Thursday, 12 March 2015

PSG pungufu yaitupa nje Chelsea

PSG pungufu yaitupa nje Chelsea

Mabingwa wa Ufaransa wameonyesha umwamba wao wa kucheza wakiwa pungufu na kuitupilia mbali Chelsea kwenye uwanja wake wa nyumbani wa Stamford Bridge, Chelsea ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kwenye dakika ya 81 na beki kisiki Cahill kabla ya kusawazishwa dakika tano baadae kupitia kwa David Luiz.
Mpira uliendelea kuwa mgumu sana kwa timu zote mbili baada ya PSG kucheza wakiwa nusu kwa kipindi kirefu baada ya mshambuliaji wake matata Zlatan Ibrahimovic.
Chelsea walipata goli la pili kwa njia ya penati ya utata baada ya beki kisiki wa PSG kunawa mpira kwenye eneo la hatari na Eden Hazard akafunga penati hiyo kwenye dakika za nyongeza za mchezo huo baada ya dakika 90 kutoka sare ya 1-1.
PSG awakukata tamaa walipigana na muda baadae dakika ya 114 nahodha mpiganaji Thiago Silva anafunga bao kwa njia ya kichwa, na mpaka mwisho wa mchezo mabao ni 2-2 na PSG anafuzu kwa bao ya ugenini.

Ajali Basi la Majinja, abiria watoa ya moyoni

Ajali Basi la Majinja, abiria watoa ya moyoni

Watu arobaini na wawili wamefariki dunia huku ishirini na wawili wakiwa wamelazwa hospitalini baada ya ajali ya barabarani iliyotokea asubuhi ya Jumatano, Machi 11, 2015 huko katika eneo la Changarawe, Mufindi katika mkoa wa Iringa.
Ajali hiyo ilitokea baada ya basi la abiria la kampuni ya Majinja Express lililokua likitokea Iringa likielekea Dar es Salaam kugongana uso kwa uso na lori lililokua likitokea Dar es Salaam kuelekea Iringa.
Kwa mujibu wa Mkuu wa polisi katika mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, amethibisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema kuwa kati ya watu 41 walioaga dunia, wanaume ni 33, wanawake 5 na watoto watatu.
Akizungumzia chanzo cha ajali hiyo mmoja wa abiria aliyekuwemo katika basi hilo amesema  kwamba dereva wa lori alijaribu kukwepa moja ya shimo katika barabara suala lililomsababisha kutoka katika upande wake wa barabara hadi upande wa basi hilo na kusababisha kugongana na basi hilo la kampuni ya Majinja Express.
Baadhi ya majina ya abiria waliokuwemo katika basi la Majinja   ni kama ifuatavyo:
Baraka Ndone (dereva), Yahya Hassan ( kondakta), Ester Emanuel, Lusekelo Enock, Jeremia Watson, Digna Solomoni, Frank Chiwango, Luteni Sanga, Teresia Kamingage, Dotto Katuga, Ester Fidelis, Paulina Justine, Mbamba Ipyana, Catherine Mwate, Mwajengo, Ndulile Kasambala, Zera Kasambala, Rebeka Kasambala, Shadrack Msigwa, Mathias Justine, Juliana Bukuku, Cristina Lyimo, Martin Haule Dominick Mashauri na Omega Mwakasege.
Wengine ni Ester Willy, Lucy Mtenga, Erick Shitindi, Edwiga Kamiyeye, Frank Mbaula, Mustapher Ramadhani, Kelvin Odubi, Upendo William, Charles Lusenge, Neto Sanga, Pili Vicent, Daniel, Jacob Doketa Iman Mahenge , Juma Sindu, Dk A. Shitindi, Six Erick, Frank Mbaule,
Wengine waliokuwepo katika ajali hiyo wametambuliwa kwa jina moja Amadi, Musa, Elias, Raphael, Hussein na Oswald.

Sakata la Escrow: Wahisani wakubali kuimwagia Tanzania mabilioni ya fedha

Sakata la Escrow: Wahisani wakubali kuimwagia Tanzania mabilioni ya fedha


Benki kuu ya Tanzania
Benki kuu ya Tanzania.
Wafadhili mbalimbali kutoka nje ya nchi watanatarajia kutoa kiasi cha shilingi bilioni 784 ambazo ni asilimia 85 ya fedha zilizobaki kukamilisha bajeti ya mwaka wa huu wa fedha.
Hatua ya wafadhili kutoa kiasi hicho cha fedha inafuatia kuridhishwa na  masharti waliyotoa waki itaka serikali serikali ya Tanzania kuwachukulia hatua vigogo serikalini waliopelekea kupotea kwa fedha za umma katika akaunti ya Tegeta Escrow mwaka jana.
Kwa mujibu wa waziri wa fedha Saada Mkuya akizungumzia utekelezaji wa ahadi zilizotolewa na wafadhili katika kusaidia bajeti ya serikali mwaka huu, amesema wafadhili hao ikiwemo nchi ya Finland wataanza kutoa dola milioni 44 za Marekani hivi karibuni.
Katika hatua nyingine  Mkuya  amesema  serikali inaendelea  kurejesha mahusiano mazuri na wahisani suala litakalo pelekea  waendelee kutoa  fedha  za  kukamilisha  miradi  mbalimbali ya  maendeleo nchini inayotegemea fedha za wahisani.

clouds stream