Showing posts with label burudani. Show all posts
Showing posts with label burudani. Show all posts

Friday, 27 October 2017

JAHAZI LAKAMATWA LIKISAFIRISHA HEROIN YA BILIONI 5




Dawa za kulevya aina ya Heroini.



Maofisa wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama wamekamata zaidi ya kilo 100 za madawa ya kulevya aina ya Heroin zenye thamani ya Shilingi bilioni 5 zilizokuwa zikisafirishwa kwenye jahazi kutoka Unguja kwenda Dar es Salaam.

Kamishna wa Sheria wa DCEA, Edwin Kakolaki amesema hatua hiyo ilifikiwa baada ya maofisa hao kutilia shaka jahazi hilo ambalo ndani yake lilikuwa na raia kumi wa Iran na Wazanzibari wawili.
“Paketi 104 za madawa ya kulevya yanayoshukiwa kuwa ni heroin zilikamatwa katika jahazi hilo na kupelekwa kwa Mkemia Mkuuwa Serikali kwa vipimo zaidi,” amesema.

Amesema hadi jana jioni walikuwa wamefanya upekuzi kwa kusaidiana na mbwa maalum wa kunusa ili kuona kama kuna mzigo zaidi katika jahazi hilo.

Naye Kamishna Mkuu wa DCEA, Rodgers Siang’a amesema kiwango cha dawa hizo kingekuwa kikubwa zaidi kama sio kitendo cha watu hao kutupa kiasi kingine baharini baada ya kuzidiwa nguvu walipozungukwa na vyombo vya ulinzi na usalama.

“Vyombo vya dola viko imara kupambana na usafirishaji wa dawa za kulevya na hatutaacha kuyadhibiti magenge na mitandao yao,” amesema Siang’a.

Hatahivyo, upekuzi huo haukukamilika kutokana na hali ya mvua ambapo unatarajiwa kuendelea leo huku taratibu za kwenda kwa Mkemia Mkuu wa Serikali zikikamailika, watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani.

Tuesday, 24 October 2017

Buffon achukua nafasi ya Neuer kikosi bora cha Fifa

Gianluigi Buffon


Gianluigi Buffon ameshinda Serie A mara kumi



Shirikisho la soka duniani Fifa limetangaza kikosi bora cha soka ya wanaume duniani mwaka 2017 ambapo kuna mabadiliko matatu kutoka kwa kikosi kilichotangazwa mwaka 2016.

Kwenye kikosi hicho, maarufu kama Fifpro World XI, mlindalango Gianluigi Buffon amechukua nafasi ya Manuel Neuer, naye beki wa AC Milan Leonardo Bonucci akachukua nafasi ya kigogo wa Barcelona Gerard Pique kwenye safu ya ulinzi.

Mshambuliaji wa PSG Neymar, ambaye ndiye mchezaji ghali zaidi duniani naye ameingia nafasi ya Luis Suarez katika safu ya mashambulizi.

Kikosi hicho kina wachezaji watano kutoka Real Madrid, wawili wa Barcelona, wawili wa PSG, mmoja wa Juventus na mmoja kutoka AC Milan.

Hakuna mchezaji hata mmoja wa Ligi ya Premia aliyefanikiwa kujumuishwa katika kikosi hicho.

Fifpro World XI

Mkufunzi bora duniani soka ya wanaume

Zinedine Zidane amemshinda meneja wa Chelsea Antonio Conte baada ya kuongoza Real Madrid kushinda La Liga msimu uliopita kwa mara ya kwanza tangu 2012 na kushinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mtawalia msimu uliopita.

Conte alishinda Ligi ya Premia msimu uliopita.
Massimiliano Allegri wa Juventus, ambaye aliongoza klabu yake kushinda Serie A na Coppa Italia msimu uliopita alikuwa wa tatu.

Mkufunzi bora soka ya wanaume
Zinedine Zidane - 46.22%Antonio Conte - 11.62%Massimiliano Allegri - 8.78%

Mkufunzi bora duniani soka ya wanawake

Kocha wa Uholanzi Wiegman aliyeongoza Uholanzi kushinda Euro 2017 nyumbani kwao amechukua taji hilo.Waliwalaza Denmark kwenye fainali.

Sarina Wiegman akipokea taji lake
Sarina Wiegman akipokea taji lake

Mkufunzi bora wa soka ya wanawake
Sarina Wiegman - 36.24%Nils Nielsen - 12.64%Gerard Precheur - 9.37%
   

Kipa bora zaidi

Mshindi wa Kombe la Dunia na mshindi wa Serie A mara 10 Gianluigi Buffon ndiye mshindi wa tuzo ya mlindalango bora duniani mwaka huu.

Aliwasaidia Juventus kushinda taji la ligi mara ya sita mtawalia msimu uliopita.
Aidha, alicheza dakika 600 Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya bila kufungwa.

Buffon, 39, amewashinda kipa Keylor Navas, wa Real Madrid na Manuel Neuer wa Bayern Munich.
"Ni heshima kubwa sana kwangu kupokea tuzo hii katika umri wangu huu," alisema Buffon.

Uchezaji haki

Mchezaji wa Togo Francis Kone, ambaye alimfanyia huduma ya dharura kipa wa Bohemians 1905 Martin Berkovec uwanjani wakati wa mechi ya ligi Jamhuri ya Czech mwezi Februari ametunukiwa tuzo ya uchezaji wa haki.

Monday, 23 October 2017

Arsenal yainyoa bila maji Everton 5-2

Mesut OzilMesut Ozil alifunga bao la kwanza la Arsenal
Everton ilishuka katika ligi kuu baada ya kutandikwa mabao 5-2 na Arsenal katika uga wa Goodison Park.

Nacho Monreal, Mesut Ozil, Alexandre Lacazette na Aaron Ramsey waliifungua Arsenal huku naye Wayne Rooney aliwafungia Everton bao lao la kwanza.

Oumar Niasse alifungua Everton bao la pili kabla ya Alexis Sanchez kuiongezea Arsenal bao la tano.

Wayne Rooney
Rooney aliifungia Everton bao la kwanza

Idrissa Gueye alitimuliia uwanjani baada ya kuonyeshwa kadi ya njano mara mbili wakati Everton walikuwa chini kwa mabao 2-1.

Ushindi huo wa Arsenal ugenini uliipandisha ngazi juu ya Watford hadi nafasi ya tano katika jedwali huku Everton wakiwa hawajashinda katika mechi tano.

Sanchez
Sanchez aliongezea Arsenal bao la tano

Monday, 25 September 2017

Alexander Lacazette Shujaa wa Arsenal

Alexandre LacazetteMshambuliaji mpya wa klabu ya Arsenal Alexandre Lacazette

Mshambuliaji mpya wa klabu ya Arsenal Alexandre Lacazette jana jumatatu usiku alifanikiwa kuifungia mabao 2 - 0 dhidi ya West Bromwich Albion katika mchezo wa Ligi kuu ya England , kwa bao la dakika ya 20 kipindi cha kwanza na bao lingine la dakika ya 67 kipindi cha alilofunga kwa njia ya penati.

Alexandre Lacazzete mpaka sasa amevunja rekodi ya Brian Marwood iliyowekwa mwaka 1988 ya kufunga katika michezo mitatu ya mwanzo ya ligi ya Epl. Kwa matokeo hayo yanawafanya Arsenal kubaki katika nafasi ya saba ya msimamo wa ligi kuu Uingereza wakiwa na alama zao 10 huku Manchester City wakiwa kileleni.

Tuesday, 22 August 2017

Everton yaivuta shati Man City nyumbani

EPL

Wayne Rooney amefikisha jumla ya magoli 200 katika ligi kuu ya nchini England
IMG-20170426-WA0006

Matajiri wa jiji la Manchester klabu ya Man city,imeshindwa kutamba katika uwanja wake wa nyumbani wa Etihad baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Everton.

Everton almaarufu kama The Toffes, ndio walianza kuzifumania nyavu za Man City, kwa goli lilifungwa na mshambuliaji Wayne Rooney, Rooney amefikisha idadi ya magoli 200 katika michezo ya ligi kuu nchini England.

Katika dakika ya 82 Man City, walisawazisha goli hilo kupitia kwa winga Raheem Sterling aliyefunga kwa shuti kali lililomshinda golikipa wa Everton, Jordan Pickford.

EPL
Raheem Sterling akipiga shuti lililokwenda moja kwa moja nyavuni

Mchezo huo ulimalizika kwa timu zote kubakia na wachezaji kumi baada ya beki wa City Kyle Walker, na kiungo wa Everton Morgan Schneiderlin, kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kila mmoja kuonyeshwa kadi mbili za njano.

Thursday, 17 August 2017

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

IMG-20170426-WA0006

Kwa mara nyengine Real Madrid imeilaza Barcelona 2-0 katika uwanja wa nyumbani wa Bernabeu na kuibuka mshindi kwa jumla ya mabao 5-1 na hivyobasi kushinda kombe la Super Cup.

Mabingwa hao wa Uhispania na Ulaya walitawala mechi hiyo licha ya kutoshoriki kwa nyota wao Cristiano Madrid.

Marco Asensio ambaye pia alifunga katika ushindi wa mechi ya kwanza huko Barcelona aliwapatia mabingwa hao uongozi wa mapema kupitia mkwaju wa maguu 25.

Karim Benzema aligusa kwa uhodari pasi nzuri iliopigwa na Marcelo na kumwezesha Samuel Umtiti kufunga bao la pili huku ikiwa wazi kwamba Barcelona wasingeweza kusawazisha.

Real Madrid ilicheza mechi hiyo kwa urahisi mkubwa huku Barca wakifanya mashambulio kupitia Lionel Messi na Suarez yaliogonga mwamba wa goli.

Akiwa kocha wa timu hiyo kwa miaka miwili pekee Zinedine Zidane ameiongoza Real Madrid kushinda mataji mawili ya vilabu bingwa na taji la La liga la 2016-17.

Na kufuatia ushindi huo ni wazi kwamba haitakuwa rahisi kwa timu nyengine kuwabwaga mabingwa hao msimu huu.

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

IMG-20170426-WA0006

Kwa mara nyengine Real Madrid imeilaza Barcelona 2-0 katika uwanja wa nyumbani wa Bernabeu na kuibuka mshindi kwa jumla ya mabao 5-1 na hivyobasi kushinda kombe la Super Cup.

Mabingwa hao wa Uhispania na Ulaya walitawala mechi hiyo licha ya kutoshoriki kwa nyota wao Cristiano Madrid.

Marco Asensio ambaye pia alifunga katika ushindi wa mechi ya kwanza huko Barcelona aliwapatia mabingwa hao uongozi wa mapema kupitia mkwaju wa maguu 25.

Karim Benzema aligusa kwa uhodari pasi nzuri iliopigwa na Marcelo na kumwezesha Samuel Umtiti kufunga bao la pili huku ikiwa wazi kwamba Barcelona wasingeweza kusawazisha.

Real Madrid ilicheza mechi hiyo kwa urahisi mkubwa huku Barca wakifanya mashambulio kupitia Lionel Messi na Suarez yaliogonga mwamba wa goli.

Akiwa kocha wa timu hiyo kwa miaka miwili pekee Zinedine Zidane ameiongoza Real Madrid kushinda mataji mawili ya vilabu bingwa na taji la La liga la 2016-17.

Na kufuatia ushindi huo ni wazi kwamba haitakuwa rahisi kwa timu nyengine kuwabwaga mabingwa hao msimu huu.

Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup


Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup
Real Madrid yailaza Barcelona na kushinda kombe la Super Cup

IMG-20170426-WA0006

Kwa mara nyengine Real Madrid imeilaza Barcelona 2-0 katika uwanja wa nyumbani wa Bernabeu na kuibuka mshindi kwa jumla ya mabao 5-1 na hivyobasi kushinda kombe la Super Cup.

Mabingwa hao wa Uhispania na Ulaya walitawala mechi hiyo licha ya kutoshoriki kwa nyota wao Cristiano Madrid.

Marco Asensio ambaye pia alifunga katika ushindi wa mechi ya kwanza huko Barcelona aliwapatia mabingwa hao uongozi wa mapema kupitia mkwaju wa maguu 25.

Karim Benzema aligusa kwa uhodari pasi nzuri iliopigwa na Marcelo na kumwezesha Samuel Umtiti kufunga bao la pili huku ikiwa wazi kwamba Barcelona wasingeweza kusawazisha.

Real Madrid ilicheza mechi hiyo kwa urahisi mkubwa huku Barca wakifanya mashambulio kupitia Lionel Messi na Suarez yaliogonga mwamba wa goli.

Akiwa kocha wa timu hiyo kwa miaka miwili pekee Zinedine Zidane ameiongoza Real Madrid kushinda mataji mawili ya vilabu bingwa na taji la La liga la 2016-17.

Na kufuatia ushindi huo ni wazi kwamba haitakuwa rahisi kwa timu nyengine kuwabwaga mabingwa hao msimu huu.

Wednesday, 9 August 2017

Ifahamu Simba SC Na Simba Day

Nembo ya Simba
Nembo ya Simba
IMG-20170426-WA0006
Klabu ya Simba ina majina mbalimbali ya utani kama vile ‘Wekundu wa Msimbazi’ na ‘Lunyasi’ na ina makao yake makuu katika mtaa wa Msimbazi jijini Dar es Salaam.
Timu hii ilianzishwa mwaka 1936 jijini Dar es Salaam ikitumia jina la Queens lakini baadaye lilibadilisha jina na kuitwa Eagle kabla ya kubadilishwa tena na kuitwa Sunderland –jina lililotumika hadi mwaka 1971 ambapo ndipo jina la Simba Sports Club lilianza kutumika.
Ingawa tayari jina la Sunderland lilikuwa maarufu na kubwa tayari, lilibadilishwa na kuwa Simba; jina la mfalme wa msituni, ikiwa ni kutokana na pendekezo la aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume, ambaye alishauri jina libadilishwe wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa jengo la makao makuu ya klabu mtaa wa Msimbazi.
Katika majina yaliyopendekezwa, jina la Simba lilikubaliwa zaidi na wengi na likaamuliwa kutumika kuanzia mwaka huo wa 1971. Simba ilianza kutanuka zaidi wakati ikitumia jina la Sunderland.
Ilikuwa na matawi yake katika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam ambapo ziliundwa timu zilizokuwa na kazi ya kupika wachezaji waliokuja kuchezea Simba baadaye. Miongoni mwa timu hizo ni Morning Stars, Canada Dry, Liverpool na Ilala Stuff, ambako huko mchezaji aliyeonekana kukomaa alipelekwa kukipiga Sunderland.
Klabu hiyo iliona ni vema ikaanzisha siku ya kuwakutanisha mashabiki wake kabla msimu mpya wa ligi haujaanza ili kuweza kufanya mambo mbalimbali ikiwamo kutambulisha jezi, wachezaji wao.
Ndipo kile kinachofahamika kwa sasa kama ‘Simba Day’ kilipoanzishwa kwa ajili hiyo mashabiki hukutana kila Agosti 8 kila mwaka kwa ajili ya tukio hilo.
Kunogesha siku hiyo huchezwa mechi na wageni kutoka mipaka ya Tanzania ili kuleta burudani tosha, pia kuwa sehemu ya maandalizi ya kikosi kwa ajili ya msimu mpya.
Simba Day ya kwanza iliadhimishwa Agosti 8, 2009 jijini Dar es Salaam.Haruna Niyonzima akiwa na Jackson Mayanja. Ni miongoni mwa wachezaji watakaotambulishwa Agosti 8, 2017 kuwa miongoni mwa wachezaji wa Simba.
Haruna Niyonzima akiwa na Jackson Mayanja. Ni miongoni mwa wachezaji watakaotambulishwa Agosti 8, 2017 kuwa miongoni mwa wachezaji wa Simba.
Simba Day 2009 (Uhuru Stadium)
Simba ilicheza na SC Villa ya Uganda. Ilikuwa mechi ya kwanza kusheherekea siku yao ya kumbukumbu waliwatendea haki mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo kwa ushindi mwembamba wa bao 1-0 lililofungwa na Hillary Echesa. Kocha alikuwa raia wa Zambia Patrick Phiri. Msimu huo Simba ilimaliza bila kupoteza mchezo wowote.
Simba Day 2010 (Uhuru Stadium)
Langoni alisimama Ally Mustafa ‘Barthez’ akilindwa na Haruna Shamte, Juma Nyosso, Amri Kiemba, Juma Nyosso, Amri Maftah dhidi ya Express ya Uganda. Mchezo huo uliochezwa dimba la Uhuru ulimalizika kwa sare tasa.
Simba Day 2011 (Sheikh Amri Abeid, Arusha)
Simba iliambulia kichapo cha bao 1-0 kutoka kwa Victors ya nchini Uganda. Mchezo huo ulichezwa katika dimba la Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Patrick Sembuya aliukwamisha mpira wavuni na kuwaacha Simba wakiwa vichwa chini.
Simba Day 2012 (Uwanja wa Taifa)
Ikiongozwa na Juma Kaseja, Felix Sunzu, Haruna Moshi ‘Boban’, Uhuru Selemani na wengineo walikubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Nairobu City ya Kenya. Bao pekee la Simba SC lilifungwa na Sunzu huku ya wageni yakitupiwa na Duncan Owiti, Bruno Okullu, Boniface Onyango. Wakati huo Simba ilikuwa ikinolewa na kocha wa Serbia Milovan Cirkovic.
Simba Day 2013 (Uwanja wa Taifa)
SC Villa walipata nafasi kwa mara nyingine tena kurudi katika ardhi ya Tanzania katika Simba Day ambapo waliamulia kichapo cha mabao 4-1. Waliopeleka kilio hicho kwa Villa walikuwa ni Jonas Mkude, William Gallas na Betram Mwombeki alitupia mawili. Kikosi cha Simba kilikuwa kinanolewa Mtanzania Abdallah Kibadeni.
Simba Day 2014 (Uwanja wa Taifa)
Zesco ya Zambia iliwazabua Simba SC mabao 3-0 katika Simba Day. Waliopeleka kilio Msimbazi ni Jackson Mwanza katika dakika ya 14, Clatos Chane katika dakika 64 na katika dakika ya 90 Mayban Mwaka alipigilia msumari wa mwisho. Simba ilikuwa mikononi mwa kocha Zdravko Logarusic.
Simba Day 2015 (Uwanja wa Taifa)
Bao pekee la Simba lilifungwa na Awadhi Juma katika dakika ya 89 dhidi ya SC Villa ambao walipata nafasi ya kurudi tena kupambana na Simba. Kinachokumbukwa katika siku hiyo ni pale mashabiki waliokuwa wakianza kuondoka kwani walijua fika kuwa wameambulia patupu.
Simba Day 2016 (Uwanja wa Taifa)
Ilikuwa ikiadhimisha miaka 80 tangu kuanzishwa kwake. AFC Leopards ya Kenya ilikubali mwaliko dhidi ya Simba SC, ambapo walijipatia ushindi mnono wa mabao 4-0. Ibrahim Ajibu alitupia mawili, Jamal Mnyate na Shiza Kichuya. Siku hiyo mshambuliaji wa Ivory Coast Fredrick Blagnon na mlinzi wa kati Method Mwanjali wa Zimbabwe walitambulishwa.
Simba Day 2017 (Uwanja wa Taifa)
Mwaka huu wanacheza na Rayon Sport ya Rwanda wachezaji zaidi ya 10 watatambulishwa akiwamo Haruna Niyonzima, Emmanuel Okwi, John Bocco, Aishi Manula.

Wednesday, 2 August 2017

Jurgen Klopp: Liverpool itashinda ligi ya Uingereza

Jurgen Klopp asema Liverpool inalennga kushinda ligi ya Uingereza

Jurgen Klopp asema Liverpool inalennga kushinda ligi
ya Uingereza

IMG-20170426-WA0006


Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp anasema kuwa kikosi chake kinaweza kushinda ligi baada ya bahati mbaya ya msimu uliopita.

Liverpool ilianza msimu wa 2016-17 vizuri na walikuwa pointi sita pekee nyuma ya viongozi na hatimaye bingwa wa ligi Chelsea mnamo mwezi Januari.

Lakini walirudi nyuma baada ya kupata ushindi mmoja mwezi Januari na Februari kabla ya kumaliza katika nafasi ya nne pointi 17 nyuma ya Chelsea.

''Tutashiriki mechi za ubingwa.hatutaki kuanza msimu bila kuwa na lengo lolote'', alisema Klopp.

"Lazima tuwe na lengo na nadhani tuna timu nzuri sana sasa.tulikuwa na bahati mbaya msimu uliopita''.

''Nadhani tunaweza kucheza vyema .Tuwe na matumaini kwamba kila kitu kitakuwa shwari. Klop alisema kuwa kwamba mchezaji Phillipe Coutinho hauzwi, licha ya Barcelona kumtaka''.

Thursday, 6 July 2017

Zambia kucheza fainali ya Cosafa na Zimbabwe

COSAFA

Wachezaji wa Tanzania wenye jezi nyeupe Himid Mao na Mzamiru Yassin wakikabwa na mchezaji wa Zambia
IMG-20170426-WA0006

Timu ya taifa ya Tanzania taifa stars imeshindwa kusonga mbele kwenye hatua ya fainali baada ya kuchapwa kwa mabao 4-2 na Zambia Chipolopolo katika mchezo wa nusu fainali ya michuano ya Cosafa.

Beki Erasto Nyoni alianza kuipatia Taifa Stars bao la kuongoza katika dakika ya 14, lakini katika dakika ya 44 Brian Mwila, akasawazisha goli hilo, dakika moja baadae Justin Shonga akaifungia Zambia goli la pili.

Kipindi cha Pili, dakika ya 56 Chipolopolo wakaongeza goli la tatu kupita kwa Chirwa aliyefunga kwa mkwaju wa penati, Justin Shonga akahitimisha kazi kwa goli la nne katika dakika ya 68.

Winga Simon Msuva aliipatia Stars goli la pili katika dakika ya 84, mchezo wa mshindi wa tatu utazikutanisha Tanzania na Lesotho ambao walifungwa na Zimbabwe kwa mabao 4-3.

Mchezo wa fainali utachezwa Jumapili ya Julai 9 kwa Zambia kukipiga na Zimbabwe

Lacazette asaini mkataba wa miaka mitano Arsenal

Arsenal

Alexandre Lacazette

IMG-20170426-WA0006

Klabu ya Arsenal imekamilisha usajili wa mshambuliaji Alexandre Lacazette toka timu ya Lyon kwa dau la pauni Milioni 52.6 na kuvunja rekodi ya usajili ya timu hiyo.

Usajili wa kiungo wa Kijerumani Mesut Ozil ndio ulikua usajili wa bei ghali zaidi klabuni hapo aliposajiliwa mwaka 2013, kutokea Real Madrid kwa dau la pauni 42.4.

Lacazette amesaini mkataba wa miaka mitano kuwatumika washika mitutu hao wa London, mshambuliaji huyu atasafiri na timu wikiendi hii kuelekea Sydney kwa ajili ya michezo miwili ya kirafiki.

Msimu uliopita, Lacazette alikuwa mfungaji bora wa ligi ya Ufaransa alikozipasia nyavu mara 28 na ameshapiga jumla ya mabao 129 katika mechi 275 tangu alipoanza kuichezea timu ya kwanza msimu wa 2009/10.

Tuesday, 27 June 2017

Meya Jacob: Kutoa Bango La Mtaa Wa Victor Wanyama Ni Siasa Chafu

Meya Manispaa ya Ubungo, Boniphace Jacob.
Meya Manispaa ya Ubungo, Boniphace Jacob.
IMG-20170426-WA0006

Meya wa Manispaa ya Ubungo, Boniface Jacob amesema kuwa mpango wa kuondolewa kwa bango la Mtaa wa Mchezaji wa Soka wa Ligi Kuu Nchini Uingereza, Victor Wanyama ni mpango ulioratibiwa kwa chuki za kisiasa dhidi yake.

Amesema kuwa aliyeratibu mpango huo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa madai kuwa anahakiki kama taratibu za kuupa jina Mtaa Wanyama zilifuatwa ama hapana.

Amedai kuwa kitendo hicho kimedhihirisha chuki kutokana na dalili za uwepo wa Meya huyo wa Chadema katika mchakato wa kuupa mtaa huo jina la Mchezaji Wanyama ambaye yupo nchini kwa Matembezi.

Meya Jacob amesema kuwa mchezaji huyo ambaye pia ni nahodha wa timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’ aliyekubali kushiriki kuangalia ligi ya Ndondo Cup alionesha nia ya kuwasaidia vijana wa kitanzania wenye hamasa ya kucheza soka lenye tija.

“Kitendo hicho ambacho si cha kiuungwana kinaweza kumkatisha tamaa mchezaji huyo ambaye angeweza kuwa rafiki mzuri wa Tanzania na kupata mafanikio kupitia mlango wa soka,” amesema.

Jacob amefafanua kuwa taratibu zote za kuupa mtaa huo jina zilipitiwa.Victor Wanyama akizindua mtaa uliopewa jina lake katika Manispaa ya Ubungo.

Victor Wanyama akizindua mtaa uliopewa jina lake katika Manispaa ya Ubungo.

19510085_1500322923344454_861370004019848212_n
19399009_1500322866677793_8835901741559392841_n

Tuesday, 6 June 2017

Cheick Tiote: Mchezaji wa zamani wa Newcastle afariki dunia

Cheick Tiote

Cheick Tiote alichezea Newcastle mechi 156 mashindano yote.
IMG-20170426-WA0006

Kiungo wa zamani wa timu ya Newcastle United Cheick Tiote amefariki dunia akiwa an miaka 30 baada ya kuzimia wakati wa mazoezi nchini China, msemaji wa mchezaji huyo amesema.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alikaa miaka saba Newcastle na kuwachezea mechi 138 ligini.

Alihamia klabu ya Beijing Enterprises mwezi Februari.

"Ni kwa huzuni kubwa ambapo ninathibitisha kwamba Cheick Tiote alifariki mapema leo baada ya kuzimia wakati wa mazoezi," msemaji wake alisema.

"Hatuwezi kusema zaidi kwa sasa na tunaomba kwamba familia yake iheshimiwe kipindi hiki kigumu. Tunaomba maombi yenu."

Tiote alizaliwa Ivory Coast na alikuwa kwenye kikosi kilichoshinda Kombe la Mataifa ya Afrika 2015.

Sunday, 28 May 2017

Simba SC Bingwa Kombe La ASFC

Wachezaji na viongozi wa Simba SC wakifurahia taji a Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania Bara (ASFC) msimu wa 2016/17
IMG-20170426-WA0006
Wachezaji na viongozi wa Simba SC wakifurahia taji a Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania Bara (ASFC) msimu wa 2016/17.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akimkabidhi Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (ASFC), Nahodha wa klabu ya Simba SC Jonas Mkude baada ya kuitandika Mbao FC kwa mabao 2-1 baada ya muda wa nyongeza.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Harrison Mwakyembe akimkabidhi Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (ASFC), Nahodha wa klabu ya Simba SC Jonas Mkude baada ya kuitandika Mbao FC kwa mabao 2-­1 baada ya muda wa nyongeza.
Nahodha wa Simba SC Jonas Mkude akipokea hundi ya Shilingi milioni 50 ikiwa ni zawadi ya bingwa wa ASFC
Nahodha wa Simba SC Jonas Mkude akipokea hundi ya Shilingi milioni 50 ikiwa ni zawadi ya bingwa wa ASFC.
Mkwaju wa penalti wa Shiza Kichuya katika muda wa nyongeza ulioipa taji kabla yake mbele ya Mbao FC kwa mabao 2-1.
Mkwaju wa penalti wa Shiza Kichuya katika muda wa nyongeza ulioipa taji kabla yake mbele ya Mbao FC kwa mabao 2-­1.
Shiza Kichuya akiiunuliwa juu baada ya ushindi huo.
Shiza Kichuya akiinuliwa juu baada ya ushindi .
Shabiki wa Simba akiwa na msumeno bandia ulioandikwa maneno ya kuisuta Mbao FC
Shabiki wa Simba akiwa na msumeno bandia ulioandikwa maneno ya kuisuta Mbao FC.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akifuatilia fainali hizo.
Waziri mkuu Kassim Majaliwa akifuatilia mpambano huo.
Mshambuliaji wa Ivory oast Fredrick Blagnon aliyetokea benchi na kuipa Simba SC bao la kuongoza akishangilia.
Mshambuliaji wa Ivory oast Fredrick Blagnon aliyetokea benchi na kuipa Simba SC bao la kuongoza akishangilia.
Wafungaji wa mabao wa Simba SCBlagnon na Kichuya wakipongezana baada ya kazi nzito.
Wafungaji wa mabao wa Simba SCBlagnon na Kichuya wakipongezana baada ya kazi nzito.
Fainali za ASFC msimu wa 2016/17 upande wa mashabiki
Upande wa mashabiki.
Manyika
Mlinda mlango chaguo la tatu la Simba SC Peter Manyika Jr akiwafariji wachezaji wa Mbao FC baada ya kumalizika kwa fainali.

DAVID BECKHAM YUKO NCHINI KWA AJILI YA UTALII

IMG-20170426-WA0006
 Kiungo nyota wa zamani wa Manchester United, David Beckham yupo nchini kwa ajili ya shughuli za utalii.

Beckham akiwa na familia yake, ametua nchini jana usiku na leo huenda akaingia mbugani kwa ajili ya shughuli za utalii.

Raia huyo wa England ambaye pia aliwahi kutamba na Real Madrid, AC Milan na LA Galaxy alionekana yuko chini ya uangalizi wa wenyeji wake alipotua.

clouds stream