Wednesday, 5 July 2017

Sare Za JWTZ Zamponza Manji

Mfanyabiashara Yusuph Manji.
Mfanyabiashara Yusuph Manji.
IMG-20170426-WA0006

Mfanyabiashara Yusuph Manji na wenzake wamekamatwa kwa tuhuma za kukutwa na sare za Jeshi la Wananchi katika ghala la Quality Motors Group.

Mara baada ya kukamatwa waliombewa dhamana lakini ilikataliwa kwa sababu zisizojulikana. Kupitia hati ya kiapo, Wakili Gudson Ndusyepo amebainisha kuwa kukamatwa kwa walalamikaji sio halali kwa sababu kosa linalodaiwa dhidi yao linahusiana na masuala ya Kampuni ya Quality Motors ambayo inaongozwa na Wakurugenzi wake na Manji.

”Kama Wakili wa waombaji nimefuatilia suala la dhamana hadi sasa saa 48 zimeshapita tangu walipokamatwa, lakini hawajafikishwa Mahakamani. Jambo hilo ni kinyume na sheria.” alisema Wakili Ndusyebo.

Monday, 3 July 2017

Trump achapisha video 'akiipiga' CNN


A screenshot of the president's tweet
Video hiyo inaonekana kuchapishwa katika mtandao wenye kumpendelea Trump mapema wiki hii.
IMG-20170426-WA0006

Rais wa Marekani Donald Trump amechapisha video katika mtandao wa Twitter ikimuonyesha akimpiga mtu aliye na nembo kichwani ya shirika la habari la CNN.

Video hiyo iliyofanyiwa ukarabati ni ile inayomuonyesha Trump wakati alihudhuria michezo ya mieleka ya WWE mwaka 2007, ambapo 'alimshambulia' mmiliki wa michezo hiyo Vince McMahon.

Video hiyo inaonekana kuchapishwa katika mtandao wenye kumpendelea Trump mapema wiki hii.

CNN baadaye ilimlaumu Rais kwa kuibua ghasia dhidi ya vyombo vya habari.

Donald Trump gets taken to the mat by 'Stone Cold' Steve Austin after the the Battle of the Billionaires at the 2007 World Wrestling Entertainment's Wrestlemania April 1, 2007 at Ford Field in Detroit, Michigan.
Video hiyo inaonekana kuchapishwa katika mtandao wenye kumpendelea Trump mapema wiki hii.

Mchambuzi mmoja katika kituo cha ABC Ana Navarro, ambaye ni mkosoaji mkubwa wa Trump, alisema kuwa video hiyo ni uchochezi na huenda ikasababisha mwandishi kuuliwa.

Lakini mshauri wa masuala ya usalama nchini Marekani Thomas Bosset, ambaye awali alihojiwa na kituo cha ABC alisema video hiyo haionekani kuwa tisho.

Mara kwa mara Rais Trump amekuwa kwenye mzozo na kituo cha CNN anachokiita 'taarifa bandia'

China: Hatua ya meli ya Marekani kukaribia kisiwa ni uchokozi mbaya

The USS Stetham, in a photo from 2015, arrives at a port in Shanghai

Meli USS Stetham
IMG-20170426-WA0006

China imetaja hatua ya manowari ya Marekani kupita karibu na kisiwa kinachozozaniwa kusinia mwa bahari ya China kuwa uchokozi mbaya wa kisiasa na kijeshi.

Manowari ya USS Stethem ilipita karibu na kisiwa kinachozozaniwa cha Triton ambacho ni moja ya visiwa vinavyodaiwa na China na nchi zingine,

Uchina ilijibu kwa kutuma meli za kijeshi na ndege kuenda kisiwa hicho.

Kisa hicho kilitokea muda kabla ya viongozi wa nchi hizo mbili kufafanya mazungumzo ya simu.Map

Eneo la kusini mwa China

Marekani mara kwa mara imeionya China dhidi ya hatua yake ya kunyakua visiwa katika maeneo yanayozozaniwea, lakini china inasema inafanya hivyo kuambatana na haki zake.

China inasema kuwa itafanya kila iwezalo kulinda usalama wake.

Pia imeilaumu Marekani kwa kuchochea vurugu eneo hilo kwa kuwa uhusiano kati ya China na majirani wake wa kusini mwa bahari ya China umeboreka.

Kisiwa hicho kidogo pia kinadaiwa na Vietnam na Taiwan. China imekuwa kwenye mzozo wa umiliki wa maeneo ya bahari na majirani zake kadha miaka ya hivi karibuni.

clouds stream