Saturday 31 December 2016

Liverpool yaendeleza ubabe kwa vigogo wenzake, Wijnaldum akiua man city.

img-20161130-wa0008

Liverpool: Mignolet 6, Clyne 7, Lovren 6.5, Klavan 7, Milner 6.5, Can 7, Henderson 7 (Origi 64, 5.5), Wijnaldum, Mane 6.5 (Lucas 89, 5), Lallana 9, Firmino 6.

Subs not used: Karius, Sturridge, Moreno, Ejaria, Alexander-Arnold.

Yellow cards: Klavan, Can

Goal: Wijnaldum 8 


Man City: Bravo 5.5, Zabaleta 6 (Jesus Navas 86, 5), Otamendi 6, Stones 6.5, Kolarov 5.5, Fernandinho 6.5, Toure 7 (Iheanacho 89, 5), Sterling 5.5, Silva 6.5, De Bruyne 6.5, Aguero 5. 

Subs not used: Sagna, Fernando, Caballero, Clichy, Garcia.

Attendance: 53,120 

 

Referee: Craig Pawson 7




 






CHELSEA YAENDELEA KUMFUKUZA MWIZI KIMYAKIMYA, YAITWANGA STOKE CITY 4-2 NA KUJISHINDILIA KILELENI


 
img-20161130-wa0008

Chelsea: Courtois 6, Azpilicueta 6, Luiz 6, Cahill 6.5, Moses 5 (Ivanovic 82, 5), Kante 6, Fabregas 8 (Matic 73, 6), Alonso 6, Willian 8.5 (Chalobah 84), Hazard 8, Costa 7.5

Subs: Begovic, Zouma, Loftus-Cheek, Batshuayi.

Goals: Cahill 34, Willian 57, 65, Costa 85.

Booked: Moses, Fabregas, Alonso.


Stoke City: Grant 8, Johnson 6, Shawcross 6, Martins Indi 7, Diouf 5, Allen 6, Adam 7, Pieters 7, Afellay 4(Bojan 6.5), Crouch 7, Shaqiri 5(Imbula 6) 

Subs: Bardsley, Whelan, Bony, Imbula, Given, Krkic, Sobhi.

Goals: Martins-Indi 46, Crouch 64. 

Booked: Diouf, Adam. 

Referee: Robert Madley 6

 





 


Ban Ki-moon akamilisha muda wake UN

Ban Ki-moon akamilisha muhula wake katika Umoja wa Mataifa ambapo amehudumu kama katibu mkuu

Ban Ki-moon akamilisha muhula wake katika Umoja wa Mataifa ambapo amehudumu kama katibu mkuu
img-20161130-wa0008

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayestaafu, Ban Ki-moon, ameondoka makao makuu ya Umoja wa Mataifa , kwa mara ya mwisho baada ya muhula wake wa mwongo mzima.

Bwana Ban Ki-moon anamaliza kazi rasmi, mwaka mpya unapoingia.

Alisema atakuwako Medani ya Times mjini New York, kuukaribisha mwaka, na kuadhimisha kumaliza kazi.

Alifanya mzaha kwamba mamilioni ya watu watakuwa wakiangalia wakati akipoteza kibarua chake.

Pahala pake panachukuliwa na waziri mkuu wa zamani wa Ureno, Antonio Guterres.

Bwana Ban anatarajiwa kurudi Korea Kusini, ambako kuna tetesi, kwamba huenda akagombea nafasi ya Rais Park Geun-Hye, ambaye anashtakiwa.

Makubaliano ya kisiasa nchini DR Congo yakwama

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Joseph Kabila
img-20161130-wa0008

Makubaliano ya kisiasa kati ya serikali na upinzani nchini DR Congo ili kumaliza mgogoro wa kisiasa yamekwama katika dakika ya mwisho.

Muhula wa rais Joseph Kabila ulikamilika mapema mwezi huu ,lakini uchaguzi umeahirishwa huku makumi ya watu wakipoteza maisha yao katika maandamano.

Wapatanishi kutoka kanisa Katoliki awali walikuwa wamesema kwamba pande hizo mbili zilikuwa zinakaribia maafikiano ambapo rais Kabila atasalia mamlakani hadi uchaguzi utakapoandaliwa mwishoni mwa 2017 .

Hatahivyo baadhi ya makubaliano hayakuafikiwa hivyobasi kuahirisha sherehe ya kutia kandarasi makubaliano hayo huku mazungumzo yakiendelea.


Wednesday 28 December 2016

ULIISIKIA HII YA MAMBO KUMUENDEA POA IBRAHIM AJIBU KULE MISRI?

Image result for ibrahim hajibu

img-20161130-wa0008

Kiungo Ibrahim Ajibu sasa ana hadi nafasi ya asilimia 70 kupata nafasi ya kuitumikia Haras El Hodood ya Misri.

Ajibu amepasi vipimo vya afya, maana yake nafasi ya kukipiga nchini Misri ni kubwa kama ambavyo taarifa zimeeleza.

Amepewa muda wa wiki moja na nusu wa majaribio na unaisha Desemba 31.

Abdel Haidar anayejishughulisha na masuala ya afya katika timu hiyo ya Jeshi la Misri, amezungumza na Championi kutoka Alexandria Misri na kusema hiyo ni hatua kubwa kwa Ajibu.

“Amefuzu vipimo vya afya. Hii ni hatua kubwa zaidi, sasa yamebaki masuala baadhi ambayo yanamhusu kocha.

“Kocha sasa anaendelea naye na mwisho atatoa maelezo kuhusiana na suala la vipimo vya afya,” alisema Haidar.

Wakati Haidar anasema hivyo, Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Usajili ya Simba, Kassim Dewji amesema wanasubiri kuhusiana na Ajibu hadi Desemaba 31.

“Taarifa za maendeleo yake tunazifuatilia kwa karibu kabisa. Tunajua hilo la vipimo vya afya lakini sisi hatutalizungumzia kwa kuwa anaendelea na majaribio hadi Desemba 31.

“Baada ya hapo, tunaamini timu hiyo itaanza mawasiliano nasi. Hivyo nafikiri mgevuta subira,” alisema Dewji maarufu mama Gwiji ambaye amewahi kuwa katibu mwenezi wa kikosi cha Simba kilichotinga fainali ya Caf mwaka 1993 na katibu mkuu wakati Simba ikiing’oa Zamalek Klabu Bingwa Afrika mwaka 2003.

Kama Ajibu atakuwa amefuzu vipimo vya afya maana yake ni sawa na kufuzu kuichezea timu hiyo kwa asilimia 80.

Hata hivyo, kama atafuzu na kujiunga nayo atakuwa na kazi ngumu kuhakikisha anapambana kuisaidia kurejea Ligi Kuu Misri baada ya kuwa imeshuka msimu uliopita.

Kwa Tanzania, Haras El Hood kwa kile kipigo cha mabao 5-1 ilichokitoa kwa Simba katika michuano ya Ligi ya Mabingwa.

Yanga Wailaza Ndanda 4-0 Shamba La Bibi

Domald Ngoma akiwahi kuupiga  mpira mbele ya beki wa Ndanda, Bakari Mtama uwanja wa uhuru Dar es salaam.
Domald Ngoma akiwahi kuupiga mpira mbele ya beki wa Ndanda, Bakari Mtama uwanja wa uhuru Dar es salaam.
img-20161130-wa0008

Klabu ya Yanga leo imejipatia pointi tatu muhimu baada ya kuifunga Ndanda ya Mtwara mabao 4­0 katika mchezo wa ligi kuu Vodacom uliochezwa uwanja wa Uhuru jijini Dares salaam.

Kufuatia ushindi huo Yanga SC inafikisha pointi 40 ikizidiwa pointi moja na watani wao, Simba SC ambao kesho watacheza na klabu ya Ruvu Shooting.

Katika mchezo huo Mshambuliaji Donald Dombo Ngoma alifunga mabao mawili mfululizo, Amissi Joselyn Tambwe alifunga bao la tatu na beki Mtogo, Vincent Bossou akafunga la nne kipindi cha pili.

AZAM FC IMEWATIMUA MAKOCHA WAKE WOTE RAIA WA HISPANIA

 

 makocha-azam-fc
Azam FC imemtimua Kocha wake Mkuu, Zeben Hernandez.


img-20161130-wa0008

Zeben na makocha wengine raia wa Hispania, wametimuliwa kazi leo baada ya Azam FC kwenda mwendo wa kusuasua.

Azam FC iko katika nafasi ya nne ikiwa na pointi 27 baada ya kucheza mechi 17.

Katika mechi 17 za Ligi Kuu Bara, Azam FC imechinda mechi saba, imepoteza nne na sare sita, hali ambayo wazi inaonekana kutoufurahisha uongozi wa Azam FC hata kidogo.

Afariki dunia, siku moja baada ya kifo cha binti yake

Debbie Reynolds na binti yake Carrie Fisher

Debbie Reynolds na binti yake Carrie Fisher
img-20161130-wa0008

Msanii wa Hollywood Debbie Reynolds amefariki akiwa na umri wa miaka 84, siku moja tu baada ya kifo cha binti yake, Carrie Fisher.

Alikimbizwa hospital baada ya kushikwa na ugonjwa nyumbani kwa mtoto wake wa kume huko Beverly Hills.

Debbie Reynolds ama Mary Frances, umaarufu wake ulikuwa mwaka 52, wakati alipofanya tamasha sambamba na Gene Kelly katika wimbo uliojulikana kama ''..Singin' in the Rain..''

Alikuwa pia ni muigizaji wa sanaa ya vichekesho

Netanyahu aipinga hotuba ya Kerry kuhusu makazi

Ujenzi wa Makaazi ya Wayahudi

Ujenzi wa Makaazi ya Wayahudi
img-20161130-wa0008

Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani John Kerry ameutetea uamuzi wa nchi yake wa kuliwezesha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuupitisha uamuzi wa wiki iliyopita, kutangaza Makazi ya Wayahudi kuwa ni kitendo kilicho kinyume na sheria.

Waziri Kerry amesema hatua hiyo ina nia ya kulinda uamuzi wa kuwepo kwa mataifa mawili ili kuzuia hatari ambayo ingeweza kutokea.

Amesema bila ya usalama wa Israel na uwepo wa Palestina, Israel hakutakuwa na amani kamili.

Lakini hata hivyo, Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ameelezea kuvunjwa moyo na hotuba iliyotolewa na John Kerry kuhusiana na jambo hilo, ambayo ameielezea kuwa haijakaa sawa.

Amesema ukweli ni kwamba Wapalestina wamekataa kukubali uwepo wa Israel.

Kwa upande wake, Rais wa Palestina Mahmoud Abbas amesema atakuwa tayari kurudi katika mazungumzo pale tu Israel itakapoacha kujenga makaazi  mapya ya wananchi wake katika eneo la Wapalestina.

Tuesday 27 December 2016

Vigogo 6 EPL Wanavyokabana Koo Baada Ya Mechi Za Jumatatu

15626182_1555185534505856_946559447888641148_o
img-20161130-wa0008

30 Wafa Maji Baada Ya Boti Kuzama

da5
img-20161130-wa0008
Polisi nchini Uganda wanasema takriban watu 30 wamekufa maji baada ya boti yao kuzama katika ziwa Albert magharibi mwa taifa hilo.
Abiria wengi walikuwa wanasoka na mashabiki wao waliokuwa wakielekea katika mechi ya kirafiki ya kuadhimisha siku ya Krismasi.
Mafisa wa polisi wamesema chombo hicho kilikuwa kimejaa kupita kiasi huku abiria wakiimba na kupiga tarumbeta.

Mkulima Apigwa Mshale Na Kutokea Shingoni Mikumi, Prof. Jay Atoa Tamko


Mkulima mmoja wa Kitongoji cha Upangwani Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata ya Masanze JImbo la Mikumi Morogoro aliyepigwa mkuki.
Mkulima mmoja wa Kitongoji cha Upangwani Kijiji cha Dodoma Isanga, Kata ya Masanze JImbo la Mikumi Morogoro aliyepigwa mkuki.(Tahadhari Picha zinatisha)
img-20161130-wa0008

Migogoro ya Wakulima na Wafugaji isiyokwisha Mkoani Morogoro imepelekea mkulima aliyejulikana kwa jina la Augustino Mtitu kupigwa mshale mdomoni na kutokea shingoni na Mfugaji wa Kimasai jana.

Kwa mujibu wa tarifa ya Katibu Ofisi ya Mbunge Prof. Jay Bw. Robert A. Galamona imebainisha kuwa Kijana huyo Augustino Mtitu alishambuliwa na wafugaji wa kimasai alipokuwa akimsaidia jirani yake kufukuza Ng’ombe wasiharibu mazao shambani kwake. 

Mkulima huyo kwa alikimbizwa hospitali ya wilayani Kilosa na baadae alipelekwa hospitali ya mkoa Morogoro ili kufanyiwa operesheni ya kuondoa mkuki huo na matibabu zaidi.

Aidha, Kipande cha mti kinachoonekana (pichani) mdomoni ndiyo mkuki uliokatwa ili kupunguza urefu wa mkuki huo wakati wakimkimbiza hospitali, Inasemekana MwenyeKiti wa kijiji na MwenyeKiti wa kitongoji hicho nao wamejeruhiwa katika tukio hilo.

Ofisi Ya Mbunge Mikumi, Profesa Jay imetoa wito kwa Serikali kuwabaini wale wote waliofanya kitendo hiki cha kinyama kuhakikisha wanachukuliwa hatua kali za kisheria ili kuweza kukomesha vitendo hivi vya kujichukulia sheria mkononi inayopelekea kuongezeka kwa uvunjifu mkubwa wa Amani na migogoro isiyokwisha kati ya wakulima na wafugaji wilayani Kilosa.

Mkuliwa aliyepigwa mshale mdomoni na kutokezea Shingoni.
Mkuliwa aliyepigwa mshale mdomoni na kutokezea Shingoni
Mkulima huyo akipelekwa Hospitali.
Mkulima huyo akipelekwa Hospitali.

Sunday 25 December 2016

Msako mkali ndege ya Urusi waendelea

Urusi

Rais Vladmir Putin wa Urusi
img-20161130-wa0008

Msako mkali unaendelea kutafuta miili ya askari wa Urusi walio waliokuwemo kwenye ndege iliyopata ajali kwenye bahari nyeusi iliyoanguka na kuua askri wote tisni na mbili waliokuwemo .

Wafanyakazi zaidi ya elfu tatu, wakiwemo wazamiaji zaidi ya elfu moja wako kwenye harakati za utafutaji manusura ama maiti za askari hao katika eneo la tukio.

Ndege iliyokuwa imebeba askari hao ilianguka dakika tatu baada ya kuanza safari kutoka katika mji wa Sochi ikiwa njiani kuelekea nchini Syria.

Abiria walio wengi walikuwa ni askari wa Urusi waliokuwa katika shamra shamra za sherehe za tamasha la kimuziki la Alexandrov wanaojulikana kama kwaya ya jeshi jekundu.

Ibada ya kuwaombea marehemu hao imefanyika mjini Sochi na miji mingine tofauti tofauti kabla ya siku maalumu ya Jumatatu iliyotangazwa kuwa ya maombolezo.

Mamlaka nchini Urusi zimetoa tamko kuwa zinafahamu fika wapi ilipo ndege hiyo katika bahari nyeusi. Mpaka sasa miili saba ya askari imepatikana .Mpaka sasa hakuna taarifa zozote za kuwepo kwa manusura wa ajali hiyo.

Msemaji wa wizara ya ulinzi nchini Urusi, Igor Konashenkov, amesema kwamba zoezi la utafutaji linaendelea.

Gereza kuu la Kigali lateketea kwa moto

Gereza kuu la Kigali maarufu 1930

Gereza kuu la Kigali maarufu 1930
img-20161130-wa0008

Gereza kuu la Kigali maarufu 1930 lateketea kwa moto. kufikia leo jioni moshi inaendelea kutanda. Kilichosababisha moto huo hakikajulikana.

Shughuli za kuzima moto bado zinaendelea huku vikosi vya Askari Jeshi na polisi vikionekana hapa na pale kando kando mwa jengo la gereza hilo.

 Hilo Ni gereza linalohifadhi wafungwa wa mchanganyiko wale wa kisiasa na wengine wa mauaji ya kimbari. Miongoni mwa wafungwa wa kisiasa Ni Victoire Ingabire aliyehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela miaka 4 iliyopita Kwa hatia ya kuchochea utengano wa kikabila na kuhatarisha usalama wa raia.

Viongozi kadhaa serikalini wamefika kwenye eneo la tukio wakiwemo mawaziri na wakuu wa jeshi na polisi.

Bado Ni mapema kujua athari zilizotokana na tukio hilo kwani waandishi wa habari hawajaruhusiwa kuingia katika jengo la gereza kuu ya Kigali.

Magari ya zima moto bado yanapishana na magari ya kubeba majeruhi huku wafungwa wakionekana nje ya gereza na ulinzi ukiwa umeimarishwa.

Papa Francis: Ataka amani baina ya Israel na Palestina

Papa Francis ametoa wito kufanywe juhudi mpya kuleta amani baina ya Waisraeli na Wapalestina

Papa Francis ametoa wito kufanywe juhudi mpya kuleta amani baina ya Waisraeli na Wapalestina
img-20161130-wa0008

Papa Francis ametoa wito kufanywe juhudi mpya kuleta amani baina ya Waisraeli na Wapalestina.

Katika hotuba yake ya Krismasi, aliyotoa Vatikani, Papa alizihimiza pande mbili zinazohusika, kujaribu kuazimia kuandika ukurasa mpya, na kumaliza chuki na kulipizana kisasi.

Kiongozi huyo wa kanisa katoliki pia ametaka kumalizwa kwa vita nchini Syria akisema ni wakati wa silaha kunyamazishwa.

Katika ujumbe wake wa Krismasi kiongozi wa kanisa la Anglikana duniani Askofu mkuu Justin Welby amewataka raia kumuomba mungu ili kukabiliana na ugaidi.

Aidha amesema kuwa mengi yanapaswa kufanya ili kukabiliana na ukosefu wa usawa.

Thursday 22 December 2016

Watu 34 wadaiwa kufariki katika maandamano DR Congo

Maandamano nchini DRC ambapo takriban watu 34 wanahofiwa kufariki kulingana na shirika la Human Rights Watch

Maandamano nchini DRC ambapo takriban watu 34 wanahofiwa kufariki kulingana na shirika la Human Rights Watch

Shirika la kibinaadamu la Human Rights Watch linasema kuwa vikosi vya usalama ini DR Congo vimewaua takriban watu 34 wakati wa maandamano wiki hii.

Mazungumzo yanayoendeshwa na kanisa katoliki yanaendelea mjini Kinshasa ,ili kujaribu kumaliza mgogoro katika ya upinzani na rais Joseph Kabila ambaye alikataa kuondoka madarakani wakati muda wake ulipokamilika siku ya Jumatatu.

Kuna ripoti tofauti kwamba watu wengine 17 wameuawa kaskazini magharibi mwa Congo.

Maafisa wa polisi wanadaiwa kukabiliana na wanachama wa kundi moja la madhehebu linaloamini kwamba mwisho wa utawala wa Kabila ndio mwanzo wa mwisho wa dunia.

Wakati huohuo Mamlaka nchini DRCongo imewakamata watu kadhaa katika mji wa pili kwa ukubwa nchini humo, Lubumbashi.

Meya wa mji huo anasema kwamba wanajeshi walikuwa wakiwakamata wahalifu, japo wenyeji wa mji huo wanasema waliokamatwa ni vijana wanaoshukiwa kupinga utawala wa rais Joseph Kabila.

Kamusi ya kiswahili sasa imo kwenye mtandao.

kiswahl

img-20161130-wa0008

Mambo sasa ni ya kidijitali na mtandaoni tu. Hata ukitaka kutafuta neno lolote la kiswahili hauna haja ya kuangalia kwenye kitabu. Kamusi ya kiswahili sasa imo kwenye mtandao.

Shirika la uchapishaji la Oxford University Press imezindua kamusi hii ya kiswahili kama njia moja wapo ya kukienzi kiswahili.

Ili kuhamu zaidi kuhusi kamusi hii mwandishi wetu Odhiambo Joseph amezungumza na Bw John Mwazemba, Mkurungenzi mkuu wa Oxford University Press , Africa Mashariki

Tuesday 20 December 2016

Goli la Mane laibeba Liverpool

Liverpool

Wachezaji wa Liverpool wakishangilia ushindi
img-20161130-wa0008

Majogoo wa Anfield Liverpool wameendelea kuwa na msimu mzuri katika ligi kuu ya England baada ya ushindi wa bao 1-0 katika mchezo wa dabi dhidi ya Everton.

Mshambuliaji nyota wa Majogoo hao Sadio Mane ndie aliyeipatia timu yake alama tatu muhimu baada ya kufunga bao pekee la ushindi, katika mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Goodson Park.

Kwa ushindi huo Liverpool, wanapanda mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi wakiwa na alama 37 huku wakiwa wamecheza michezo 17 ya ligi.

Chelsea wanasalia katika nafasi ya kwanza wakiwa na alama 43.

Marekani: Wajumbe waidhinisha ushindi wa Donald Trump

Donald Trump akihutubu Crown Coliseum mnamo December 6, 2016 eneo la Fayetteville, North Carolina.

Donald Trump sasa amehakikishiwa kuwa Rais wa 45 wa Marekani
img-20161130-wa0008

Wajumbe wa Jopo la Kuamua Mshindi wa Urais nchini Marekani wamemuidhinisha Donald Trump kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Novemba.

Hii ni licha ya juhudi za dakika za mwisho za kutaka kumzuia kuingia ikulu ya White House mwezi Januari.

Wiki sita baada ya uchaguzi mkuu kufanyika tarehe 8 Novemba, mwanachama huyo wa Republican amepata zaidi ya kura 270 za wajumbe ambazo alikuwa anahitaji kufanya rasmi ushindi wake.

Baada ya ushindi huo, Bw Trump ameahidi "kufanya kazi kuunganisha nchi yetu na kuwa rais wa Wamarekani wote".

Wajumbe walikuwa wametumia ujumbe mwingi kupitia barua pepe na pia kupigiwa simu wakihimizwa kutomuunga mkono bilionea huyo kabla yao kukutana kupiga kura.

Shughuli yao ya kupiga kura kwa kawaida huwa kama shughuli ya kutimiza wajibu tu, ambapo huwa wanamuidhinisha mshindi, lakini mwaka huu uchaguzi umegubikwa na tuhuma za kuingiliwa na wadukuzi kutoka Urusi.

Jimbo la Texas hatimaye lilimuwezesha kufikisha idadi ya kura 270 za wajumbe alizohitaji,, licha ya wajumbe wawili wake kugeuka na kupiga kura kumpinga.

Gazeti la New York Times pia linaripoti kwamba kuna wajumbe wanne wa chama cha Democratic, chake Hillary Clinton, ambao walimpigia kura mgombea mwingine lakini Bi Clinton.

Matokeo ya kura hiyo yatatangazwa rasmi tarehe 6 Januari kwneye kikao maalum cha pamoja cha bunge la Congress.

"Nawashukuru Wamarekani kwa kunipigia kura kwa wingi kuwa rais wa Marekani," Bw Trump alisema kupitia taarifa baada ya matokeo kutangazwa.

"Kwa hatua hii ya kihistoria, tunaweza sasa kutazama mbele na kutarajia maisha ya kufana siku za usoni. Nitafanya kazi kwa bidii kuunganisha nchi yetu na kuwa rais wa Wamarekani wote," alisema.

Donald Trump used Twitter to thank his supporters and take a swipe at the mediaDonald Trump used Twitter to thank his supporters and take a swipe at the media

Makamu wa rais mteule Mike Pence alimpongeza mkubwa wake kwa ushindi kupitia Twitter, na kuandika: "Hongera kwa @realDonaldTrump; ameteuliwa rasmi kuwa Rais wa Marekani leo na Jopo la Kuamua Mshindi wa Urais." 

Aliongeza kwamba ni heshima kubwa kwake kuchaguliwa kama makamu wa rais wa Marekani.

Ujumbe wake kwenye Twitter ulipendwa sana na kusambazwa mara nyingi mtandaoni.

Waliokuwa wanafanya juhudi za kumzuia Bw Trump walikuwa wamepigana vikali kuwashawishi wajumbe wa chama cha Republican kutomuunga mkono mgombea wa chama chao.

Mamilioni ya Wamarekani walitia saini ombi mtandaoni kuwahimiza wajumbe hao kutomuunga mkono Bw Trump.

Siku ya kufanyika kwa uchaguzi, maelfu ya watu wanaompinga Trump walikusanyika na kuandamana katika miji mikuu ya majimbo kote nchini humo.

Waandamani Augusta, Maine wakimpinga Trump
Waandamani Augusta, Maine wakimpinga Trump

Katika jimbo la Pennsylvania, zaidi ya waandamanaji 200 walivumilia baridi kali na kuandamana wakiimba, "Hatutaki Trump, hatutaki KKK, hatutaki Wafashisti Marekani!" na "Hatutaki uhaini, hatutaki Trump".

Jimbo la Maine, waandamanaji walipiga ngoma na kubeba mabango yaliyosema, "Msiache Putin Aamue Rais Wetu," - wakirejelea tuhuma kwamba wadukuzi walioungwa mkono na serikali ya Urusi walijaribu kuvuruga uchaguzi kumfaa Bw Trummp.

Kimsingi, waliokuwa wanampinga Bw Trump hawakuwa na nafasi ya kuzuia ushindi wake.

Ndipo waweze kumzuia kuingia ikulu, wangehitaji kuwashawishi wajumbe 38 wa chama cha Republican kubadili msimamo wao.

Na hilo huenda labda lingechelewesha tu ushindi wake.

Iwapo kungetokea iwe kwamba hakuna mgombea aliyefikisha kura 270 za wajumbe, Bunge la Wawakilishi ndilo lingekuwa na jukumu la kuamua nani angekuwa rais.

Ikizingatiwa kwamba bunge hilo linadhibitiwa na chama cha Republican, bila shaka wangemchagua Bw Trump.

Mwandamanaji mjini Los Angeles akiwahimiza wajumbe 18 Desemba 2016
Mwandamanaji mjini Los Angeles akiwahimiza wajumbe

Monday 19 December 2016

China yarejesha chombo cha Marekani

Chombo cha USNS Bowditch kilikuwa kikifanya utafiti

Chombo hicho kilikuwa kinatumiwa na maafisa wa meli ya USNS Bowditch kufanya utafiti
img-20161130-wa0008

Marekani imethibitisha kwamba China imerejesha chombo cha baharini ambacho kilikuwa kimetwaliwa kutoka kwenye bahari ya South China Sea.

Kutwaliwa kwa chombo hicho kulikuwa kumetishia kuvuruga uhusiano kati ya Marekani na Uchina.

Chombo hicho ni cha kufanya utafiti baharini.

Maafisa wa Pentagon wanasema chombo hicho kisicho na nahodha kilisalimishwa kwa maafisa wa Marekani karibu na pahala ambapo kilitwaliwa, kilomita 92 kaskazini magharibi mwa Ghuba ya Subic.

Taarifa ya Marekani imesema maafisa wake wataendelea "kupaa, kuendesha vyombo vya baharini, na kuhudumu katika bahari ya South China Sea" maeneo yanayoruhusiwa na sheria za kimataifa.

Baada ya kutwaliwa kwa chombo hicho, Rais Mteule wa Marekani Donald Trump aliituhumu China kwa kutekeleza wizi.

Manuwari ya Marekani iliokamatwa na China
Chombo cha Marekani kilichokamatwa na China (cha rangi ya manjano)

Baadaye, alipendekeza China waruhusiwe kukaa na chombo hicho.

clouds stream