Monday, 27 March 2017

Uholanzi yamtimua kocha wa timu ya taifa

Danny Blind ni baba wa mlinzi wa Man United Daley Blind

Danny Blind ni baba wa mlinzi wa Man United Daley Blind
img-20161130-wa0008

Uholanzi imemtimua kocha wa timu yake ya taifa Danny Blind baada ya kudumu kwa takriban miaka miwili.

Hii inafuatia kichapo cha magoli 2-0 dhidi ya Bulgaria siku ya Jumamosi na kuwaacha Uholanzi katika nafasi ya nne kwenye mbio za kufuzu kushiriki kombe la dunia.

Blind mwenye miaka 55 alichukua nafasi hiyo kutoka kwa Guus Hiddink mwaka 2015 huku ikishuhudiwa kikosi chake kikishindwa kufuzu fainali za michuano ya Ulaya mwaka jana.

Chama cha soka nchini Uholanzi kimesema kuwa ameicha timu hiyo katika wakati mgumu kufuzu kucheza kombe la dunia nchini Urusi.

Fred Grim ameteuliwa kuwa kocha wa mpito na atakiongoza kikosi hicho siku ya Jumanne dhidi ya Ufaransa.

Wasichana waliovalia suruali za kubana wazuiwa kuabiri ndege ya United Airlines Marekani

Ndege za United Airlines

Shirika hilo la ndege limeshutumiwa sana kwenye Twitter
img-20161130-wa0008

Shirika la ndege la United Airlines nchini Marekani limeshutumiwa sana baada ya kudaiwa kuwazuiwa wasichana wawili waliokuwa wamevalia suruali ndefu za kubana kuabiri ndege hiyo.

Kisa hicho kilitokea kwenye safari ya ndege iliyokuwa ikitokea Denver kuelekea Minneapolis Jumapili asubuhi, mwanaharakati Shannon Watts amesema.

Shirika la United limesema wasichana hao walikuwa wanasafiria hati maalum, ambayo hutumiwa na wafanyakazi wa shirika la ndege na wageni wao.

United wamesema huwa kuna kanuni za mavazi kwa wanaotumia hati hiyo kusafiria.

Shirika hilo limefafanua kwamba abiria wa kawaida, ambao wanalipia tiketi zao, wako huru kuvalia mavazi yao ya kubana.

Hati hiyo maalum ya kusafiria ya United huwawezesha walio na hati hiyo kusafiri kwa ndege bila malipo au kwa tiketi za bei nafuu sana.

Kanuni za mavazi kwa wanaotumia hati hiyo huel

UN yalaani mauaji ya watoa misaada Sudan Kusini

Wafanyakazi 12 wa mashirika ya kutoa misaada wameuawa mwaka huu pekee

Wafanyakazi 12 wa mashirika ya kutoa misaada wameuawa mwaka huu pekee
img-20161130-wa0008

Umoja wa mataifa umelaani vikali mauaji ya wafanyakazi sita wa kutoa misaada nchini Sudan Kusini.

Miongoni mwa waliouawa ni raia watatu kutoka Kenya, na watatu kutoka Sudan Kusini ambao walitekwa siku ya Jumamosi walipokuwa wakisafiri kutoka mji mkuu Juba kwenda mji wa Pibor.

Hili ni tukio la tatu la aina hiyo ndani ya mwezi mmoja likiwa limepoteza maisha ya watu wengi tokea kuanza kwa mgogoro huo mwaka 2013.

Mkuu wa mashirika ya kibinaadam nchini Sudan Kusini Eugene Owusu ameelezea mauaji hayo kama uhalifu wa kutisha.

Wafanyakazi 12 wa mashirika ya kutoa misaada waneuawa mwaka huu, wakati huu ambapo wanajaribu kuelekea sehemu ambazo umaskini ni mkubwa kutokana na vita.

clouds stream