia chama cha Mapinduzi kumzawadia nafasi hiyo nyeti ya ubunge.

clouds stream