Saturday 31 December 2016

Makubaliano ya kisiasa nchini DR Congo yakwama

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila
img-20161130-wa0008

Makubaliano ya kisiasa kati ya serikali na upinzani nchini DR Congo ili kumaliza mgogoro wa kisiasa yamekwama katika dakika ya mwisho.

Muhula wa rais Joseph Kabila ulikamilika mapema mwezi huu ,lakini uchaguzi umeahirishwa huku makumi ya watu wakipoteza maisha yao katika maandamano.

Wapatanishi kutoka kanisa Katoliki awali walikuwa wamesema kwamba pande hizo mbili zilikuwa zinakaribia maafikiano ambapo rais Kabila atasalia mamlakani hadi uchaguzi utakapoandaliwa mwishoni mwa 2017 .

Hatahivyo baadhi ya makubaliano hayakuafikiwa hivyobasi kuahirisha sherehe ya kutia kandarasi makubaliano hayo huku mazungumzo yakiendelea.


clouds stream