Saturday, 4 March 2017

Balozi wa Korea Kaskazini nchini Malaysia apewa saa 48 kuondoka nchini humo

Balozi wa Korea Kaskazini nchini Malaysia apewa saa 48 kuondoka nchini humo

Balozi wa Korea Kaskazini nchini Malaysia apewa saa 48 kuondoka nchini humo.
img-20161130-wa0008

Malaysia imemfukuza balozi wa Korea Kaskazini kuhusiana na kifo cha Kim Jong nam ,ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea kaskazini.

Kang Chol amepewa agizo la kuondoka nchini humo katika kipindi cha saa 48, alisema waziri wa maswala ya kigeni nchini humo.

Kim Jong nam ndugu wa kambo wa Kim Jong un ,alifariki wiki tatu baada ya wanawake 2 kumpaka kemikali ya sumu usoni mwake katika uwanja wa kuala Lumpur .

Malaysia haijailaumu Korea kaskazni kwa shambulio hilo lakini kuna shauku kwamba Pyongyang ilihusika.

Balozi wa Korea Kaskazini, Bwana Kang alitangazwa persona non grata{ hatakiwa nchini humo} siku ya Jumamosi baada ya kusema kuwa taifa lake haliweza kuamini uchunguzi uliofanywa na Malaysia na kwamba uchunguzi huo ulikuwa ukiingiliwa.

Ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim jong nam aliuawa katika njia za kutatanisha
Ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim jong nam aliuawa katika njia za kutatanisha

Waziri wa maswala ya kigeni wa Malaysia Anifah Aman alisema katika taarifa kwamba taifa lake linataka kuombwa msamaha na balozi huyo kwa matamashi yake lakini mwanadiplomasia huyo hakuomba msamaha.

''Malaysia itajibu matusi yoyote dhidi yake ama jaribio lolote la kutaka kuiharibia sifa'',alisema bwana Anifah.

Malaysia ni miongoni mwa mataifa machache yaliokuwa na urafiki na Korea Kaskazini.

Aliyetangaza ''afya ya Mugabe imedhoofika'' akamatwa

Rais Robert Mugabe

 Robert Mugabe
img-20161130-wa0008

Waandishi wawili wa Zimbabwe wamekamatwa kuhusiana na ripoti ya gazeti moja ilioelezea kwamba afya ya rais wa taifa hilo Robert Mugabe 'imedhoofika' alipoelekea nchini Singapore kwa kile afisi ya rais huyo ilisema ni zaira ya kimatibabu.

Muhariri wa gazeti la kibinafsi la NewsDay ,Wisdom Mudzungairi na mwandishi aliyeandika ripoti hiyo Richard Chidza hatahivyo wameachiliwa na ni sharti wajiwasilishe mahakamani.

Wakili wao Obey Shava amesema kuwa wameshtakiwa kwa kuhujumu na kutusi afisi ya rais.

Taarifa hiyo iliosema 'Mugabe yuko katika hali mbaya' ilinukuu duru zikisema kuwa rais huyo alisafirishwa kwa ndege siku ya Jumatano alfajiri.

Mugabe alisherehekea siku yake ya kuzaliwa ya mwaka 93 na amekuwa katika mamlaka tangu 1980.

Kulingana na chombo cha habari cha AP, watu wanaopatikana na hatia ya kumtusi Mugabe, uhudumia kifungo ijapokuwa kesi nyengine zimetupiliwa mbali.

Uhispania Yateua Waziri Wa ‘Ngono’, Kazi Yake Kubwa Hii Hapa

Bunge la Uhispania.
Bunge la Uhispania.
img-20161130-wa0008

Serikali ya Uhispania imeamua kuteua Waziri wa Masuala ya Ngono ikiwa ni katika juhudi za kuongeza idadi ya watu inayoendelea kupungua.

Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Mariano Rajoy amethibitisha uteuzi wa Edelmira Barreira kuwa Afisa Mkuu wa masuala ya ngono.

Hatua ya kubuni wizara nzima ya inayojihusisha na ngono na mahaba huko Uhispania imetokana na hofu waliyo nayo wanasiasa ya kupungua kwa idadi ya watu. 

Wakati kwengineko duniani watu wana hofu kwamba idadi ya watu nchini mwao inaongezeka kushinda rasilimali zilizopo huko Uhispania hofu ni kwamba idadi ya watu inapungua tena kwa kasi ya kutisha.

Takwimu za hivi karibuni za Umoja wa Mataifa zinaorodhesha Uhipania kama moja wapo ya mataifa yanayoongoza kwa kuporomoka kwa idadi ya watoto wanaozaliwa.

Naye Waziri wa Elimu hivi majuzi amewasilisha ripoti yake kwa Serikali na Baraza la Mawaziri akilalamika kwamba madarasa ya shule hayana idadi ya kutosha ya watoto na akaonya kwamba hili huenda likaathiri Uhispania kiuchumi katika miaka ijayo.

Kazi kubwa ya Waziri huyo mpya ni kuja na mbinu na mikakati ya kuwahamasisha na kuuchochea umma wa Uhispania kurudi vitandani na kusaidia kutengeneza watoto ili kuijaza tena Uhispania.


clouds stream