Friday 16 December 2016

Syria:Maelfu ya watu wapelekwa sehemu salama Aleppo

Maisha mapya baada ya vita

Maisha mapya baada ya vita
img-20161130-wa0008

Watu takriban elfu tatu wakiwemo mamia ya watoto wameanza kuokolewa kutoka maeneo yaliyokuwa yanashikiliwa na waasi huko Aleppo.

Kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu imesema watoa misaada kwa sasa wanachukua mamia ya watu kutoka maeneo mbalimbali na kuwapeleka sehemu salama zaidi.

Mlolongo wa magari ya wagonjwa na magari ya abiria yamekuwa yakifanya kazi kubwa kusaidia kuwasogeza watu hao katika sehemu zinazoshikiliwa na serikali.

Takriban watu 50,000 wanasemekana bado wanaishi Mashariki mwa Aleppo
Takriban watu 50,000 wanasemekana bado wanaishi Mashariki mwa Aleppo

Maafisa wanasema uokoaji huo unatarajiwa kuchukua siku kadhaa.

clouds stream