Sunday, 6 March 2016

Walimu Mbaroni Kwa Kufanya Mapenzi Na Wanafunzi

Walimu Mbaroni Kwa Kufanya Mapenzi Na Wanafunzi

Tarehe March 5, 2016
Walimu waliofanya mapenzi na wanafunzi wakiwa chini ya ulinzi.
Walimu waliofanya mapenzi na wanafunzi wakiwa chini ya ulinzi.
Walimu wanane wa Shule ya Sekondari Mihama, Kata ya Kitangili, Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza akiwemo Mkuu wa Shule, wamesimamishwa kazi huku watano kati yao wakishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kufanya mapenzi na wanafunzi kufuatia ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo.
Mulongo pia amevunja bodi ya shule hiyo baada ya kubainika kutofanya kikao hata kimoja tangu ilipoteuliwa Aprili 24, 2013.
Mkuu wa Shule hiyo Joseph Malifedha na walimu wengine waliotiwa mbaroni ni Rodrick Uroki, Denis Sanga, Edmund Boaz, Steven Samuel.
Walimu wengine watatu waliokuwa wakifundisha shuleni hapo, lakini wakahamishwa na hivi sasa wanasakwa na polisi kwa tuhuma hizo ni Joseph Lamongi na Joeza Mzava waliohamia Sekondari ya Sangabuye pamoja na Abdallah Mtelwe aliyehamia Tanga.
Malifedha anadaiwa kuwachangisha fedha wanafunzi wa kidato cha kwanza na cha tatu kwa ajili ya picha za kuweka kwenye vitambulisho (passport size).
Akitangaza uamuzi huo, Mulongo alisema tume maalumu ya uchunguzi iliyoundwa Januari 27, kuchunguza tuhuma dhidi ya walimu hao kujihusisha na mapenzi na wanafunzi imebaini ukweli baada ya kuwahoji wanafunzi kadhaa.
“Ni fedheha na haivumiliki kuona walimu wakifanya mapenzi na wanafunzi wao. OCD wakamate walimu wote na uanze uchunguzi mara moja na kukusanya ushahidi utakaowezesha wahusika kufikishwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake,” aliagiza Mulongo.
Amri hiyo ilitekelezwa mara moja kwa walimu hao kuwekwa chini ya ulinzi.
Mulongo pia alimwagiza Katibu wa Idara ya Utumishi wa Walimu Mkoa wa Mwanza, Genzi Sahani kuwaandikia barua za onyo walimu wa kike shuleni hapo kwa kushindwa kulinda na kutetea masilahi ya wanafunzi wa kike waliokuwa wakidhulumiwa kingono na walimu wenzao kiasi cha baadhi yao kuathirika kisaikolojia.
Pia, alimwagiza Ofisa Elimu Mkoa wa Mwanza, Khamisi Maulid kuangalia uwezekano wa kuwahamishia shule nyingine wanafunzi waliodhulumiwa kingono na walimu wao ili kuwaepusha na matatizo ya kisaikolojia.
Maulidi alisema wanafunzi walioathirika zaidi ni wale wa kidato cha nne.
Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mkoa wa Mwanza, Said Mselem alisema kitendo hicho kimeifedhehesha taaluma ya ualimu na kuahidi kuwa ofisi yake itatanua wigo wa uchunguzi hadi kwenye shule nyingine.

Friday, 4 March 2016

Maalim Seif Atua Z’bar, Adai Polisi Sasa Ni Tawi La CCM

Maalim Seif Atua Z’bar, Adai Polisi Sasa Ni Tawi La CCM

Tarehe March 5, 2016
Maalim Seif akirejea Visiwani Zanzibar.
Maalim Seif akirejea Visiwani Zanzibar.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad aliyewasili  jana Zanzibar kutoka nchini India  kwa matibabu  amelishushia lawama Jeshi la Polisi visiwani humo kuwa limegeuka tawi la CCM.
Akizungumza na wafuasi wake waliofika kumpokea katika Uwanja wa Ndege wa Abeid Amani Karume na baadaye kumsindikiza hadi nyumbani kwake Mbweni mjini hapa Maalim amedai kusikitishwa na kuona hujuma, watu wakipigwa na kujeruhiwa na Mazombi kila kukicha wakati Polisi wapo wanayaona na hakuna aliyeitwa kuhojiwa.
Aiidha, Maalim Seif alimlaumu, Dk Ali Mohamed Shein kuwa si muungwana akidai kuwa amekataa kuondoka madarakani.
Alisema la kushangaza zaidi ni kuona aking’ang’ania uchaguzi wa marudio, ilihali hakuna mantiki wala kifungu chochote cha sheria kinachohalalisha hatua hiyo.
Baadhi ya viongozi wa CUF waliohudhuria mapokezi hayo ni pamoja na Mansour Yussuf Himid, Nassor Ahmed Mazrui, Fatma Abdulhabibi Ferej na aliyekuwa mgombea mwenza wa Chadema chini ya mwavuliwa wa Ukawa katika urais wa Muungano, Juma Duni Haji.
Maalim Seif pia  alimtahadharisha Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha asijaribu kulazimisha chama hicho kushiriki uchaguzi ‘batili’ wa marudio.
Uchaguzi wa marudio visiwani humo umepangwa kufanyika machi 20 mwezi huu,huku serikali ya Zanzibar ikisema maandalizi ya uchaguzi huo yanaendelea vizuri.

Msiharibu Kazi Mkitegemea Uhamisho-Waziri Mkuu Aonya

Msiharibu Kazi Mkitegemea Uhamisho-Waziri Mkuu Aonya

Tarehe March 4, 2016
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema watumishi wa umma wako huru kuhamia kokote wapendako lakini wahakikishe wanaenda huko wakiwa safi na kamwe mtu asiharibu kazi akitarajia kuwa atahamishiwa sehemu nyingine.
Majaliwa ametoa onyo hilo leo wakati akizungumza na watumishi wa Wilaya ya Itilima kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo ambao ameuzindua leo Mkoani Simiyu.
Amesema Serikali hii haina utumishi kwa mtu aliyeharibu kazi. Usije ukaharbu hapa Itilima ukadhani utaenda Bunda kuendelea na kazi. Serikali ya awamu hii haina nafasi na watumishi wa aina hiyo.
“Watumishi wenzangu huu ni wakati wa kubadilika na kuona mwelekeo wa Serikali hii ya Awamu ya Tano ukoje na jukumu letu ni kuwatumikia Watanzania wote bila kujali itikadi zao, rangi wala dini zao,” amesema.
Waziri Mkuu aliwahakikishia watumishi hao kwamba Serikali inatambua changamoto walizonazo kutokana na upya wa Wilaya hiyo na Mkoa huo na akawaahidi kuwa  mazingira Yao yataboreshwa.
“Msiwaadhibu wananchi kwa kisingizio cha mazingira magumu ya kazi zenu, tunajua mnayo madai ya nauli, posho za mafunzo, kupandishwa madaraja na malimbikizo ya likizo,” alisema huku akishangiliwa.
Alisema Serikali itayalipa madeni hayo japo haitamaliza yote kwa wakati mmoja ila ana uhakika wa kukamilisha walau kwa asilimia 80.
Mapema akitoa taarifa Mkuu wa Wilaya hiyo, Bibi Georgina Bundala alisema wilaya hiyo iliyoanzishwa Machi, 2012 na kupata Halmashauri Julai 2013 haina kituo cha polisi cha wilaya, haina gereza, ofisi za TAKUKURU, mahakama ya wilaya, hospitali ya wilaya wala benki.

clouds stream