Monday, 7 December 2015

Kasi ya Rais Magufuli yawakumba Omba Omba Dar es salaam

Kasi ya Rais Magufuli yawakumba Omba Omba Dar es salaam

Tarehe December 6, 2015
Omba omba katika moja ya eneo jijini Da res salaam.
Omba omba katika moja ya eneo jijini Da res salaam.
Kasi ya Rais John  Magufuli ime endelea kutikisa katika maeneo mbalimbali ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Ndugu Said Mecky Sadiki amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za jiji la Dar es Salaam, kuwaondoa ombaomba wote walioko katika barabara za jiji.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Sadiki  amesema kwamba utekelezaji wa kauli ya Rais John Magufuli ya kutumia siku ya Desemba 9 mwaka huu kufanya usafi, utakwenda sambamba na kuwaondoa ombaomba hao, ambao wanachangia kuongeza uchafu.
“Siwezi kusema wao ni uchafu lakini mazingira yanayowazunguka katika maeneo wanayofanyia shughuli zao wanayachafua, wanajisaidia kwenye mifuko na kutupa ovyo,” alisema.

Amesisitizia  Wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa ombaomba hao hawarudi mjini kutokana na kuwa na mazoea wakiondolewa kurudi tena katika maeneo hayo.
Licha ya timua timua hiyo kuwakumba  Omba omba wapiga debe  nao wameunganishwa katika kundi la watakao ondolewa  kufuatia kuwa kero kwa abiria.

Kasi ya Rais Magufuli yawatimua Vigogo 7 Tanecso

Kasi ya Rais Magufuli yawatimua Vigogo 7 Tanecso

Tarehe December 6, 2015
Makao makuu ya Shirika la Umeme Tanzania.
Makao makuu ya Shirika la Umeme Tanzania.
Kasi ya Rais John Pombe Magufuli ime endelea kushika kasi katika kuwashughulikia watendaji wazembe ambapo Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewatimua kazi  wafanyakazi 7 kutokana na makosa mbalimbali.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Tanesco imebainisha kuwa imewachukulia hatua wafanyakazi ambao wamekuwa wakitoa huduma  mbaya na kuwa Kero kwa wateja zikiwemo lugha mbaya, wateja kudaiwa rushwa kabla ya kupewa huduma, kucheleweshewa huduma na ubadhirifu.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa katika kipindi cha miezi miwili Shirika limewaachisha kazi maofisa 7 waandamizi kutokana na makosa mbali mbali ikiwemo wizi na ubadhirifu.
Aidha, Miongoni mwao ni wale waliofikishwa mahakamani kule Kagera na kuripotiwa na vyombo vya habari jana. Walioachishwa kazi ni pamoja na wafanyakazi wa ngazi za Mameneja, Wahandisi na Wahasibu.


Taarifa hiyo imesisitiza kuwa  Shirika linaendelea na uchunguzi na mfanyakazi ye yote atakayebainika analaghai wateja, anadai rushwa, anatoa lugha chafu au huduma mbovu atawajibishwa mara moja na pale atakabobainika    ataachishwa kazi.
Kwa upande mwingine shirika hilo limesema kwamba ili kuendana na agizo la Rais Magufuli la kufanya usafi Desemba 9 nchini Wafanyakazi wote wa TANESCO watashiriki katika shughuli mbali mbali za usafi wa mazingira katika maeneo yote yanayozunguka ofisi, mitambo na vituo nchi nchi nzima.

Makampuni 41 yatajwa ukwepa kodi Sakata la makontena 329

Makampuni 41 yatajwa ukwepa kodi Sakata la makontena 329

Tarehe December 6, 2015
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA,Phillip Mpango.
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA,Phillip Mpango.(katikati) akizungumza na wanahabari.
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA)  imeyataja majina ya kampuni 41 na wamiliki wa makontena 329 ambayo yalipitishwa bandarini bila kulipiwa ushuru.
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Dk. Philip Mpango alisema Mamlaka hiyo iliagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa kuchukua hatua mara moja kwa kufuatilia na kubaini wamiliki wa Bandari Kavu (ICD) zilizohusika katika kashfa hiyo.
Bidhaa zilizokuwemo ndani ya makontena hayo ni pamoja na matairi ya magari, samani mbalimbali, betri za magari, vifaa vya ujenzi, nguo na bidhaa zingine mchanganyiko.
Dk. Mpango aliyataja majina ya makampuni na watu binafsi na idadi ya makontena waliyopitisha bila kulipia ushuru ambayo ni kama ifuatavyo;

clouds stream