Tuesday, 2 August 2016

Sabodo Akoshwa Na Magufuli, Asitisha Misaada Chadema


Tarehe August 2, 2016Mfanyabiashara maarufu, Mustapha Jaffer Sabodo wakati alipomkabidhi Mwenyekiti Chadema hundi ya Fedha kusaidia kuimarisha Demokrasia.
Mfanyabiashara maarufu, Mustapha Jaffer Sabodo wakati alipomkabidhi Mwenyekiti Chadema hundi ya Fedha kusaidia kuimarisha Demokrasia. Mfanyabiashara maarufu, Mustapha Jaffer Sabodo ametangaza rasmi kusitisha kukisaidia fedha chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kufuatia kukoshwa na utendaji wa Rais Dkt John Pombe Magufuli.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dares salaam jana , Sabodo alisema atawekeza dola za Marekani bilioni 5 (Sh trilioni 10) mkoani Dodoma, ikiwa ni njia ya kumuunga mkono Rais John Magufuli kuhamisha makao makuu ya serikali kwenda mkoani humo.
 “Huko nyuma nilikuwa nawapa Chadema fedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo na kuimarisha demokrasia, sasa natangaza tena kwamba sitawapa tena fedha, niwape za nini wakati Rais aliyeko madarakani anafanya kazi ambayo ndio nilikuwa naipigania” alisema Sabodo.
Sabodo alisema iwapo serikali yote itahamia mkoani humo, itakuwa ametimiza ndoto ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambaye alitamani kuona mkoa huo unakuwa makao makuu ya nchi.
Aliongeza alichofanya Rais Magufuli, kimewashinda marais wengine waliomtangulia, hivyo yeye kama mfanyabiashara na mtu mwenye mapenzi makubwa kwa nchi yake, lazima aunge mkono hatua hiyo ya Serikali kuhamia Dodoma ambayo aliita ‘Azimio la Dodoma’.
“Kwa hiyo natangaza kuunga mkono Azimo la Dodoma kwa kuwekeza dola za Marekani bilioni 5, ambazo zitatumika kwa ajili ya uwekezaji mkubwa katika huduma mbalimbali za jamii mkoani humo,” alisema Sabodo.
Kuhusu uwekezaji alisema atawekeza kwenye viwanda kama vya mvinyo, viwanda vya kusindika mihogo na viwanda vingine ambavyo vitahitajika katika mkoa huo.
Sabodo alisema kwamba juhudi zake za kuwekeza katika huduma za jamii kama shule, pia ataziendeleza katika mkoa huo kwa kuhakikisha kwamba zinajengwa shule kadhaa za kisasa, ambazo zitamudu mahitaji ya watu wa eneo hilo.
Kwa upande wa huduma ya afya, Sabodo alisema atatumia umaarufu wake kuwashawishi wamiliki wa Hospitali ya kimataifa ya Apollo ya India ili waje nchini wakashirikiane naye kujenga hospitali ya kisasa, ambayo itakuwa inatoa huduma za kisasa mkoani humo.
Sabodo ni mfanyabiashara wa kitanzania mwenye asili ya Kihindi ambaye alizaliwa mkoani Lindi. Katika maisha yake amekuwa anafanya biashara katika nchi za Kenya, Ufaransa, India, Sudan na Zimbabwe.

Monday, 1 August 2016

Mo Dewj Afunguka, Ofa yake kwa simba bado ipo.


Tarehe August 1, 2016Mohammed-Dewji
Mohammed Dewji akisalimiana na mmoja wa wadau kwenye jukwaa kuu wakati wa tamasha la Simba Day. Mfanyabiashara bilionea Mohamed Dewji baada ya jana kufanikiwa kushinda imani ya wanachama wa simba na kupewa idhini ya kuendeleza timu hiyo leo ameibuka na kuwashukuru wanachama wa Simba kwa uamuzi huo na kupinga hoja ya kuwa hajazungumza na viongozi wa klabu hio.
Dewji alianza kwa kuwashukuru wanachama wa Simba kwa kupitisha ajenda ya mabadiliko licha ya viongozi kutowasilisha taarifa ya maoni ya kamati iliyoteuliwa kukusanya maoni ya kubadilisha mfumo wa uendeshaji. ” Mimi Mohamed Dewji nashukuru sana wanachama wa Simba kwani wamevuja damu, jasho kwa ajili ya Simba, nasema nitakuwa nao bega kwa bega. ”
” Kwa namna moja au nyingine, kuna hoja zimeniumiza na zilikuwa za upotoshaji na nimeona ni vyema kuziongelea kwa undani. ” ” Kuna hoja ya kwanza viongozi wanasema natangaza kwenye vyombo vya habari na sisihatujawahi kukutana. Leo labda niwe wazi zaidi, nishakutana na Rais wa Simba , Evan Aveva zaidi ya mara tatu. Alikuja na wajumbe wa kamati kuu.”
Dewji pia amefafanua hoja ya kutotuma ofa yake kwa maandishi na kudai alikuwa anasubiria ridhaa ya wanachama. Kwa kuwa wanachama wameshatoa ridhaa ametuma rasmi barua kwa viongozi wa Simba.
“leo asubuhi nimeandika barua kwenda kwa Rais wa Simba bahati mbaya ofisi yake imefungwa, ikifunguliwa tu barua yangu ya kwanza”.
” Ni dhahiri kwamba baadhi ya viongozi wanaoongozwa na Rais Evans Aveva hawataki mabadiliko lakini nashukuru wanachama wananiunga mkono”.

Baada Ya Mo Dewj Kufanya Yake Jana,Huko Moro Omog Ashikiki.

Tarehe August 1, 2016
OMOG
Katika kuhakikisha wachezaji wa Simba wanakuwa na stamina ya hali ya juu, kocha wa kikosi hicho, Joseph Omog, jana asubuhi aliamua kuwakimbiza wachezaji wake kwenye milima kwa takriban dakika 30.
Mazoezi hayo ya jana Jumapili, yalianza saa 2:00 na kumalizika saa 4:15, yalianzia uwanjani, kisha wakahamia milimani kabla ya kurudi tena uwanjani kumalizia programu ya asubuhi.
Katika mazoezi hayo mwanzo mpaka mwisho wachezaji walianza kwa kunyoosha misuli na kuchezea mpira kwa saa moja, kabla ya kuelekea milimani. Katika zoezi la kukimbia milimani, Kocha Mkuu Joseph Omog aligawa makundi mawili ambapo kundi moja aliliongoza yeye huku lingine likiongozwa na msaidizi wake, Jackson Mayanja.
Zoezi hilo lililodumu kwa takriban dakika 30, lilikuwa rafiki kwa wachezaji wote kwani hakuna hata aliyetegemea wala kulalamika kuchoka huku wakionekana kuwa na ari kubwa ya mazoezi.
Baada ya hapo, wakarudi uwanjani kumalizia dakika 45 kwa kuchezea mpira.
Omog ameyazungumzia mazoezi hayo ya milimani kwa kusema: “Ni maalum kwa ajili ya kuongeza pumzi, stamina lakini pia ni mazuri kwa kunyoosha misuli baada ya wiki nzima kucheza uwanjani pekee. Kikubwa wachezaji wangu wanaonyesha ushirikiano mzuri kwa kila zoezi.”

clouds stream