Monday, 30 October 2017

RAIS MAGUFULI APONGEZA MABADILIKO CUF



Daraja la Furahisha



Rais Dkt. John Pombe Magufuli amesema kuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaunga mkono mabadiliko yanayotokea katika Chama cha Wananchi (CUF) na kupongeza hatua hiyo.

Rais Magufuli amesema hayo leo Jijini Mwanza wakati wa ufunguzi wa daraja la Furahisha litakalotumiwa na waenda kwa miguuMkoani humo.

Akikamilisha hotuba yake na kumtambua Mbunge wa Liwaled, Mhe. Zuberi Kuchauka (CUF), Rais Magufuli amesema wanawapongeza CUF kwa mabadiliko wanayofanya na kumtaka mbunge huyo kufikisha salamu zake na pongezi nyingi kwa mabadiliko hayo.

“Tunawapongeza sana kwa mabadiliko mnayofanya na ukawafikishie salamu zetu,” amesema Rais Magufuli.

Awali mbunge huyo alipopewa nafasi ya kusema machache, alimmiminia sifa nyingi Rais Magufuli na kumuombea dua ili awe na afya njema aweze kutimiza lengo lake na kukuza viwanda na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati.

“Mhe. Rais, sisi sote tunatambua kazi nzuri unayoifanya ya kuwaletea maendeleo Watanzania na mimi napenda nikupongeze sana kwa hilo na ndiyo maana nakuombea dua uzidi kuwa na afya njema,” amesema.

Hivi karibuni CUF imekuwa katika hekaheka na migogoro isiyokwisha na kupelekea chama hicho kupasuka vipande viwili, ambapo upande mmoja unaamini katika CUF ya Mwenyekiti anayetambulika na Msajili wa Vyama vya Siasa, Prof. Ibrahim Lipumba huku upande wa pili ukiwa unaamini katika CUF ijulikanayo kama CUF Maalim, ambaye ni Katibu Mkuu wa CUF.

NECTA YAONYA WANAFUNZI WASIMAMIZI MTIHANI WA KIDATO CHA NNE UKIANZA LEO

Image result for wanafunzi

Wanafunzi katika moja ya shule ya sekondari nchini.



Baraza la Mtihani nchini (NECTA) limesema halitosita kumchukulia hatua mwanafunzi yeyote pamoja wasimamizi wa Mitihani hiyo
ambao watakiuka sheria za mitihani ya kidato cha nne ambayo inaanza leo saa mbili za asubuhi.

Hayo yamesemwa na Katibu Mtendaji wa (NECTA), Dkt Charles Msonde wakati wa mkutano na waandishi, ambapo amesema
Baraza hilo linatoa wito kwa kwa wasimamizi wa mitihani wote kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu.

“Tunawaasa wasimamizi wa mitihani pamoja na wanafunzi kujiepesha na vitendo vya udanganyifu kwani Baraza litachukua hatuakali kwa yeyote yule atakayebainika kukiuka taratibu za uendeshaji wa mitihani ya Taifa” amesema Dkt Msonde.

Amesema Baraza hilo linawataka wamiliki wa shule kutambua kuwa shule zao ni vituo maalum vya mitihani na hivyo havitakiwi
kuingilia majukumu ya wasimamizi.

Aidha,katika mitihani huo jumla ya watahiniwa 585,938 wamesajiliwa kufanya mtihani huo, ambapo kati yao watahiniwa wa shule ni 323,513 na watahiniwa wa kujitegemea ni 62,425.

“Kati ya watahiniwa wa shule 323,513 waliosajiliwa ,wanaume ni 159.103 sawa na asilimia 49.18 na wanawake ni 164,410 sawa
na asilimia 50.82,huku watahiniwa wenye uono hafifu ni 305 ambapo maandishi yao yanakuzwa”amesema Dkt Msonde.


Friday, 27 October 2017

JAHAZI LAKAMATWA LIKISAFIRISHA HEROIN YA BILIONI 5




Dawa za kulevya aina ya Heroini.



Maofisa wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) wakishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama wamekamata zaidi ya kilo 100 za madawa ya kulevya aina ya Heroin zenye thamani ya Shilingi bilioni 5 zilizokuwa zikisafirishwa kwenye jahazi kutoka Unguja kwenda Dar es Salaam.

Kamishna wa Sheria wa DCEA, Edwin Kakolaki amesema hatua hiyo ilifikiwa baada ya maofisa hao kutilia shaka jahazi hilo ambalo ndani yake lilikuwa na raia kumi wa Iran na Wazanzibari wawili.
“Paketi 104 za madawa ya kulevya yanayoshukiwa kuwa ni heroin zilikamatwa katika jahazi hilo na kupelekwa kwa Mkemia Mkuuwa Serikali kwa vipimo zaidi,” amesema.

Amesema hadi jana jioni walikuwa wamefanya upekuzi kwa kusaidiana na mbwa maalum wa kunusa ili kuona kama kuna mzigo zaidi katika jahazi hilo.

Naye Kamishna Mkuu wa DCEA, Rodgers Siang’a amesema kiwango cha dawa hizo kingekuwa kikubwa zaidi kama sio kitendo cha watu hao kutupa kiasi kingine baharini baada ya kuzidiwa nguvu walipozungukwa na vyombo vya ulinzi na usalama.

“Vyombo vya dola viko imara kupambana na usafirishaji wa dawa za kulevya na hatutaacha kuyadhibiti magenge na mitandao yao,” amesema Siang’a.

Hatahivyo, upekuzi huo haukukamilika kutokana na hali ya mvua ambapo unatarajiwa kuendelea leo huku taratibu za kwenda kwa Mkemia Mkuu wa Serikali zikikamailika, watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani.

clouds stream