Wednesday, 1 July 2015

Uhaba wa mafuta nchini wachukua sura mpya Bungeni

Uhaba wa mafuta nchini wachukua sura mpya Bungeni


Naibu wazii wa Nishati na Madini Charles Mwijage .
Naibu wazii wa Nishati na Madini Charles Mwijage .
Serikali imesema kwamba  akiba ya Mafuta ya Petrol nchini Tanzania inatoshelea hadi siku 40.Hatua hiyo inafuatia kuwepo kwa madai  kutokea uhaba wa mafuta siku kadhaa zijazo.
Akijibu hoja  ya Mbunge wa Ubungo John Mnyika aliyeomba Bunge hilo kujadili hoja hiyo kwa njia ya dharula kwa kuwa linamaslahi kwa uchumi wa  taifa Naibu wazii wa Nishati na Madini Charles Mwijage amesema mafuta yapo na kuna meli  zipo nje maji  marefu zinakuja nchini zikiwa na shehena ya mafuta.
Amewahakikishia wananchi kuwa nchi haiwezi kuapata tatizo la uhaba wa mafuta huku akisisitiza kuwa  kwa kushirikiana  na TCRA  wanawatafuta waliosambaza taarifa hizo.
Naye Naibu waziri wa Fedha Adam Malima amesema serikali itahakikisha kuwa wananchi wanapata  huduma  ya mafuta   kama  kwaida.

Urais 2015: Lowassa afunga mahesabu ya Wadhamini Morogoro

Urais 2015: Lowassa afunga mahesabu ya Wadhamini Morogoro

Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Kulwa Milonge, akionyesha fomu zenye orodha ya majina ya wanachama wa ccm,104,03  waliomdhamini kugombea urais, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
Katibu wa CCM Wilaya ya Morogoro Mjini, Kulwa Milonge, akionyesha fomu zenye orodha ya majina ya wanachama wa ccm,104,03 waliomdhamini kugombea urais, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wa Mkoa wa Morogoro jana wakati wa akitoa shukrani katika kuhitimisha Mkoa wa mwisho wa kupokea orodha ya majina ya wadhamini.
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, akizungumza na wanachama wa CCM na wananchi wa Mkoa wa Morogoro jana wakati wa akitoa shukrani katika kuhitimisha Mkoa wa mwisho wa kupokea orodha ya majina ya wadhamini.
Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa amehitimisha safari ya kusaka wadhamini katika mikoa 15 ya Tanzania bara na mitatu ya visiwani Zanzibar.
Akiwa Mkoani Morogoro Lowassa amepata wanaccm 104,038 waliojitokeza kumdhamini katika safari yake ya matumaini aliyoa ianza mara baada ya kutangaza nia ya kugombea urais uwanja wa sheikh Abeid Karume  jijini Arusha may 29 maka huu.
Lowassa pamoja na watia nia wengine CCM wanatakiwa kurejesha fomu za urais makao ya Makuu ya CCM mkoani Dodoma  wiki hii huku mwisho wa kurejesha fomu hizo  ikiwa ni julai 3,2015.
Baada ya kurejesha fomu watasubiri matokeo ya mchujo utaofanywa na kamatia Kuu CCM itakayoketi na kuanza zoezi a uchujaji.
Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na chama hicho inaonesha kuwa  vikao vya uchujaji vitakuwa kama ifuatvyo,
Kamati ya usalama na Maadili Zanzibar 4/7/2015
Kamati maalumu ya Halmashauri kuu ya Taifa 5/7/2015
Kamati ya Usalama na Maadili Taifa 8/7/ 2015
Kamati ya Halmashauri kuu ya Taifa 9/7/2015
Halmashauri kuu ya Taifa 10/7/2015
Mkutano mkuu wa Taifa 11-12/7/2015

Ghana yaanza kupaa Kimataifa, yazindua gari lake

Ghana yaanza kupaa Kimataifa, yazindua gari lake


Baadhi ya Magari yanayotengenezwa nchini Ghana.
Baadhi ya Magari yanayotengenezwa nchini Ghana.
Gari la Kantanka kutokana nchini Ghana.
Gari la Kantanka kutokana nchini Ghana.
Mafundi wa magari hayo.
Mafundi wa magari hayo.
Nchi ya Ghana imefungua njia kwa nchi  nyingine barani Afrika kufuatia kuanza utengenezaji wa magari aina ya Kantanka ambayo ni pamoja na lile  aina ya 4 by 4 ambalo linatarajiwa kuuzwa kwa takriban pauni 14,000.
Lakini je,kampuni hiyo itaweza kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa magari kama vile Toyota,Land Rover na BMW?.
Kwadwo sarfo ni mwana wa mmiliki wa magari hayo. Babaake ni m’bunifu ambaye pia ni kiongozi wa dini. Hupata fedha kutokana na kilimo na uchimbaji.
Magari ya Kantanka yanafananishwa na magari makubwa kama vile Toyota Prado ama MItsubishi Pajero.
Mbele ya gari hilo kuna michoro ya kucha za chui pamoja na nembo ya kampuni hiyo ya nyota ya Afrika.
Kwa mujibu wa mmoaja wa raia nchini humo amesema  watu wanapenda kununua bidhaa kutoka nje kwa hivyo italazimu kufanyika kwa mauzo ya ziada kwa gari hizi za kantanka kukubalika.
Inaonekana kwamba raia wengi kama alivyodai hapo awali Professa wana wasiwasi kuhusu usalama wa gari hilo na kudumu kwake.
Profesa Robert Ebo Hinson ambaye ni mkuu wa kitengo cha mauzo katika chuo kikuu cha Ghana:Nadhani kile kilichotokea hapo awali ni kwamba tumefanywa tuamini kwamba kile kinachotengezwa katika mataifa ya magharibi ni imara.

clouds stream