Monday 28 December 2015

CCM Wajipanga Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar

CCM Wajipanga Uchaguzi Wa Marudio Zanzibar

Tarehe December 28, 2015
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduz Dk Alli Mohamed Shein.(aliyekaa) pembeni ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduz Dk Alli Mohamed Shein.(aliyekaa) pembeni ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai.
Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar   chini ya Mwenyekiti wake Dk Ali Mohamed Shein kimewataka wananchi na wanachama kujiandaa kwa uchaguzi mkuu wa marudio visiwani humo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Katibu wa Itikadi na Uenezi Zanzibar, Waride Bakari Jabu, amesema wananchi wametakiwa kujiandaa kwa uchaguzi wa marudio na kuachana na propaganda zinazotolewa na watu wachache kwa lengo la kupotosha ukweli..
Amesema  matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar wa Oktoba 25 ulifutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha kwa kile alichoeleza ni kuwepo kwa ukiukwaji wa kanuni na sheria za uchaguzi huru wa kidemokrasia.
Aidha, chama hicho  kimepongeza na kutoa baraka kwa mazungumzo yanayoendelea ya viongozi wakuu wa kisiasa yakiwa na lengo la kuleta amani ya kudumu. Kamati ya mazungumzo ya hali ya kisiasa Zanzibar yenye lengo la kusaka amani ya kudumu iliyovurugika kutokana na kufutwa kwa uchaguzi mkuu.
Kamati hiyo  inaundwa na viongozi wastaafu wakiwemo marais, Dk Salmin Amour, Amani Abeid Karume, Balozi Seif Ali Iddi ambaye ni Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharif Hamad na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.
Kwa upande wake  Rais wa Zanzibar, Dk Shein baada ya kufanya mazungumzo na Rais John Magufuli alisema mazungumzo hayo yanaendelea vizuri na taarifa kamili itatolewa  yatakapofikia tamati.
Alipoulizwa kuhusu hatma ya CCM kama uchaguzi mkuu utaorudiwa, Waride alisema chama bado kiko imara na hakijatetereka.
Licha ya chama cha Mapinduzi kujiandaa na uchaguzi mkuu Zanzibar, chama cha Upinzani cha CUF bado hakijatoa tamko lolote hadi sasa kufuatia kupinga vikali kurudiwa uchaguzi mkuu  visiwani humo.

Van Gaal Akubali Kuondoka Mwenyewe


Van Gaal Akubali Kuondoka Mwenyewe


Tarehe December 27, 2015


Kocha wa Manchester United Louis van Gaal amesema kuwa anaweza “kujiuzulu mwenyewe” baada ya Stoke City kuwapiga magoli 2-0 katika kichapo chao cha nne mfululizo katika michuano yote.
Mholanzi huyo, ambaye anakabiliwa na shinikizo baada ya kusajili mechi saba sasa bila ushindi, aliulizwa katika mahojiano na waandishi wa habari baada ya mechi iwapo ”anahofia kibarua chake kitaota nyasi ?”
Van Gaal, 64, alijibu kuwa hjilo lilikuwa jambo analostahili kujibu katika mazungumzo na mkurugenzi wa klabu hiyo Ed Woodward na si vyombo vya habari.
“Si siku zote ambapo ni klabu ndiyo inauwezo wa kufurusha kocha la ”
“Wakati mwingine mimi mwenyewe naweza kuchukua jukumu hilo mwenywe na kuhusiana na hilo sharti niende nifanye mkutano na mamlaka inayosimamia Manchester United safu yangu ya ukufunzi na kisha wachezaji wangu wala sio waandishi wa habari” alifoka van Gaal.
United imekuwa na msururu wa matokeo duni uliosababisha Red Deivls wakatupwa nje ya Ligi ya Mabingwa katika hatua ya makundi mbali na kuporomoka kutoka kwenye orodha ya nne bora katika jedwali la ligi kuu ya Uingereza.
Van Gaal, aliyechukua nafasi ya David Moyes katika msimu wa 2014, alisema klabu hiyo alimuunga mkono siku zote ila aliongeza: “Tumepoteza hivyo kuna hali mpya.
“Nahisi msaada wa wachezaji wangu na bodi yangu,Hata hivyo mashabiki wataudhika lakini hiyo inatarajiwa baada ya kushindwa mara nne ,” Van Gaal hafikiri ni muhimu kwamba Woodward haja muunga mkono hadharani .
“Kwangu mimi ni muhimu zaidi kwamba watu wanasema nini kuhusu utendaji kazi wangu ” alisema. “Mimi sina haja sana na matamshi ya umma.”

Lowassa Sasa Ni Mchungaji Ng’ombe?

Lowassa Sasa Ni Mchungaji Ng’ombe?

Tarehe December 26, 2015
Aliyekuwa Mgombea urais Edward Lowassa akichunga ng'ombe zake.
Aliyekuwa Mgombea urais Edward Lowassa akichunga ng’ombe zake.
Aliyekuwa Mgombea urais wa tiketi ya Ukawa Edward Lowassa ameanza rasmi uchungaji ng’ombe ikiwa ni ahadi yake kwa wananchi kuwa endapo akishindwa urais atakwenda kuchunga ng’ombe.
Aidha, hizi ni baadhi ya picha zikimuonesha Lowassa akiswaga  mifugo yake porini ambapo baadhi ya wananchi wameoneshwa kufurahishwa na utekelezaji wa ahadi zake mwenyewe.
Katika hizo Picha Lowassa alikuwa   akichunga ng’ombe zake huko Handeni mkoani Tanga.
Mwanasiasa Edward Lowassa akiswaga ng'ombe zake.
Mwanasiasa Edward Lowassa akiswaga ng’ombe zake.

Ridhiwani Aukana Utajiri, Atoa Tamko Utoroshwaji Makontena

Ridhiwani Aukana Utajiri, Atoa Tamko Utoroshwaji Makontena

Tarehe December 26, 2015
Ridhiwani Kikwete
Ridhiwani Kikwete
Familia ya aliyekuwa Rais wa awamu ya nne Dkt Jakaya Kikwete kupitia Mbunge wa Chalinze,  Ridhiwani Kikwete,  ambaye ni mtoto wa Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete akiiwakilisha familia ametoa kauli kuhusiana na kuhusishwa na  tuhuma za upitishaji makontena bila kulipiwa kodi bandarini.
Akizungumzia sakata hilo Ridhiwani alisema baada ya Rais Kikwete kumaliza muda wa miaka 10  madarakani, baadhi ya watu wamekuwa wakiiandama familia yao kwa tuhuma mbalimbali.
Alizitaja tuhuma hizo kuwa ni utoroshaji wa makontena kwenye bandari ya Dar es Salaam na kusisitiza kwamba tuhuma zote zinazotolewa hazina ukweli wowote bali zimelenga kumchafua yeye na familia yake.
Ridhiwani alisema tangu serikali ya awamu ya tano ianze kuwabana  watu wanaokwepa kulipa kodi za serikali,baadhi ya watu wanafanya jitihada za kumhusisha  na  watuhumiwa  hao.
Alisema hajawahi kuagiza bidhaa yoyote kutoka nje,kuwa na kontena la kulipiwa ushuru,kukwepa au kumuombea msamaha wa kupunguziwa kodi mfanyabiashara yeyote aliyeagiza kontena kutoka nje, hivyo mwenye ushahidi juu ya hilo autoe.
“Kama kuna mtu mwenye ushahidi autoe hadharani mimi niuone,dunia iuone, nawahakikishia ushahidi huo haupo na hautokuwepo labda uwe wa kughushi na wakifanya hivyo wataumbuka.
Kuhusu madai ya kumiliki Malori, mabasi na vituo vya mafuta Ridhiwani amesema ,
“Sina na sijawahi kumiliki lori au basi katika maisha yangu.Sina hisa wala ubia na mtu yeyote  au kampuni ya malori au mabasi.” Alisema Ridhiwani
“Naambiwa hapa nchini siku hizi kila jengo jipya linalojengwa inasemekana ni langu na vituo vipya vya mafuta naambiwa ni vyangu.Huo ni uongo mtupu”.Amesema Ridhiwani
Amesisitiza kuwa wanaosema, kuandika na kueneza maneno hayo wanajua wanasema uongo isipokuwa wanafanya hivyo kwa nia mbaya dhidi yake  na familia yake.

Tuesday 22 December 2015

Sanchez Kukosa Mechi Nne Tena

Sanchez Kukosa Mechi Nne Tena

Tarehe December 22, 2015
Alexis Sanchez
Alexis Sanchez
kocha wa Arsenal,Arsene Wenger amethibitisha kuwa mshambuliaji wa timu hiyo Alexis Sanchez atalazimika kukaa nje kwa michezo minne ijayo kutokana na jeraha lake la awali kutokupona kwa wakati.
Sanchez aliumia sehemu ya kifundu cha mguu baada ya kugongana na mpiga picha wakati timu hiyo ikikutana na Norwich
“Sanchez atakaa nje hadi Januari 10 mwakani pia tulipanga awe katika benchi wakati tulipokutana na Man City ila imeshindikana na hayo ni masuala ya kitabibu,”amesema Wenger.
Sanchez  atalazimiaka kukosa mchezo dhidi ya  Southampton, Bournemouth, Newcastle pamoja na mchezo wa  FA Cup wakicheza na Sunderland on Januari 9 2016.

Arsenal Noma, Yaitandika Man City 2-1

Arsenal Noma, Yaitandika Man City 2-1

Tarehe December 22, 2015
Wachezaji wa Arsenal wakimpongeza Theo Walcot ambaye alifunga goli la kwanza wakati timu hiyo ilipokutana na Man City
Wachezaji wa Arsenal wakimpongeza Theo Walcot ambaye alifunga goli la kwanza wakati timu hiyo ilipokutana na Man City
vijana wa Arsen Wenger leo wamezuia pointi tatu muhimu kwa kuitandika Manchester City kwa
moja katika mchezo wao wa ligi kuu ya Uingereza uliomalizika hivi punde.
Arsenal walianza kuzitingisha nyavu za Man City dakika ya 33 ambapo mshambuliaji machachari
wa timu hiyo Theo Walcot alikwamisha mpira wavuni baada ya mabeki wa Man City
kujichanganya.
Oliver Girioud aliipatia Arsenal goli la pili dakika ya 45 na kufanya timu hiyo iende
mapumziko ikiwa mbele kwa magoli mawili kwa bila.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na Man City walifanikiwa kupata bao la kufutia machozi
kupitia Yaya Toure dakika ya 82,hivyo basi mpaka mpira unamalizika Arsenal walichukua pointi
tatu katika mchezo huo

Blatter,Platini Wafungiwa Miaka Nane

Blatter,Platini Wafungiwa Miaka Nane

Tarehe December 21, 2015
Rais wa FIFA, Joseph Sepp Blatter na Michel Platini
Rais wa Fifa ,Sepp Blatter na yule wa Uefa Michel Platini wamefungiwa kujihusisha na masuala ya soka kwa muda wa miaka nane na kamati ya madili ya FIFA.
Blatter na  Platini wote wamekuwa kizuini kwa muda ambapo kamati ya maadili ya FIFA ilikuwa ikiwachunguza ambapo wote walisimamishwa mwezi oktoba kutokana na kashfa ya ufisadi wa kuhamisha Pauni Milioni 1.34 kutoka kwa Blatter kwenda kwa Platini ambaye Rais wa FIFA,Blatter alithibitisha mualamala huo.
Kamati ya maadili imewapata na hatia na hivyo wameonywa kutokujiingiza katika masuala ya soka kwa kipindi hicho pamoja na kungoja taratibu nyingine za kisheria kufuata

Rais Magufuli Amng’oa Mkurugenzi Mwingine

Rais Magufuli Amng’oa Mkurugenzi Mwingine

Tarehe December 22, 2015
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli leo  ametangaza kumsimamisha kazi mkurugenzi mkuu wa kampuni ya RAHCO Mhandisi Benhadad Tito na kuvunja Bodi hiyo.
Aidha, RAHCO ni Kampuni Miliki ya Rasilimali za Watu iliyo chini shirika la Reli Tanzania TRL.
Katika hatua nyingine Bodi hiyo iliiyovunjwa leo ilizinduliwa  na aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Samuel Sitta tarehe 29 Oktoba, 2015 chini ya Mwenyekiti Prof. Mwanuzi Fredrick.
Taarifa kamili itakujia katika mtandao huu hivi punde.

Rais Magufuli, Maalim Seif Wapata Suluhu Mgogoro Zanzibar ?

Rais Magufuli, Maalim Seif Wapata Suluhu Mgogoro Zanzibar ?

Tarehe December 22, 2015
Picha ya pamoja ya Maalim Seif,Rais Dkt John Magufuli pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu.
Picha ya pamoja ya Maalim Seif,Rais Dkt John Magufuli pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli jana  amekutana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Mgombea Urais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharrif Hamad,  Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Viongozi hao kwa pamoja wamejadili hali ya kisiasa Zanzibar na wamefurahishwa na hali ya usalama na utulivu inayoendelea mara baada ya kutokea mgogoro huo wa kisiasa visiwani humo.
Katika mkutano huo  Rais Magufuli amewapongeza Rais wa Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Kwanza wa Rais  wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, na viongozi wote wanaoshiriki katika mazungumzo ya kuleta hali ya uelewano Zanzibar.
Rais Magufuli pia  amewapongeza na kuwashukuru wananchi wa Zanzibar kwa kudumisha amani na utulivu wakati wa mazungumzo baina ya viongozi wa CUF na CCM yakiendelea huko Zanzibar.
Katika Mazungumzo hayo Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharrif  Hamad amemueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juu ya hali ya siasa Zanzibar kadiri anavyoielewa yeye na Rais Magufuli amemshukuru Makamu huyo wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kwa taarifa yake nzuri huku akimsihi waendelee na mazungumzo hadi suluhisho muafaka lipatikane
Mazungumzo ya Viongozi hao pia yamehudhuriwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Viongozi hao  wote kwa pamoja wamewaomba wananchi waendelee kuwa watulivu ili kutoa nafasi ya majadiliano yanayoendelea kufikia hatma njema huku wakieleza  matumaini yao kuwa vyama vya CCM na CUF haviwezi kushindwa kupata suluhu ya mgogoro huo.
Kwa upande mwingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemuhakikishia kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano itahakikisha kuwa amani na utulivu unaendelea kudumishwa Zanzibar.

Kasi Ya Rais Magufuli Yatua Rwanda, Kagame Afunguka

Kasi Ya Rais Magufuli Yatua Rwanda, Kagame Afunguka

Tarehe December 22, 2015
Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Rais Paul Kagame wa Rwanda.
Rais wa Rwanda Paul Kagame   amefunguka kwa mara ya kwanza mara baada ya rais John Magufuli kuingia Ikulu Novemba 5 mwaka 2015.
Kwa mujibu wa Balozi wake nchini, Uegene Kayihura amesema kwamba Rais Kagame amefurahishwa na hatua ambazo Rais John Magufuli anazichukua, hasa katika usimamizi na utendaji kazi wa bandari.
Kayira amesema hayo alipofika Ikulu ya Rais Magufuli  ambapo  amemhakikishia kuwa Rwanda iko tayari kushirikiana na Tanzania, hasa katika kuitumia Bandari ya Dar es Salaam kwa  kuwa Rwanda inapitisha asilimia 70 ya mizigo yake katiba Bandari ya Dar es salaam.
Ameongeza kuwa  Kagame amempongeza Rais Magufuli kwa hatua alizochukua kusafisha uozo katika bandari, kufichua ufisadi wa mabilioni ya shilingi kutokana na upotevu wa makontena, ambayo hayakulipiwa kodi stahili kwa serikali, kuvunjwa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), kutengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Awadhi Massawe na kusimamisha maofisa kadhaa wa bandari hiyo na wengine wanaohusika na usimamizi wa bandari kavu.
Katika kuimarisha utendaji Bandarini  na Mamlaka ya Mapato Rais Magufuli alimsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade na maofisa wengine wa mamlaka hiyo, ambao miongoni mwao tayari wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kutokana na ubadhirifu huo.

Monday 7 December 2015

Mgombea urais Uganda amtumia Magufuli kuingia Ikulu

Mgombea urais Uganda amtumia Magufuli kuingia Ikulu

Tarehe December 7, 2015
MgombeaUrais Bw. Kizza Besigye wa chama cha Forum for Democratic Change (FDC).
MgombeaUrais Bw. Kizza Besigye wa chama cha Forum for Democratic Change (FDC).
Kampeni za uchaguzi mkuu zimepamba moto nchini Uganda ambapo Mgombea Urais  wa upinzani anayemtikisa Rais Yoweri Museveni katika kinyang’anyiro hicho, Dk. Kizza Besigye wa chama cha Forum for Democratic Change (FDC) amemtumia Rais Magufuli kuomba kura kwa wananchi.
Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni  wiki iliyopita Kiiza alisema  kuwa atafuata nyayo za Rais John Magufuli katika kuhakikisha kuwa serikali inaendesha mambo yake kwa nia ya kubana matumizi yasiyo ya lazima, kukomesha ufisadi na mwishowe kuwanufaisha watu wa tabaka la chini kupitia uboreshaji wa huduma za jamii
Aliongeza kuwa  ili kubana matumizi ataiuza  ndege  inayotumiwa na Museveni kwa maelezo kuwa inalibebesha taifa lao gharama kubwa ambazo zinaweza kutumiwa katika kuboresha huduma za jamii.
Besigye alisema yeye anaunga mkono jitihada zinazofanywa na Rais mpya wa Tanzania, Magufuli kutokana na kuchukua hatua kadhaa dhidi ya ufisadi na  kuongeza ufanisi wa kazi katika ofisi za umma na pia kuongeza nidhamu ya matumizi kwa manufaa ya taifa na siyo watu wachache Uchaguzi Mkuu nchini Uganda unatarajiwa kufanyika mwanzoni mwa Februari, 2016.

Rais Magufuli amfukuza Kazi katibu mkuu wizara ya uchukuzi

Rais Magufuli amfukuza Kazi katibu mkuu wizara ya uchukuzi

Tarehe December 7, 2015
Rais Dkt.John Pombe Magufuli.
Rais John Pombe  Magufuli  leo amemsimamisha  kazi katibu mkuu wizara ya uchukuzi Bw.Shabani Mwinjaka.
Licha ya kumfukuza kazi Katibu Mkuu amevunja bodi yote ya Bandari na kutengua uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi mkuu wa bandari Bw. Awadhi Massawe, Mwenyekiti wa bodi ya bandari pamoja maofisa 8 wa bandari na kuagiza wawekwe chini ya Ulinzi.
Habari kamili itafuata hivi punde.

CCM wajitokeza Kuzungumzia Kasi ya Rais Magufuli

CCM wajitokeza Kuzungumzia Kasi ya Rais Magufuli

Tarehe December 7, 2015
Rais John Pombe Magufuli.
Rais John Pombe Magufuli.
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimejitokeza kwa mara ya kwanza na Kumpongeza Rais John  Magufuli katika utendaji wake tangu aingie madarakani mapema novemba,2015.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es Salaam, Ramadhan Madabida amesema kuwa CCM inamuunga mkono hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Rais John Magufuli za kutumbua majipu.
Wamempongeza kwa  kubana matumizi ya umma, kuziba mianya ya rushwa, kupiga vita ubadhirifu wa mali ya umma na kurejesha nidhamu na uwajibikaji kwenye taasisi za umma na nchi kwa ujumla.
Wenyeviiti hao  wamemuomba Rais Magufuli aendeleze kasi yake ya kutekeleza majukumu yake na asisite kuwawajibisha watendaji wote wazembe wanaozalisha kero ya utoaji huduma duni kwa wananchi.
Madabida alisema katika kampeni zilizoendeshwa kote nchini, Dk Magufuli aliahidi Watanzania watakapomchagua kuwa Rais atatekeleza kwa juhudi na maarifa masuala ya kuondoa umasikini; kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira hasa kwa vijana; kuendeleza vita dhidi ya adui rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma na kuendelea kudumisha amani, ulinzi na usalama kwa maisha ya wananchi na mali zao. Kwa upande mwingine  wenyeviti hao wamefadhaishwa na vitendo vya vilivyofanywa na wabunge wa kambi ya Upinzani vya kupiga kelele na kusababisha kutolewa nje kabla ya Dk Magufuli kutoa hotuba yake Bungeni  hivi karibuni.

Kasi ya Rais Magufuli yawakumba Omba Omba Dar es salaam

Kasi ya Rais Magufuli yawakumba Omba Omba Dar es salaam

Tarehe December 6, 2015
Omba omba katika moja ya eneo jijini Da res salaam.
Omba omba katika moja ya eneo jijini Da res salaam.
Kasi ya Rais John  Magufuli ime endelea kutikisa katika maeneo mbalimbali ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Ndugu Said Mecky Sadiki amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za jiji la Dar es Salaam, kuwaondoa ombaomba wote walioko katika barabara za jiji.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Sadiki  amesema kwamba utekelezaji wa kauli ya Rais John Magufuli ya kutumia siku ya Desemba 9 mwaka huu kufanya usafi, utakwenda sambamba na kuwaondoa ombaomba hao, ambao wanachangia kuongeza uchafu.
“Siwezi kusema wao ni uchafu lakini mazingira yanayowazunguka katika maeneo wanayofanyia shughuli zao wanayachafua, wanajisaidia kwenye mifuko na kutupa ovyo,” alisema.

Amesisitizia  Wakurugenzi hao kuhakikisha kuwa ombaomba hao hawarudi mjini kutokana na kuwa na mazoea wakiondolewa kurudi tena katika maeneo hayo.
Licha ya timua timua hiyo kuwakumba  Omba omba wapiga debe  nao wameunganishwa katika kundi la watakao ondolewa  kufuatia kuwa kero kwa abiria.

Kasi ya Rais Magufuli yawatimua Vigogo 7 Tanecso

Kasi ya Rais Magufuli yawatimua Vigogo 7 Tanecso

Tarehe December 6, 2015
Makao makuu ya Shirika la Umeme Tanzania.
Makao makuu ya Shirika la Umeme Tanzania.
Kasi ya Rais John Pombe Magufuli ime endelea kushika kasi katika kuwashughulikia watendaji wazembe ambapo Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limewatimua kazi  wafanyakazi 7 kutokana na makosa mbalimbali.
Kwa mujibu wa Taarifa ya Tanesco imebainisha kuwa imewachukulia hatua wafanyakazi ambao wamekuwa wakitoa huduma  mbaya na kuwa Kero kwa wateja zikiwemo lugha mbaya, wateja kudaiwa rushwa kabla ya kupewa huduma, kucheleweshewa huduma na ubadhirifu.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa katika kipindi cha miezi miwili Shirika limewaachisha kazi maofisa 7 waandamizi kutokana na makosa mbali mbali ikiwemo wizi na ubadhirifu.
Aidha, Miongoni mwao ni wale waliofikishwa mahakamani kule Kagera na kuripotiwa na vyombo vya habari jana. Walioachishwa kazi ni pamoja na wafanyakazi wa ngazi za Mameneja, Wahandisi na Wahasibu.


Taarifa hiyo imesisitiza kuwa  Shirika linaendelea na uchunguzi na mfanyakazi ye yote atakayebainika analaghai wateja, anadai rushwa, anatoa lugha chafu au huduma mbovu atawajibishwa mara moja na pale atakabobainika    ataachishwa kazi.
Kwa upande mwingine shirika hilo limesema kwamba ili kuendana na agizo la Rais Magufuli la kufanya usafi Desemba 9 nchini Wafanyakazi wote wa TANESCO watashiriki katika shughuli mbali mbali za usafi wa mazingira katika maeneo yote yanayozunguka ofisi, mitambo na vituo nchi nchi nzima.

Makampuni 41 yatajwa ukwepa kodi Sakata la makontena 329

Makampuni 41 yatajwa ukwepa kodi Sakata la makontena 329

Tarehe December 6, 2015
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA,Phillip Mpango.
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA,Phillip Mpango.(katikati) akizungumza na wanahabari.
Mamlaka ya Mapato Nchini (TRA)  imeyataja majina ya kampuni 41 na wamiliki wa makontena 329 ambayo yalipitishwa bandarini bila kulipiwa ushuru.
Kaimu Kamishna Mkuu wa TRA, Dk. Philip Mpango alisema Mamlaka hiyo iliagizwa na Waziri Mkuu Majaliwa kuchukua hatua mara moja kwa kufuatilia na kubaini wamiliki wa Bandari Kavu (ICD) zilizohusika katika kashfa hiyo.
Bidhaa zilizokuwemo ndani ya makontena hayo ni pamoja na matairi ya magari, samani mbalimbali, betri za magari, vifaa vya ujenzi, nguo na bidhaa zingine mchanganyiko.
Dk. Mpango aliyataja majina ya makampuni na watu binafsi na idadi ya makontena waliyopitisha bila kulipia ushuru ambayo ni kama ifuatavyo;

Wednesday 25 November 2015

Rais Kenyatta aongoza wananchi kumpokea Papa Francis

Rais Kenyatta aongoza wananchi kumpokea Papa Francis

Tarehe November 25, 2015
Papa Francis akiwa na mwenyeji wake Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta.
Papa Francis ambaye ni Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amewasili nchini Kenya leo na kupokewa na mwenyeji wake Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta katika uwanja wa Ndege wa Kimaataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.
Ziara ya Kiongozi huyo mkubwa Duniani  kwa nchi ya Kenya inatarajiwa kuwa  siku tatu  kuanzia leo.
Alipotua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta ( JKIA ), kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki Duniani alilakiwa na mwenyeji wake Rais Uhuru Kenyatta.
Ziara ya Papa Francis nchini Kenya ni mwanzoni mwa ziara yake ya Afrika itakayomchukua pia hadi nchini Uganda na baadaye Jamuhuri ya Afrika ya Kati.

Kibadeni asema sasa ni kazi tu

Kibadeni asema sasa ni kazi tu

Tarehe November 25, 2015
Abdallah Kibaden
Abdallah Kibaden
Kocha wa Timu ya Taifa bara (Kilimanjaro Stars) Abdallah Kibadeni amesema kuwa atahakikisha timu yake inaendelea na kasi ya wimbi la ushindi katika michuano ya Chalenge na kusisitiza kikosi hicho kitakua kinafanya kazi Tu.
Kibadeni alisema hayo wakati akihjiwa na kituo cha televisheni cha Super Sport baada ya mechi kati ya Kilimanjaro Stars na Rwanda kumalizika kwa matokeo ya 2-1 ambapo Stars ilishinda mchezo huo.
Kibadeni alisema kuwa michuano ni migumu lakini aoni sababu ya timu yake kushindwa kutwaa ubingwa huo sababu anakikosi kizuri ambacho anakiamini.
katika mechi ya awali Stars ilitandika Somalia bao 4-0.

BOT yarejesha Chenji za Sarafu

BOT yarejesha Chenji za Sarafu

Tarehe November 25, 2015
Benki Kuu ya Tanzania.
Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imerejesha huduma ya chenji za sarafu ili kukidhi mahitaji ya chenji ya sarafu kwa wananchi pamoja na wafanyabiashara.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa huduma za Kibenki wa Benki kuu ya Tanzania (BOT), Martin Kobelo amesema hatua hiyo inafuatia kuadimika kwa sarafu ya shilingi 50, 100, 200,na 500 katika mzunguko wa fedha kwa watu na wafanyabiashara.
Amesema benki kuu imeanzisha dirisha la utoaji wa chenji za sarafu ambalo litaanza kufanya kazi kwa miezi sita ya mwanzo ili kuona kama uhitaji wa sarafu utaendelea kuwepo au utapungua.
<a href='https://mpakasi.com/ads/www/delivery/ck.php?n=a08724c9&cb=Math.random()' target='_blank'><img src='https://mpakasi.com/ads/www/delivery/avw.php?zoneid=19&source=https%3A%2F%2Fmpakasi.com&cb=Math.random()&n=a08724c9' border='0' alt='' /></a>
Akizungumzia utaoaji chenji Kobelo amesema huduma hiyo ya chenji sasa  itatolewa kikanda ambapo itatolewa na Benki kuu makao makuu na katika matawi yake ya Mikoa ya Arusha, Mbeya, Mwanza na Zanzibar.
Kwa upande mwingine amesema kuwa huduma ya chenji ni bure kwa wananchi wote na hutolewa mara mbili kwa wiki, Jumanne na Alhamisi kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa sita mchana.

Waziri mkuu akerwa kusuasua Mabasi yaendayo kasi


Waziri mkuu akerwa kusuasua Mabasi yaendayo kasi

Tarehe November 25, 2015

Waziri mkuu Mhe.Kassim Majaliwa amekerwa na kusua sua kwa mradi wa mabasi yaendayo kwa kasi  licha kuwa mabasi kadhaa yalianza kufanya kazi siku kadhaa zilizopita jijini Dar es salaam.
Kutokana na kusua sua huko  ambako hakuendani na kauli mbiu ya ‘Hapa Kazi Tu’ Majaliwa ameitisha kikao ofisini kwake leo saa 4 asubuhi akitaka kupatiwa taarifa ni kwa nini mradi wa mabasi yaendayo kasi (DART) haujaanza kazi hadi sasa.
“Ninataka kupata haya maelezo kwa sababu Watanzania na hasa wana-Dar es salaam, wamesubiri kwa muda kuona mradi ukianza kazi ili uondoe kero ya usafiri. Wao wanajua anayehusika ni TAMISEMI,”aliongeza.

Watakao jieleza mbele ya Waziri mkuu ni Katibu Mkuu, Mkurugenzi Mkuu DART na watendaji wake wote pamoja na watu wengine wanaohusika katika utekelezaji mradi huo.
Baaada  ya kujieleza watatakiwa  kutoa majibu ya lini  Mabasi hayo yataanza kazi, je ni nani anakwamisha na hata kama ni sheria, ni kwa nini wasitafute namna  kuondoa hivyo vikwazo.

Sunday 22 November 2015

Liverpool ni noma,waitandika Man City 4-1

Liverpool ni noma,waitandika Man City 4-1

Tarehe November 21, 2015
wachezaji wa Liverpool wakishangilia
Liverpool wameibuka kidedea baada ya kuwashushia Manchester City mvua ya magoli 4-1 katika mchezo wa ligi kuu uliomalizika mapema jioni ya leo.
Eliaquim Mangala aliipatia Liverpool goli la kwanza dakika ya 8 ya mchezo na Phillippe Coutinho aliipatia bao la pili liverpool dakika ya 23 kabla ya Roberto Firmino kuipatia Liverpool goli la tatu katika dakika ya 32 na mpaka mapumziko Liverpool walikuwa mbele kwa 3-0
Dika ya 44 Sergio Aguero aliisawazishia Man City na kupatia goli la kwanza lakini matumaini yao yalizimwa na Martin Skrtel baada ya kuipatia Liverpool goli la nne dakika ya 81 na mpaka dakika ya 90 liverpool walikua mbele kwa 4-1

Real Madrid yapigwa 4-0 na Barcelona,Suarez atupia mbili

Real Madrid yapigwa 4-0 na Barcelona,Suarez atupia mbili

Tarehe November 21, 2015

Mshamburiaji wa Barcelona Luis Suarez akishangilia bao dhidi ya ya Real Madrid.
Real Mardid leo imepokea kipigo cha Mmbwa mwizi kutoka kwa maasimu wao wakubwa klabu ya Barcelona baada ya kukubali kipigo cha magoli 4-0 katika mchezo uliomalizika jioni ya leo.
Luis Suarez alikuwa wakwanza kuzitingisha nyavu za Real Madrid kwa kufunga goli dakika ya 11 ya mchezo huo kabla ya Neymar kuipatia Barcelona goli la pili dakika ya 39 na mpaka dakika 45 za kwanza Barcelona walikuwa mbele kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili Andres Iniesta aliipatia Barcelona goli la tatu dakika ya 53 na dakika ya 74 Luis Suarez alirudi tena kambani na kuifungia Barcelona goli la nne,mpaka dakika ya 90 Barcelona walikuwa mbele kwa mabao 4-0.

Monday 16 November 2015

Mkwasa: nitashinda mapema Algeria

Mkwasa: nitashinda mapema Algeria

Tarehe November 16, 2015

.
Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Charles Boniface Mkwasa amesema atahakikisha timu yake inapata ushindi wa mapema katika mchezo wa marudiano dhidi ya Algeria utakaochezwa kesho.

Stars imeondoka jana usiku nyuma ya Algeria mara baada ya mchezo huo kumalizika kuelekea nchini Algeria tayari kwa ajili ya marudiano.

 Mkwasa alisema kuwa sasa nguvu zake anazielekeza katika mchezo huo ili kuhakikisha wachezaji wake wanatengeza nafasi na kuzitumia ipasavyo ili kupata ushindi wa mapema.

Alisema kwa sasa anaimani kubwa na kikosi chake kutokana na  mchezo mchezo waliouonesha katika uwanja wa Taifa.
Alisema kuwa kwa kuwa hakuna muda wa kupumzika na wa mazoezi magumu atahakikisha anatumia muda uliopo ili kuondoa kasoro zilizowakosesha magoli katika mchezo wa awali.

“Kikubwa ni kutengeneza nafasi na kuhakikisha tunazitumia ipasavyo ili kuweza kuondoka na ushindi wa mapema kwani tutahakikisha tunapambana zaidi ya tulivyopambana Taifa”, alisema Mkwasa.

Akizungumzia mchezo uliopita Mkwasa alisema kuwa ni kweli kuwa mabadiliko aliyoyafanuya kipindi cha pili yalikuwa na makosa yaliyopelekea Algeria kurudisha magoli na mchezo kuisha kwa sare ya 2-2.

Alisema, lengo la kufanya mabadiliko ni kuongeza nguvu na kasi ya mchezo lakini kwa bahati mbaya ilikuwa kinyumena matarajio yao.

“Wachezaji wetu wamecheza vizuri ila tulifanya makosa kwa kufanya mabadiliko kwasababu timu ilikuwa inaongoza lakini mchezo ndivyo ulivyo na nafikiri bado tuna safari mbele yetu na ninavyowatazama hawa nyumbani kwao watabadilika”, alisema Mkwasa.

Mkwasa alisema kuwa watanzania waendelee kuwa na imani kwani Algeria wanafungika na sivyo kama walivyokuwa wakiwasikia kuwa ni timu ngumu kutokana na wachezaji wake 18 wanaounda kikosi hicho kuchezea barani Ulaya.

Tuesday 10 November 2015

Chama kipya cha Siasa chaanzishwa nchini

Chama kipya cha Siasa chaanzishwa nchini

Tarehe November 10, 2015
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini amewataka  viongozi wa chama kipya  cha siasa nchini Tanzania  cha Tanzania Patriotic Front (TPF-Mashujaa) kuzingatia  Katiba na sheria ya vyama vya siasa.
Akizungumza  ofisini kwake Dar es Salaam jana, Jaji Mutungi alisema kumekuwa na ongezeko la vyama vya kisiasa nchini na wengine wameanzisha kama mchezo wa kuigiza, wanafanya udanganyifu na kukiuka Sheria, Katiba na Kanuni za vyama vya siasa.
Amewapongeza waasisi wa chama kipya cha kwa dhamira yao ya dhati kwa kuanzisha chama baada ya Uchaguzi Mkuu kumalizika kwa kuwa  wameonesha wana  dhamira ya dhati ya kuanzisha chama kitakacholeta mabadiliko.
Mmeacha uchaguzi upite, maana ingekuwa mnataka madaraka pekee, mngeanza kabla ya uchaguzi,” alisema Jaji Mutungi kabla ya kukabidhi cheti cha usajili wa muda kwa waasisi hao, Denatus Mutani na Optatus Likwelile.
Nao, waanzilishi wa chama hicho, Mutani (Mwenyekiti wa muda) na Likwelile (Katibu wa muda), waliahidi kwa nyakati tofauti kuwa watasimamia ipasavyo sheria na kanuni za usajili pamoja na Katiba ya nchi. Chama hicho kimedai kinalenga kuwaelimisha Watanzania kuwa siasa ni maisha badala ya kudhani kuwa lengo ni kushika madaraka fulani pekee.
Msajili alisema kutokana na usanii wa kuanzisha vyama kiholela mpaka sasa kuna vyama 22 vyenye usajili wa kudumu nchini na vingine kadhaa visivyo na usajili.

HESLB yawatangazia neema wanafunzi vyuo vikuu

HESLB yawatangazia neema wanafunzi vyuo vikuu

Tarehe November 10, 2015
Moja ya chuo kikuu nchini Tanzania.
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza kutoa mikopo kwa waombaji wenye sifa wapya 40,836 kati ya waombaji 50,830  mwaka wa masomo wa 2015/2016 walio omba mikopo hiyo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Bodi hiyo, George Nyatega amesema  hadi sasa imekwishawapangia mikopo jumla ya waombaji mikopo wenye sifa 40,836 wa mwaka wa kwanza kwa mwaka wa masomo 2015/2016.
“Majina ya waombaji waliofanikiwa kupata mikopo kutoka katika awamu zote mbili yanapatikana kupitia mtandao wa Bodi wa olas.heslb. go.tz na tovuti ya Bodi (www.heslb. go.tz),” alisema Nyatega
Katika awamu ya kwanza, HESLB ilitoa orodha yenye jumla ya waombaji 12,282 waliopata mikopo hiyo ikifuatiwa na waombaji wengine wapya 40,836.
Bodi hiyo imewasihi waombaji wa mikopo kuwa watulivu wakati mchakato wa upangaji wa mikopo kwa wanafunzi wenye sifa unaendelea.
Ameongeza kuwa  orodha hizo pia zimetumwa vyuoni kwa ajili ya taratibu za usajili  huku lengo la Bodi hiyo likiwa  ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza wenye sifa ya kupata mikopo katika mwaka wa masomo 2015/2016 ambao ni 50,830, wote wanapata mikopo.
Katika hatua nyingine Nyatega aliwataka Watanzania kupuuza taarifa zisizo za kweli zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kwamba, HESLB, haitatoa mikopo kwa waombaji wapya.

Wenger atangazwa kocha bora mwezi Oktoba

Wenger atangazwa kocha bora mwezi Oktoba

Tarehe November 10, 2015
Meneja wa Arsen,Arsenal Wenger
Meneja wa Arsenal ,Arsene Wenger ametajwa kama kocha bora wa mwezi Octoba katika ligi kuu ya Uingereza ( Barclays Premier League )
Wenger alikuwa kiungo muhimu kwa washika bunduki hao wa uingereza kwa kuanza na ushidni wa 3-0 dhidi ya mahasimu wao manchester United pia alishinda dhidi ya  Watford, Everton na Swansea City pia aliisaidia Arsenal kutoa droo na Manchester City.
“Ni vizuri kwani ina nikumbusha pia baada ya kushindwa kwa magoli matano kwa moja dhidi ya Baryen Munich lakini inaonyesha atujafanya vibaya sana katika mwezi uliopita”amesema Wenger

Viera apata ulaji kuinoa New York City, asaini miaka mitatu

Viera apata ulaji kuinoa New York City, asaini miaka mitatu

Tarehe November 10, 2015
Patrick Viera
Patrick Viera  (39) aliyewahi kutesa na timu za Arsenal na Manchester city zinazoshiriki ligi kuu ya Uingereza amepata shavu ya kuinoa timu ya New York City.
Vieira amesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuifundisha timu hiyo ambayo inakipiga katika ligi kuu ya soka nchini marekani.
Vieira ataanza majukumu yake rasmi Januari 1, 2016 akiwa na kibarua cha kuiongoza timu hiyo kufanya vizuri katika ligi ya Marekani.

Samatta awafunga tena waalgeria,Tp Mazembe watwaa ubingwa wa Afrika

Samatta awafunga tena waalgeria,Tp Mazembe watwaa ubingwa wa Afrika

Tarehe November 9, 2015
Mshabuliaji wa Kimataifa wa Tanzania na Klabu ya Tp Mazembe Mbwana Samatta akishangilia mara baada ya kufunga goli
Mbwana Samatta ameendelea kufanya vema na kuitangaza Tanzania katika soka la kimataifa na leo amedhihirisha ubora wa kiwango chake baada ya kuifungia timu yake ya TP Mazembe  goli moja na kuseti goli la pili  na kuondoka na ushindi wa magoli 2-0  dhidi ya USM Alger ya Algeria katika fainali za klabu bingwa Afrika.
Tp Mazembe wametangazwa mabingwa wa Klabu Bingwa Afrika baada ya kuinyuka USM Alger jumla ya mabao 4-1.
Samatta alifunga goli lake katika dakika ya 75 ya kipindi cha pili baada ya kuangushwa kwa Rogger Asale katika eneo la hatari.
Mchezo huo ulikuwa wa marudiano ambapo mchezo wa awali mazembe walishinda mabao 2-1 na Samatta alifunga goli moja kwa mkwaju wa penati.

Rais Kagame ‘aishutumu’ Burundi kisa mauaji ya Raia

Rais Kagame ‘aishutumu’ Burundi kisa mauaji ya Raia

Tarehe November 9, 2015
Rais wa Rwanda Paul Kagame pamoja na Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza.
Rais wa Rwanda Paul Kagame ameshutumu vikali viongozi wa Burundi kutokana na mauaji yanayoendelea nchini humo na kuonya kuwa huenda kukatokea mauaji ya halaiki
Kagame ameshangaa ni vipi viongozi wa taifa hilo jirani “wanaweza kuruhusu wananchi wao kuuawa kiholela.
Rais Kagame alisema hayo Ijumaa, lakini hotuba  yake haikutangazwa hadi mwishoni mwa wiki  wakati  akihutubia katika hafla ya kuwatunuku Wanyarwanda waliosaidia kuwaficha na kuwaokoa Watutsi wakati wa mauaji ya kimbari 1994 pamoja na wanaharakati wanaotetea umoja na maridhiano miongoni mwa Wanyarwanda.
Akizungumza kwa Kinyarwanda Rais Kagame alisema: ”Tazama nchi jirani kama Burundi, maisha yao yamesimama kabisa. Lakini sababu ni ipi? Wana historia inayofanana na yetu. Ila viongozi wao wapo kwa ajili ya kuua wananchi kuanzia asubuhi hadi jioni.”
Rais akijifungia sehemu isiyojulikana, hakuna anayejua sehemu alikojificha, hakuna anayezungumza naye, huyo anaongoza watu vipi?” alisema Bw Kagame,
”Watu wanakufa kila siku, maiti zinazagaa  barabarani  kinachosikitisha ni kuwa bara la Afrika lina ugonjwa wake lenyewe kiasi kwamba hata nitalaumiwa eti nimekosea kuitaja nchi nyingine, eti ningechezea diplomasia au siasa. Siyo haki mimi nitasema wazi”Alisema Kagame
Amesisitiza  kuwa Viongozi wanashinda wakiua watu, maiti zinatapakaa sehemu zote; wakimbizi wanarandaranda sehemu  watoto, wanawake kisha wanasema ni siasa. Hiyo ni siasa gani?”Amehoji Kagame.
Uhusiano kati ya Rwanda na Burundi umekuwa wa kusua sua  sana tangu Bw Nkurunziza atangaze kuwa atawania urais kwa muhula wa tatu, hatua iliyopingwa na wapinzani. Katika hatua nyingine Mwezi uliopita, Burundi ilimuondoa  Balozi mmoja kutoka Rwanda ikimtuhumu kwa kuhujumu usalama wa nchi hiyo.

Friday 6 November 2015

Mikutano ya CCM, Chadema yapigwa marufuku nchini

Mikutano ya CCM, Chadema yapigwa marufuku nchini

Tarehe November 7, 2015
Wafuasi wa CCM na UKAWA, pande mbili kubwa zinanzochuana katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 25.
Wafuasi wa CCM na UKAWA, pande mbili kubwa zilizochuana katika Uchaguzi mkuu wa Oktoba 25.
Jeshi la Polisi limepiga marufuku maandamano na mikutano ya vyama vya siasa iliyokuwa imepangwa kufanyika kwa nyakati tofauti kwa madai ya kuwepo na hali tete ya  kisiasa.
Kwa mujibu wa  msemaji wa Jeshi la Polisi, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP), Advera Bulimba amesema, polisi imefikia hatua hiyo kutokana na hali ya kisiasa ilivyo kwa sasa.
Amesema  vyama vya CCM na Chadema tayari vilikuwa vimeshawasilisha maombi ya kufanya mikutano na maandamano sehemu mbalimbali hapa nchini.
SSP Bulimba ameongeza  kuwa,  kwa mujibu wa tathmini iliyofanywa na vyombo vya usalama nchini  hali ya kisiasa kwa sasa nchini bado si nzuri kwani bado kuna mihemko mikubwa ya kisiasa kufuatia uchaguzi mkuu uliomalizika wiki iliyopita.
“Baadhi ya Vyama vya Siasa vimekuwa vikiomba kufanya mikutano ya hadhara na maandamano nchi nzima kwa siku moja na vingine maandamano yasiyo na kikomo. Katika hali ya kawaida hili halikubaliki,”amesema SSP Bulimba na kuongeza:
Amesisitiza kuwa tathmini iliyofanywa na vyombo vya usalama imebaini kuwa bado kuna mihemko mikubwa ya kisiasa  hivyo kufanyika mikutano hiyo kunaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Jeshi la Polisi nchini bado linasisitiza katazo lake la awali la mikutano na maandamano hadi hapo hali ya kisiasa itakapotengamaa.”Amesema Bulimba
Kwa upande mwingine Jeshi hilo limetoa wito kwa wananchi kuendelea kuwa watulivu na kujiepusha na vitendo vya uvunjifu wa amani na kuwasihi kuendelea na shughuli zao za maendeleo.

Magufuli aanza kwa kuwashitukiza Wizara ya Fedha

Magufuli aanza kwa kuwashitukiza Wizara ya Fedha

Tarehe November 6, 2015
Rais Dkt.Magufuli akiwa Wizara ya fedha kukagua utendaji kazi wa watumishi wa wizara hiyo.
Rais Dkt.Magufuli akisaini kitabu cha wageni Wizara ya Fedha jijini Dares salaam leo.
Rais Dkt.John Pombe Magufuli leo ameanza kazi kwa kuwashitukiza watendaji wa wizara ya fedha.Aidha, Magufuli ametembea kwa miguu kutoka Ikulu jijini Dar es salaam hadi wizara ya Fedha akiwa ameongozana na maofisa wa usalama ambapo mara baada ya kufika katika ofisi ya Wizara ya Fedha aliwakuta maofisa wengine wakiwa nje ya ofisi zao.
Inadaiwa huenda akatembelea wizara nyingine za serikali yake kujionea utendaji kazi wa wafanya kazi katika serikali yake mpya ya awamu ya tano.

JK awasamehe wafungwa 4,160 akiaga Ikulu

JK awasamehe wafungwa 4,160 akiaga Ikulu

Tarehe November 6, 2015
Rais mstaafu wa awamu wa nne Dkt.Jakaya Kikwete.
Wafungwa 4,160 wamepata msamaha kutoka kwa aliyekuwa Rais wa awamu ya nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliyekabidhi nchi kwa rais mpya Dkt.John Pombe Magufuli aliyeapishwa jana jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mathias Chikawe kwa vyombo vya habari jana Dar es Salaam imebainisha kuwa  kati ya wafungwa hao, wafungwa 867 wataachiwa huru na wafungwa 3,293 watapunguziwa vifungo vyao na kubaki gerezani wakitumikia sehemu ya vifungo vyao vilivyobaki.
Amewataja walionufaika na msamaha huo kuwa ni wafungwa wote wapunguziwe moja ya sita ya vifungo vyao zaidi ya punguzo la kawaida linalotolewa chini ya Kifungu cha 49(1) cha Sheria ya Magereza Sura ya 58 isipokuwa wafungwa walioorodheshwa katika ibara ya 1 (i-xix).
Wafungwa  wengine kuwa ni wafungwa wagonjwa wenye magonjwa kama Ukimwi, kifua kikuu, saratani ambao wako kwenye hatua ya mwisho ambao watathibitishwa na waganga chini ya Mganga mkuu wa mkoa au wilaya.
Ameongeza kuwa  wazee wenye umri zaidi ya miaka 70, wafungwa wa kike walioingia na mimba gerezani na walioingia na watoto wanaonyonya na wasionyonya na walemavu wa mwili na akili na ulemavu huo uthibitishwe na jopo la waganga.
Katika hatua nyingine taarifa hiyo imesema kuwa msamaha hautawahusu wafungwa wenye adhabu za kunyongwa, waliohukumiwa kunyongwa na adhabu hiyo baadaye kubadilishwa kuwa kifungo cha maishaau kifungo gerezani.
Wengine ni wafungwa waliotumikia kifungo kwa makosa ya usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya, makosa yanayohusu uombaji, upokeaji na utoaji rushwa, unyang’anyi na kujaribu kutenda makosa hayo, kubaka, kulawiti au kujaribu kutenda makosa hayo. Aidha, makosa mengine ambayo vifungo vyake haviko kwenye msamaha huo ni makosa ya kuwapa mimba wanafunzi, wizi wa magari, pikipiki au kujaribu kutenda makosa hayo, matumizi mabaya ya madaraka, waliowahi kupunguziwa vifungo na Rais.
Wafungwa wengine  ni  wanaotumikia vifungo kwa makosa ya wizi na ubadhirifu wa fedha za Serikali, kutoroka au kujaribu kutoroka wakiwa chini ya ulinzi halali na wafungwa wanaotumikia vifungo chini ya Sheria ya Bodi ya Parole Sheria Namba 25 ya Mwaka 1994 ya Sheria ya Huduma kwa Jamii Namba 6 ya Mwaka 2002.

Thursday 5 November 2015

Rais Magufuli awataka wagombea wenzake kuweka itikadi pembeni


Rais Magufuli awataka wagombea wenzake kuweka itikadi pembeni

Tarehe November 5, 2015

John Pombe Joseph Magufuli (56) akiapishwa kuwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Sherehe za kumuapisha Magufuli zilihudhuriwa na viongozi wa ndani na nje ya nchi akiwemo Rais Rorbert Mugabe wa Zimbabwe,Joseph Kabila wa Congo,Paul Kagame wa Rwanda,Jacob Zuma wa Afrika Kusini na Raila Odinga wa Kenya.
Baada ya kuapishwa na Jaji Mkuu wa Tanzania Jaji Othaman Chande Rais John Magufuli alitoa neno la shukrani kwa watanzania na kuwataka washindani wake saba waliokuwa wakichuana katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 mwaka huu kuweka   itikadi za vyama  pembeni na kushirikiana kwa  kufanya kazi kwa maslahi ya Taifa zima.
Amesema kuwa kwa kuwa uchaguzi umekwisha ni vema viongozi hao wakaweka itikadi,maslahi na matakwa yao binasfi kando na kuungana nae kujenga taifa imara.
“Uchaguzi umekwisha na Rais ni mimi John Magufuli sasa ni wakati wa kufanya kazi tu…na nitafanya kazi kwa nguvu zangu zote na kwa kumtanguliza Mungu mbele,”alisema Rais
Magufuli.
Ameongeza kuwa dhamana waliyopata kutoka kwa watanzania ni kubwa sana na ni jukumu la Serikali ya awamu ya tano kuhakikisha wanatekeleza ahadi zote walizotoa wakati wa
kampeni walipokuwa wakiomba ridhaa ya kuliongoza taifa.
Rais Magufuli hakusita kumshukuru Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Wiliam Mkapa ambaye alimteua kuwa waziri wa Ujenzi kwa kipindi chake chote cha miaka 10 wakati huo akiwa na umri wa miaka 35 tu.
Pia alimshukuru Rais Mstafu wa awamu ya nne Dkt Jakaya Mrisho Kikwete ambaye naye alimchagua kuwa waziri katika Serikali yake na baadae akiwa Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kumpa dhamana ya kupeperusha bendera ya chama hico na kuwa Rais wa tano wa Jamhuri ya Muungano ya watu wa Tanzania. Magufuli ni nani? alihoji na kuendelea kusema..mpaka achaguliwe na kuaminiwa kuliongoza Taifa hili….nakosa maneno mazuri ya kuongea lakini leo sio sehemu ya kutoa hutuba nipo hapa kushukuru tu,amesema Rais Magufuli.

clouds stream