Monday, 26 May 2014

AFRIKA MASHARIKI KUONGOZA KWA UKUAJI WA UFISADI.


Kampuni hewa, ufisadi na ukuwaji uchumi Afrika Mashariki

Takwimu za mashirika ya fedha duniani zinaonesha kwamba eneo la Afrika ya Mashariki linakuja juu kiuchumi na kwamba huenda likawa kituo kikuu cha ukuwaji wa uchumi katika Afrika iliyo chini ya jangwa la Sahara.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ameidhinisha malipo yenye utata kwa kampuni mbili za Anglo Leasing.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya ameidhinisha malipo yenye utata kwa kampuni mbili za Anglo Leasing.
Hata hivyo, uwepo wa ufisadi mkubwa uliotitia katika eneo hilo unatishia ukuwaji wenyewe wa uchumi, na pia ongezeko la ukosefu wa usawa, na mambo yanayotakana nayo - kama vile uhalifu wa kawaida na hata ugaidi.
Mfano wa kashfa kubwa za kifisadi ambazo zimekuwa zikiandama nchi za eneo hilo ni kama ile ya Anglo-Leasing ya Kenya au za IPTL, Dowans, EPA, na hivi majuzi ya akaunti ya Escrow nchini Tanzania. Haya ndiyo mataifa mawili makubwa miongoni mwa mataifa matano yanaounda sasa kanda ya Afrika ya Mashariki.
Mifano ya kashfa hizo inaonesha kwamba serikali zimekuwa zikichuma kwa mkono mmoja, na kuzila fedha hizo kwa mkono mwengine kupitia mkururo wa kampuni za ukweli na uongo ambazo hupatiwa tenda za mabilioni ya fedha.
John Githongo, afisa wa serikali ya Kenya aliyefichua kashfa ya Anglo Leasing.
John Githongo, afisa wa serikali ya Kenya aliyefichua kashfa ya Anglo Leasing.
Yanapobainika hayo, serikali hizi hujidai kuja juu kuchukua hatua, lakini kampuni hizo huja juu kuelekea mahakamani ambako mara kadhaa serikali hushindwa na matokeo yake kampuni zikaendelea kufaidi fedha ya walipa kodi.
Tunajiuliza chimbuko la kampuni za aina hii? Ni zipi nguvu zake? Na je, ni kweli serikali za eneo la Afrika ya Mashariki zina udhaifu huo kwenye mihimili yake ya kisheria kiasi ya kwamba mara nyingi hubwagwa mahakamani kwenye kesi za namna hii? Kubwa kuliko yote: Je, Afrika ya Mashariki bila ya ufisadi inawezekana?
Washiriki:
1. Mbunge David Kafulila kutoka Tanzania, ambaye hivi majuzi tu aliibua kile kilichopewa jina la kashfa ya akaunti ya Escrow, ambayo inatajwa kumeza shilingi bilioni 200. Tayari Ofisi ya Mkaguzi wa Serikali na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini humo zinasemekana kuanza kazi ya kuchunguza madai hayo.
2. Koigi Wamwere kutoka Kenya, ambaye aliwahi kuwa waziri msaidizi anayeshughulikia mawasiliano na habari katika serikali ya chama cha NARC, ambayo iliingia madarakani kwa kaulimbiu ya kulimaliza kabisa suala la kashfa ya Anglo-Leasing kwa kuwafikisha wahusika kwenye mikono ya sheria. Lakini serikali hiyo chini ya Rais Mwai Kibaki ikamaliza muda wake bila ya kuchukua hatua ya maana na matokeo yake hivi majuzi Rais Uhuru Kenyatta akaagiza deni la shilingi bilioni 1.4 linalodai kampuni mbili za Anglo Leasing lilipwe. Kwa mujibu wa Katibu Mkuu wa Hazina wa Kenya, Kamau Thugge, tayari deni hilo lilishalipwa tangu tarehe 19 Mei mwaka huu wa 2014.
3. Foum Kimara kutoka Uingereza, ambaye ni mwanaharataki na mchambuzi wa masuala ya kiuchumi na kijamii, ambaye amekuwa akifuatilia na kuandika sana juu ya mapungufu ya kimfumo katika eneo la Afrika ya Mashariki.
Muongozaji: Mohammed Khelef
Mhariri: Josephat Charo

HOUSE FOR SALE AT KIGAMBONI DAR.

LOCATION: TUANGOMA  KIGAMBONI

FEATURES: 4 BEDROOMS , SITTING ROOM, STORE  AND KITCHEN

PRICE: TSH 150 MIL

CONTACT: +255 652 314 181

EMAIL: nijuzetz@gmail.com

BRAZUCA NDIO JIN RASMI LA KOMBE LA DUNIA BRAZIL.


Brazuca - mpira wa world cup
Brazuca ndilo jina la mpira rasmi utakaotumika katika mchuano wa kombe la dunia Brazil hapo 12 mwezi ujao.
Watengenezaji Adidas pamoja na baadhi ya wachezaji wameusifu kwa shabaha na wepesi.
Brazil kwenyewe ndiko kuna wasiwasi - na Gwiji wa soka nchini humo Pele anawahimiza raia wenzake warekebishe mambo. Balozi huyo wa soka mwenye umri wa miaka 73 Ametiwa wasiwasi na maandamano ya mara kwa mara ya kupinga matumizi ya hela nyingi za kuandaa kombe la dunia.
Maandamano hayo yameshangaza wengi kwani Brazil inahusudu na kusifika kwa ubingwa wao wa kusakata kandanda.

Ushauri

Pele anasihi maandamano hayo yakome kwani yatawafanya wapenzi wa kandanda wa ng'ambo waliokuwa wanauia kwenda kujionea mchuano huo kughairi.
Katika mkutano na waandishi habari huko Mexico amenukuliwa kusema, ana taarifa kuwa tayari 25%ya mashabikii wa kigeni wameshavunja safari zao za kwenda Brazil kwa sababu ya maandamano hayo na kama yakiendelea basi wengine wengi huenda wakakata safari hizo na hivyo kuleta hasara ya Brazil kukosa biashara hasa za kitalii.
Japo Pele anakubaliana nao katika maandamano hayo ya kutaka kuboreshwa kwa huduma za kijamii hasa za matibabu, usafiri na elimu, anasisitiza kuwa timu ya taifa ambayo imeiletea sifa tele nchi hiyo isitumiwe kulipia makosa ya ufisadi unaofanywa na wanasiasa ambao wanalaumiwa kwa maovu mengi ikiwemo kucheleweshwa kwa kukamilika kwa viwanja 12 vya mpira , huku kukiwa zimesalia takriban wiki 3 tu kabla kombe hilo kuanza.
Brazil ikiwa ndilo taifa lililoshinda kombe la dunia mara nyingi kuliko lengine tena ugenini inakumbwa na shinikizo kubwa la kushinda kombe hilo nyumbani.

Maandalizi

Kufikia sasa ni nchi chache tu ambazo tayari zimetaja vikosi vyao ikiwemo hiyo Brazil na Uingereza, ambako, nahodha wa timu hiyo Steven Gerald nae amekuwa akitathmini jinsi kikosi cha timu ya taifa lake kilivyo na wachezaji chipukizi kiasi cha kuogofya.
Anasema anatumaini kuwa hawatashikwa na mchecheta wa uoga watakapokuwa uwanjani Brazil. Majina yanayotajwa sana katika timu hiyo ya Uingereza ni akina Ross Barkley, Raheem Sterling na Luke Shaw. Nahodha Gerrard amewaomba wachezaji waliokomaa pamoja na yeye mwenyewe wawashauri vyema vijana hao chipukizi watakapokuwa huko safarini kutafuta ubingwa wa dunia katika soka.
Mechi ya kwanza ya Uingereza watakumbana na wa-italaino hapo juni 15 katika uwanja ulioko eneo la msitu wa nyika ya Amazon kunakojulikana kuwa na joto si haba.
Nasi hapa kikosi cha BBC michezo tukapopasha kila joto hilo la kombe la dunia litakavyokuwa linapanda, huku Afrika tukiwakilishwa na Aljeria , Nigeria, Ghana, Cameroon na IVORY Coast .

clouds stream