Samatta awafunga tena waalgeria,Tp Mazembe watwaa ubingwa wa Afrika
Mshabuliaji wa Kimataifa wa Tanzania na Klabu ya Tp Mazembe Mbwana Samatta akishangilia mara baada ya kufunga goli
Tp Mazembe wametangazwa mabingwa wa Klabu Bingwa Afrika baada ya kuinyuka USM Alger jumla ya mabao 4-1.
Samatta alifunga goli lake katika dakika ya 75 ya kipindi cha pili baada ya kuangushwa kwa Rogger Asale katika eneo la hatari.
Mchezo huo ulikuwa wa marudiano ambapo mchezo wa awali mazembe walishinda mabao 2-1 na Samatta alifunga goli moja kwa mkwaju wa penati.