Wednesday, 18 October 2017

LISSU KUTIBIWA AWAMU YA TATU NJE YA NAIROBI ,KAMERA CCTV YAIBUA MAMBO




Tundu Lissu.



Mwenyekiti wa Chadema, Mhe. Freeman Mbowe amesema kuwa Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu
anaendelea vizuri sasa na hatumii tena mirija kwa ajili ya kula chakula bali anakula mwenyewe na anakula chakula anachokitaka
na kwa mara ya kwanza ameweza kutoka Chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU), na kuliona jua tangu afikishwe hospitalini.
Mbowe amesema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokutana na waandishi wa habari kwa ajili ya kutoa taarifa za maendeleo ya
Mhe. Lissu na kudai kuwa licha ya maendeleo hayo mazuri, muda sio mrefu Mhe. Lissu ataanza awamu ya tatu ya matibabu.
Amesema Lissu ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), amefanyiwa upasuaji mara 17 na kwamba ni
maajabu ya Mungu kwamba Kiongozi huyo ni mzima na anaendelea kupumua vizuri baada ya misukosuko yote.
“Tunatarajia baada ya muda kidogo ataanza matibabu ya awamu ya tatu ambayo hayatakuwa Nairobi tena,” amesema Mhe.Mbowe.
Mbowe ameongeza kuwa katika awamu ya tatu ya matibabu, wataiachia familia nafasi ya kufanya maamuzi na kuweza kusaidia
pale watakapohitajika kusaidia.
Aidha, Mhe. Mbowe amehoji ni kwanini kamera za ulinzi za CCTV zilizokuwepo eneo la tukio Mjini Dodoma wakati Lissu
aliposhambuliwa kwa kupigwa risasi zimeondolewa.
“Lissu ameshambuliwa lakini ilichukua masaa mawili kwa polisi kufika kwenye eneo la tukio, kwanini tusiingie hofu?, pia Mh.Lissu
ni jirani wa Waziri, tuna taarifa kuwa ile CCTV Camerailiyokuwepo eneo la tukio imeondolewa, je imeondolewa na nani?,”amehoji Mbowe.
Mhe. Lissu alishambuliwa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana, Septemba 7, mwaka huu akiwa kwenye gari lake, nyumbanikwake Area D, Mkoani Dodoma, majira ya mchana akiwa anatoka bungeni.
Tangu wakati huo hakuna mtu yeyote Yule aliyetiwa nguvuni kuhusiana na tukio hilo la kinyama huku Jeshi la Polisi likiendelea nauchunguzi kubaini wahusika wa tukio hilo.
Wakati uchunguzi ukiendelea, Mhe. Lissu amekuwa kitandani alipolazwa katika Hospitali ya Jijini Nairobi, Kenya akiendelea na
matibabu.

Monday, 16 October 2017

Nkamia Aibua Mapya Hoja Binafsi Ukomo Wa Bunge, Nape Afunguka




Juma Nkamia, Mbunge wa Chemba (CCM).



Wakati kukiwa na taarifa zisizo rasmi zinazozagaa katika mitandao ya kijamii tangu jana, Oktoba 14, 2017 zikidai kuwa Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia amelazimika kuondoa kwa muda hoja yake binafsi ya ukomo wa bunge ambayo alikusudia kuiwasilisha katika bunge lijalo baada ya mashauriano na maelekezo ya viongozi wa juu wa CCM, Mbunge mwenzake wa Jimbo la Mtama (CCM), Mhe. Nape Nnauye amepigilia msumari kauli iliyotolewa na Spika wa zamani wa Bunge , Pius Msekwa.

Mhe.Nape amesema misimamo hiyo ndiyo misimamo ya Chama Cha Mapinduzi chini ya Mwalimu Julius Nyerere.

Mhe. Nnauye ameweka kipande cha video inayomuonesha Mzee Pius Msekwa akielezea juu ya ukomo wa kiongozi madarakani na kusema chama hicho kilishafikiria miaka ya nyuma kuongeza miaka kutoka 10 na kuendelea lakini waliona miaka kumi inatosha kwa mtu kuongoza na kusisitiza ikiwa miaka 15 ikatokea mkapata kiongozi mbaya miaka hiyo itakuwa ni mingi sana.

“Miaka 15 mkipata kiongozi mbaya ni mingi sana, nashauri ibaki miaka 10 kama kiongozi ni mbaya angalau tumvumilie kwa miaka 10 tu halafu basi ndivyo hoja ya miaka 10 ilivyopita si kama hiyo mingine hatukufikiri ilifikiriwa ndiyo maana naposikia kuna Mbunge mmoja anataka kupendekeza twende kwenye miaka saba kwa vipindi viwili ninataka kumjulisha kwamba hili si wazo jipya
tulishafikiri na lilikataliwa kwa hiyo mimi na imani CCM itaendelea kulikataa hilo, tutabaki kwenye miaka mitano tu mara mbili basi,” amenukuliwa akisema Msekwa.

Kufuatia kauli hiyo ndipo Nape Nnauye akashindilia na kusema kuwa hicho ndicho Chama Cha Mapinduzi (CCM) cha Mwalimu JuliusNyerere anachokijua yeye.

Siku za karibuni Mbunge wa Chemba (CCM), Juma Nkamia alidai anataka kupeleka hoja bungeni kuongeza muda wa utawala hadi
miaka 7 badala ya miaka mitano ya sasa.

Hatahivyo, Nkamia amesema kuwa kesho ataweka hadharani taarifa yake kuhusiana na minong’ono inayoendelea nchini kuwa ameondoa hoja yake.

“Nitazungumza na waandishi wa habari Jumatatu nitaeleza ukweli,” amesema Nkamia alipoulizwa kuhusiana na uvumi huo wakuondoa hoja yake.

Mwanafunzi Aua Wenzake 5 Na Mlinzi Kwa Risasi






Mwanafunzi mmoja nchini Kenya amewaua wenzake watano katika Shule ya Sekondari Mchanganyiko ya Lokichogio na mlinzi mmoja kwa kuwapiga risasi na baada ya kusimamishwa masomo shuleni hapo.

Akithibitisha tukio hilo, Kamishna wa Kaunti ya Turkana Seif Matata amesema mmoja wa wauaji ni mwanafunzi aliyekuwa amesimamamishwa masomo shuleni hapo kutokana na utovu wa nidhamu

Mwanafunzi huyo ajulikanaye kwa jina la Abrahamu wa kabila la Toposa kutoka Sudan Kusini,
aliyeshirikiana na watu wengine watatu kufanya ukatili huo anadaiwa kusimamishwa masomo kwa utovu wa nidhamu baada ya kusikika akitoa vitisho kuwaatakuja kuichoma shule hiyo kwa moto ili kulipa kisasi.

Siku ya tukio, mwanafunzi huyo akiambatana na wengine watatu alikuja asubuhi na kumuua mlinzi kisha kuelekea kwenye bweni la wavulana ambako ndipo alihisi wanafunzi waliomsababishia kufukuzwa shule walikuwa wakilala kisha kuhamia bweni la wasichana na kuwajeruhi wengine kadhaa.

clouds stream