Sunday, 25 January 2015

Lungu Rais mpya Zambia

Lungu Rais mpya Zambia

Edgar Lungu rais mpya nchini Zambia.
Edgar Lungu rais mpya nchini Zambia.
Gari la kamapeni la mgombea Edgar Lungu
Gari la kamapeni la mgombea Edgar Lungu
Wananchi katika kampeni za urais nchini Zambia.
Wananchi katika kampeni za urais nchini Zambia.
Mgombea wa chama cha Patriotic Front Edga Lungu ameshinda uchaguzi wa urais nchini Zambia. Tume ya uchaguzi nchini humo imesema kuwa Lungu amepata asilimia 48 ya kura zilizopigwa.
Alikabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mgombea wa upinzani  Bw. Hakainde Hichilema aliyepata asilimia 46. Katika kampeni zao  wote walikuwa wameahidi kuboresha mifumo ya elimu na kubuni nafasi za ajira.
Uchaguzi huo umefanyika  kufuatia kifo cha rais Michael Sata ambaye aliaga dunia mwezi Oktoba mwaka uliopita.

Prof. Muhongo ajiuzulu

Prof. Muhongo ajiuzulu

Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo akitangaza kujiuzulu leo jijini Dar es salaam.
Waziri wa Nishati na Madini Prof Muhongo akitangaza kujiuzulu leo jijini Dar es salaam.
Habari zilizotufikia hivi punde  ni kwamba Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Muhongo ametangaza kujiuzulu wadhifa wake.
Mtandao wa Hivi sasa utakujulisha zaidi kuhusiana na tukio hili.

Saturday, 24 January 2015

Gyan aiokoa Ghana, aipa pointi 3

Gyan aiokoa Ghana, aipa pointi 3


24FC80C600000578-0-image-a-46_1422036591690
Asamoah Gyan akiifungia Ghana goli dakika za mwisho
Ghana wapata ushindi wa kwanza wa michuano ya mataifa ya Afrika baada ya kupata ushindi wa 1-0 kwenye dakika za mwisho huku mwokozi akiwa mchezaji aliyekosa mechi ya kwanza ya Ghana dhidi ya Senegal Asamoah Gyan.Ushindi huo wa Ghana unainua matumaini ya kufuzu huku kundi hilo likionekana bado lina ushindani mkubwa.Kwenye kundi C mpaka sasa Senegal anaongoza baada ya kutoka sare na Afrika Kusini kwenye mechi iliyofuata baada ya mechi ya Ghana kumalizika.
24FC805B00000578-0-image-a-47_1422036608250
Black Stars walifanya mabadiliko mawili kwenye kikosi kilicholazwa 2-1 na Senegal, badiliko muhimu likiwa kureja kwa Asamoah Gyan safu ya mashambulizi, na wakarejelea mpangilio wa 4-4-2.
Mbweha wa Fennec nao walifanya mabadiliko matatu kwenye kikosi kilicholaza Afrika Kusini 3-1, Madjid Bougherra akiingia nafasi ya Rafik Halliche ulinzi, na washambuliaji Saphir Taider na Ishak Belfodil wakiingia.
24FC4F4100000578-0-image-a-26_1422034463036
Mechi hiyo ilionekana kana kwamba ingeisha sare, lakini dakika za ushei mpira kutoka safu ya ulinzi ya Ghana ulimfikia Gyan na kwa ujanja mkubwa na kasi akamlemea difenda Carl Medjani na kisha kumbwaga kipa Rais Mbolhi na kufunga bao safi la ushindi.
Ghana XI: Brimah, Afful, Rahman, Amartey, Mensah, Acquah, A. Ayew, Badu, Atsu, Gyan, J. Ayew
Algeria XI: M’Bolhi, Mandi, Bougherra, Medjani, Ghoulam, Lacen, Taider, Bentaleb, Brahimi, Feghouli, Belfodi

clouds stream