Wednesday, 21 September 2016

Aliyeng’atwa Ulimi Mbaroni.

Tarehe September 21, 2016
1V 1
Siku saba tangu tukio la kijana Saidi Mnyambi (26) ang’atwe ulimi na jirani yake, Mwajabu Jumanne (36) hadi kupoteza uwezo wa kuongea na kula, hatimaye Jeshi la Polisi limesema linawashikilia wote wawili kwa uchunguzi zaidi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Peter Kakamba amesema, polisi wamechukua maamuzi ya washikilia wote kutokana na maelezo yao kuonekana kutofautiana.
Kamanda Kakamba amesema, wakati kijana huyo anadai kuwa tukio hilo lilitokea baada ya yeye kulazimishwa kufanya mapenzi, lakini mwanamke huyo naye anadai kuwa alimng’ata ulimi wakati akijaribu kujiokoa ili asibakwe na kijana huyo.
Kutokana na hali hiyo, Kamanda Kakamba amesema jeshi hilo limeona kuna haja ya kuwashikilia wote wawili kwa uchunguzi zaidi ili kubaini ukweli wa jambo hilo kabla ya kuwafikisha mbele ya Mahakama.
“Tumeona tuwashikilio wote wawili kwani kila mmoja anaonekana kutoa maelezo tofauti na mwenzake, ili kuweza kupata maelezo yaliyokamilika ni bora kuwashikilia wote,” amesema Kamanda Kakamba.
Kijana Mnyambi alinyofolewa theluthi moja ya ulimi wake na mke wa jirani yake kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kumlazimisha kufanya naye mapenzi Sikukuu ya Idd El Hajj saa 3.30 usiku, mwanamke huyo alimwomba amsindikize nyumbani kwake kwa kuwa alikuwa amelewa.
Walipofika njiani inadaiwa kuwa mama huyo alimtaka kijana huyo wafanye mapenzi jambo ambalo alimkatalia lakini akamwomba waagane, angalau kwa kunyonyana ulimi (ampe denda), lakini ghafla kijana huyo alishtukia aking’atwa ulimi na mama huyo na kukimbilia nyumbani kwake.
Naye muuguzi Mwandamizi Hospitali ya Mkoa wa Singida alikolazwa kijana Mnyambi, Herman Mallya amesema, hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri ingawa hajapata uwezo wa kuongea mpaka sasa.

Milioni 50 Za Magufuli Kila Kijiji Kuanza Mwakani.

Tarehe September 21, 2016
150428213302_noti_za_tanzania_640x360_bbc_nocreditV 1
Baraza la Taifa la Uwezeshaji limesema utaratibu wa utoaji wa fedha Shilingi milioni 50 za kila kijiji zilizoahidiwa na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli, unaandaliwa na mapema mwanzoni mwa mwaka ujao zitakuwa zimetoka.
Mkurugenzi wa Mifuko ya Uwezeshaji katika Baraza hilo, Edwin Chrisant ameyasema hayo Jijini Dar es Salaam katika juma la benki za maendeleo vijijini (Vicoba) na kuongeza kuwa fedha hizo zitakwenda kwa wananchi walioko katika vikundi peke yake.
Maadhimisho hayo ya Vicoba yameandaliwa na Asasi iliyo ya kiserikali ya kijamii ya Maendeleo na Uchumi inayojishughulisha kutoa elimu na mafunzo kwa wanachama wa vyama hivyo (SEDIT).
Kuhusu fedha hizo za ahadi za Rais Magufuli, mkurugenzi huyo alisema serikali itakamilisha mpango wa fedha hizo kwa kila kijiji na zitakwenda kwa wale walioelimishwa namna nzuri na utaratibu wa fedha ili zifanye kazi iliyokusudiwa.
Amesema utoaji wa fedha hizo kwa kipindi hicho utakuwa wa aina tofauti na zitahakikishwa zinawafikia wananchi wa kipato cha chini kwa masharti yaliyo rahisi, ikiwa ni pamoja na kuwatambua zaidi walioko katika vikundi.

JPM Awalilia Marehemu Ajali Basi La New Force.

Tarehe September 21, 2016
magauf

V 1
1

clouds stream