Thursday, 7 September 2017

Taarifa Uchunguzi Almasi, Tanzanite Kutua Kwa JPM ‘Live’ Leo

Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
IMG-20170426-WA0006

Rais, Dkt. John Pombe Magufuli leo anatarajiwa kupokea taarifa ya uchunguzi wa madini ya Tanzanite na Almasi uliofanywa na Kamati Maalum mbili zilizoundwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai.

21317572_994121220729369_7894129644206341507_n

Tuesday, 5 September 2017

Wabunge UKAWA Wasusia Kuapishwa Kwa Wabunge Wa CUF

Related image

Wabunge kutoka Upinzani katika Umoja wa Ukawa leo asubuhi wametoka nje ya Bunge na kususia shughuli ya kuapishwa kwa wabunge 7 wa Viti Maalum CUF.

Shughuli ya kuapishwa kwa wabunge hao imefanyika leo na Spika Job Ndugai kabla ya kuanza kwa kipindi cha maswali na majibu katika Mkutano wa 8 Bunge la 11.

Wabunge hao waliteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuziba nafasi ya wabunge nane wa Viti Maalum CUF waliotimuliwa uanachama na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba.

Mmoja wa wateule hao, Bi. Hindu alifariki dunia siku chache kabla ya kuapishwa na hivyo kufanya idadi ya wabunge waliokula kiapo leo kuwa saba badala ya nane kama walivyoteuliwa.

Meya Chadema,Waziri Ummy Wazindua Bima Ya Afya Bure Kwa Wazee

Wazee mara baada ya kupata Bima ya  Afya.
Wazee mara baada ya kupata Bima ya Afya.
IMG-20170426-WA0006

Meya wa Ubungo Boniface Jacob pamoja na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu wamezindua huduma ya Bima ya Afya Bure kwa wazee wilaya ya Ubungo.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa vitambulisho vya wazee Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu amesema utekelezaji wa matibabu bure kwa wazee ni wa lazima na siyo hiari kwakuwa serikali ya awamu ya tano imeweka sera zinazotekelezeka kwa kila hospitali za umma.

Mwalimu amezitaka Hospitali kubwa za rufaa kuweka taratibu maalumu za kuwasaidia wazee wenye kadi za bima ya afya ili kuhakikisha wanaokoa maisha yao.

Naye Mstahiki Meya wa Ubungo Boniface Jacob amesema gharama zilizotumika ni za mapato ya wilaya hiyo na sio mkopo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Kisare Makori amesema utekelezaji wa kutoa huduma kwa wazee kwa Manispaa hiyo kwa kufuata kadi hizo utazingatia weledi na haki ili kuondoa kero kwa wazee hao.

clouds stream