Sunday 12 November 2017

Taarifa Muhimu Kutoka Bodi Ya Mikopo Kwa Wanafunzi Elimu Ya Juu



Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul Razaq Badru



Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza orodha nyingine yenye wanafunzi 1,775 wa Mwaka waKwanza waliofanikiwa kupata mikopo na hivyo kufanya jumla ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza waliopangiwa mikopo hadi sasakufikia 31,353.

Katika Awamu ya Kwanza, wanafunzi 10,196 wa mwaka wa kwanza walipangiwa mikopo, Awamu ya Pili wanafunzi 11,481, nasasa Awamu ya Tatu wanafunzi 7,901.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana (Jumapili, Novemba 12, 2017) na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru, orodha kamili ya wanafunzi hao inapatikana katika tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz) na pia imetumwa kwa vyuo husika jana ili kuwawezesha wanafunzi kufanya usajili na kuendelea na masomo.

“Tumekua tukifanyia kazi orodha za udahili ambazo tumekuwa tukipokea, na kila tunapokamilisha, tunatoa orodha za wanafunzi waliopangiwa mikopo ambao wana sifa – leo tumetoa hao 1,775,” amesema Badru.

Aidha, Badru amekumbusha kuwa kiasi cha shilingi bilioni 427.54 zimetengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi kwa mwaka 2017/2018 na tayari Serikali imeshatoa shilingi 147.06 bilioni kwa ajili ya robo ya kwanza ya mwaka huu wa 2017/2018.

Fedha hizo, shilingi bilioni 427.54, ni kwa ajili ya jumla ya wanafunzi 122,623 wa mwaka wa kwanza na wale wanaoendelea na masomo.

Wakati huohuo, HESLB imetangaza kufungua dirisha la rufaa kuanzia leo, Jumatatu, Novemba 13, 2017 hadi Novemba 19, 2017 ili kuwapa fursa waombaji wote ambao hawajaridhika na upangaji wa mikopo kuwasilisha rufaa kupitia vyuo walivyopata udahili.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji huyo wa HESLB, lengo la HESLB ni kuhakikisha wanatangaza orodha ya majina ya waombaji mikopo waliofanikiwa katika rufaa zao ifikapo au kabla ya tarehe 30 Novemba mwaka huu.

“Tunatoa wito kwa uongozi wa vyuo vyote kupokea maombi ya rufaa za wanafuzi na kuwasilisha kwa Bodi ya Mikopo kabla ya Novemba 22, 2017 ili kuiwezesha Bodi kutoa orodha ya waombaji waliofanikiwa katika rufaa zao ifikapo Novemba 30, 2017,” amesema Badru katika taarifa yake.

Maelezo ya kina kuhusu utaratibu wa kuwasilisha rufaa yatatolewa kupitia tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz).

Mgomo Mabasi Mikoani Wanukia, Wananchi Waaswa Kutokata Tiketi




Taswira nzima ya mabasi yaendayo Mikoani na Nchi Jirani katika Kituo cha Ubungo.



Chama cha Wamiliki wa Mabasi yaendayo Mikoani na Nchi Jirani Tanzania (TABOA), kimewataka wananchi kutokata tiketi za kusafiri kwa siku ya kesho, Jumanne, kufuatia mgomo wa mabasi hayo.

Katibu Mkuu wa TABOA, Enea Mrutu amesema hayo kupitia Mkutano Mkuu Maalum wa TABOA na kudai kuwa maamuzi ya mgomo huo ni katika kuwashinikiza wabunge kutopitisha sheria kandamizi dhidi ya wamiliki wa mabasi.

Amesema sheria hiyo ni kandamizi kwakuwa inashindwa kutofautisha kosa la mmiliki wa basi na dereva.

“Tunaomba radhi wateja wetu wote kwa kuwanyima huduma lakini kimsingi sheria hiyo ndiyo inayowanyima huduma,” amesema.

Ameongeza kuwa vita yao kubwa ni sheria ambayo haikutenganisha makosa baina ya dereva na mmiliki wa chombo husika na kupelekea kumfunga mmliki kwa kosa linalomhusu dereva.

“Tulisema sheria hiyo ibainishe makosa ili kosa linalomhusu dereva liende kwa dereva na lile linalomhusu mmiliki liende kwa mmiliki lakini wenzetu hawakusikia hivyo tumesema watu wasikate tiketi na Jumanne ndio mwisho wa kutoa huduma,” amesisitiza.

Lema Atoa Ushauri Kuhusu ‘Wabunge Wa Lipumba’



Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.



Mbunge wa Arusha Mjini, Mhe. Godbless Lema amemshauri Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai kutumia busara kuwaondoa bungeni wabunge nane walioingia bungeni kuziba nafasi za wabunge nane waliokuwa wamevuliwa uanachama wa Chama cha Wananchi (CUF) Julai 24, mwaka huu.

Lema ametoa ushauri huo kupitia mtandao wake wa kijamii ikiwa ni siku chache tu baada ya Mahakama Kuu kutengua uamuzi wa
kufukuzwa kwa Wabunge 8 na Madiwani 2 wa CUF mpaka pale shauri la msingi litakaposikilizwa.

“Mh Spika anapaswa kuzingatia kwa busara uamuzi uliotolewa na mahakama kwa kuwaondoa wale Wabunge wa Lipumba ndani ya Bunge na kuwarejesha Wabunge halali sasa, mpaka hapo haki itakaposhinda zaidi,”ameandika Lema.

Wabunge hao nane walivuliwa uanachama Julai 24 na Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la Chama cha Wananchi, CUF linaloongozwa na Prof. Lipumba kwa madai ya utovu wa nidhamu yakiwemo kukisaliti chama hicho na Tume ya Uchaguzi (NEC) kuteua wabunge wengine kutokana na uamuzi huo na kuchukua nafasi zao maramoja.

Thursday 9 November 2017

Papa Francis apiga marufuku uuzaji wa sigara Vatican

Licha ya sigara kuiletea mamilioni ya fedha Vatican ,papa Francis amesema kuwa hawezi kuruhusu binaadamu kuathiriwa kiafyaLicha ya sigara kuiletea mamilioni ya fedha Vatican ,papa Francis amesema kuwa hawezi kuruhusu binaadamu kuathiriwa kiafya

Papa Francis ameagiza marufuku ya uuzaji wa sigara ndani ya Vatican , kuanzia mwaka ujao.

Msemaji wa Vatican Greg Burke alisema kuwa mji huo mtakatifu hauwezi kukubali na kitendo ambacho kinahatarisha maisha ya binaadamu.

Takriban wafanyikazi 5000 wa Vatican na wale waliostaafu wanaruhusiwa kununua sigara zilizopunguzwa bei .

Mauzo hayo yanakadiriwa kuiletea Vatican mamilioni ya yuro kila mwaka.

Lakini bwana Burke amesema kuwa hakuna faida ambayo ni halali iwapo sigara zinaathiri afya za wanaadamu.

Mtoto amvua kofia Papa Francis

Alinukuu takwimu za shirika la afya duniani WHO ambazo zinalaumu uvutaji sigara kwa kusababisha vifo vya takriban watu miioni 7 duniani kila mwaka.

''Nadhani watu wengi wanapenda sigara kwa sababu ya ufadhili wanaopata'' ,alisema.

''Ni kitu ambacho ni lazima kufutilia mbali licha ya kuleta mapato Vatican, muhimu ni kufanya kile kilicho sawa''.

Papa Francis ambaye pafu lake moja liliondolewa wakati alipokuwa kijana havuti sigara.

Wafanyikazi wa vatican na wale waliostaafu wanaruhusiwa kununua pakiti tano za sigara kila mwezi kutoka kwa duka lisilotozwa ushuru.

Aliyedaiwa Kununua Nyumba Za Lugumi Akamatwa Na Polisi



Moja ya nyumba hizo za Lugumi.



Mtu aliyedaiwa kujitokeza leo na kufanikiwa kununua nyumba mbili za Mfanyabiashara, Said Lugumi, Dkt. Luis Shika amekamatwa na Jeshi la Polisi baada ya kushindwa kutoa asilimia 25 ya fedha kama yalivyo masharti ya mnada. Mnada huo sasa unarudiwa tena muda huu.

Awali mtu huyo aliyefika mnadani hapo akiwa amevaa suruali, shati, tai na makobazi (sandals) alidaiwa kufanikiwa kununua nyumba hizo mbili za Mfanyabiashara, Said Lugumi zilizopo Mbweni, Jijini Dar es Salaam kwa Shilingi Bilioni 1.1 na Shilingi Milioni 900 kupitia kampuni ya udalali ya Yono.

Nyumba hizo zinauzwa kwa njia ya mnada kufuatia deni alilokuwa akidaiwa Lugumi na Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambapo katika mnada wa awali nyumba hizo zilikosa wateja kutokana na bei yake kuwa juu sana.


Dkt. Luis Shika.

Rais Magufuli Awasili Uganda Kwa Ziara Ya Siku 3





Rais, Dkt. John Pombe Magufuli leo amewasili nchini Uganda kwa ziara ya siku 3 kwa mwaliko wa Rais, Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kukamilisha siku 4 za ziara yake Mkoani Kagera.

Kwa pamoja, marais hao wataweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa Bomba la kusafirishia Mafuta kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga, Tanzania.

Thursday 2 November 2017

Tottenham yaichapa Real Madrid 3-1 yatinga 16 bora

Dele Alli alikuwa katika kiwango kizuri cha mchezo

Dele Alli alikuwa katika kiwango kizuri cha mchezo

Dele Alli alifunga mara mbili na kushuhudia Tottenham Hotspur ikiichapa miamba ya Hispania na mabingwa watetezi wa kombe la klabu bingwa Ulaya Real Madrid na kufanikiwa kutinga hatua ya 16 bora.

Real Madrid wamefungwa kwa mara ya kwanza katika hatua ya makundi tokea mwaka 2012.

Christian Eriksen aliiandikia Spurs goli la tatu na la ushindi na kuizamisha kabisa Madrid ambayo itahitaji kushinda michezo iliyosalia ili kufuzu hatua inayofuata.

Goli la Madrid lilipachikwa na Cristiano Ronaldo ambaye licha ya kufunga goli hilo hakuwa katika kiwango kizuri sana.

Spurs wamefikisha alama 10 huku Madrid ikiwa na alama 7.

Mahakama Yasitisha Uchaguzi Liberia






Mahakama ya juu zaidi nchini Liberia imeamrisha maandalizi ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais kusitishwa kufuatia madai ya udanganyifu kutoka kwa mgombea aliyeondolewa kutokana na kinyanganyiro hicho.

Mcheza soka wa zamani George Weah na Makamu wa Rais Joseph Boakai wanatarajiwa kukutana katika duru hiyo ya pili ya Uchaguzi Novemba 7, mwaka huu.

Lakini mgombea wa chama cha Liberty Charles Brumskine, ambaye alishika nafasi ya tatu amepinga matokeo hayo ya awali akituhumu kuwa kulikuwa na udanganyifu.

Uchaguzi wa mwezi uliopita ndio wa kwanza huru kufanyika tangu kukamilika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2003 nchini humo.

Mahakama imeamrisha chama cha Liberty na tume ya uchaguzi nchini humo kupeleka kesi zao ifikapo Alhamisi.

Lakini msemaji wa Tume ya Uchaguzi, Henry Flomo amenukuliwa akisema kuwa hajajulishwa rasmi kuhusu amri hiyo ya mahakama.

Waangalizi wa kimataifa wakiwemo wale kutoka muungano wa Ulaya hawajaelezea hitilafu yoyote wakati wa duru ya kwanza ya uchaguzi.

Mahakama Yasitisha Uchaguzi Liberia






Mahakama ya juu zaidi nchini Liberia imeamrisha maandalizi ya duru ya pili ya uchaguzi wa urais kusitishwa kufuatia madai ya udanganyifu kutoka kwa mgombea aliyeondolewa kutoka kinyanganyiro hicho.

Mcheza soka wa zamani George Weah na Makamu wa Rais Joseph Boakai wanatarajiwa kukutana katika duru hiyo ya pili ya  Uchaguzi Novemba 7, mwaka huu.

Lakini mgombea wa chama cha Liberty Charles Brumskine, ambaye alishika nafasi ya tatu amepinga matokeo hayo ya awali akituhumu kuwa kulikuwa na udanganyifu.

Uchaguzi wa mwezi uliopita ndio wa kwanza huru kufanyika tangu kukamilika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2003
nchini humo.

Mahakama imeamrisha chama cha Liberty na tume ya uchaguzi nchini humo kupeleka kesi zao ifikapo Alhamisi.

Lakini msemaji wa Tume ya Uchaguzi, Henry Flomo amenukuliwa akisema kuwa hajajulishwa rasmi kuhusu amri hiyo ya
mahakama.

Waangalizi wa kimataifa wakiwemo wale kutoka muungano wa Ulaya hawajaelezea hitilafu yoyote wakati wa duru ya kwanza ya uchaguzi.

NASA Kuanza Maandamano Kupinga Serikali Ya Kenyatta






Muungano wa Upinzani nchini Kenya (NASA) umesema kuwa una mpango wa kuanza kufanya maandamano kuanzia wiki ijayo yenye lengo la kuonyesha kutoitambua serikali.

Hili linajiri siku chache baada ya Taifa hilo kufanya uchaguzi wa marudio uliofanyika Oktoba 26, mwaka huu na kususiwa na Mgombea wa NASA, Raila Odinga na kushuhudiwa Rais, Uhuru Kenyatta akitangazwa kuwa mshindi na Rais Mteule wa Kenya.

Aidha,NASA imepanga orodha ya bidhaa na huduma zitakazo susiwa na wafuasi wake ikiwa ni pamoja na majengo ya kibiashara ambayo yametundikwa picha ya Rais Kenyatta na kuamuru wafuasi wake wasifanye biashara ama miamala na benki moja maarufu nchini humo.

Hatahivyo, Viongozi wa Jubilee wamemtaka kinara wa NASA, Raila Odinga kulegeza msimamo wake ili kulisaidia taifa hilo kusonga mbele.

NASA wamesema maandamano hayo yatakuwa ya amani na wametoa mafunzo kwa watu watakaoyaongoza ili yasidhuru
wananchi wengine.

Wednesday 1 November 2017

UEFA: Man U yaichapa Benfica 2-0


Kwa mara ya mwisho Daley Blind kufunga goli ilikuwa Desemba 2016Kwa mara ya mwisho Daley Blind kufunga goli ilikuwa Desemba 2016

Manchester United ikiwa nyumbani katika dimba la Old Trafford imefanikiwa kuichapa Benfica 2-0 na kwa mara ya kwanza ndani ya miaka minne inaweza kuingia katika hatua ya mtoano.

United ambayo imeingia katika mashindano hayo kwa kuchukua kikombe cha ligi ya Europa msimu uliopita wameshinda michezo yote minne waliocheza na hivyo wanahitaji alama moja pekee katika michezo miwili iliyosalia ili kuweza kufuzu moja kwa moja.

Anthony Martial, ambaye alikuwa tishio katika mchezo huo, alikosa mkwaju wa penalti baada ya kuangushwa katika eneo la hatari na Douglas na mkwaju wake kuchezwa na mlinda mlango wa Benfica Mile Svilar ambaye alikuwa katika kiwango kizuri.

Licha ya kushindwa kufunga mkwaju wa penalti, Antony Martial alionyesha kiwango boraLicha ya kushindwa kufunga mkwaju wa penalti, Antony Martial alionyesha kiwango bora

Svilar aliokoa pia mikwaju miwili mikali ya Mbelgiji mwenzake Romelu Lukaku kabla ya kujifunga goli la kwanza baada ya mkwaju mkali wa Nemanja Matic kumgonga mgongoni.

Marcos Rashford aliyeingia kipindi cha pili aliongeza mashambulizi zaidi kwa upande wa Manchester United na kusababisha penalti ambayo ilifungwa vyema na Daley Blind.

Benfica ilionyesha kiwango kizuri lakini mlinda mlango wa Man U David de Gea aliokoa mikwaju yao yote.

Kwa matokeo hayo Man U inaongoza ikiwa na alama 12, huku Benfica ikiburuta mkia na alama 0.

Mshambuliaji awaua watu 8 kwa kuwagonga kwa gari New York

Marekani

Shambulizi nchini Marekani baisikeli na miili ya watu ilitapakaa ardhini



Meya wa mji wa New York, Bill De Blasio, amearifu kwamba watu 8 wamefariki dunia na zaidi ya 12 wamejeruhiwa na gari iliyowagonga waendesha baiskeli mjini humo.

Bill amelielezea tukio hilo kuwa la ugaidi lililosababisha hofu mjini humo.

Kamishna wa polisi wa jiji wa New York, James O'Neill, amemuelezea mtu aliyetekeleza tukio hilo kuwa ni kijana wa miaka 29 aliyekuwa anaendesha gari ndogo la kubebea mizigo alilokuwa amelikodi.

Alisema gari hilo liliwagonga watembea kwa miguu na wapanda baiskeli kabla ya kugongana na basi la shule.

Kwa upande wake bwana O'Neill, amesema kuwa dereva wa gari hilo alitoka ndani ya gari lake na kuanza kuandaa silaha mbili kwa ajili ya shambulizi na kabla ya hilo, polisi walimuwahi na kumpiga risasi zilizomjeruhii.
Marekani

Gari lililosababisha tukio hilo

Polisi mjini humo wametoa tamko kwamba wanalichukulia tukio hilo kama shambulizi la kigaidi , Mtuhumiwa wa tukio hilo alichukuliwa na polisi kwa mahojiano zaidi ambao walithibitisha taarifa hizo katika kituo cha Lower Manhattan.

Vyombo vya habari nchini Marekani vimenukuu taarifa za polisi kuwa kijana huyo aliamua kuendesha gari hilo katika njia ya waendesha baisikeli iliyoko karibu na Mto Hudson eneo la Lower Manhattan ya chini ,kabla ya kupigwa risasi na maafisa wa polisi ili kuzuia shambulio alilolipanga.

Raila Odinga: ''Hatutambui uchaguzi wa Uhuru Kenyatta''

Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila OdingaKiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga

Kiongozi wa muungano wa upinzani nchini Kenya Nasa Raila Odinga ameapa kuendelea kufanya maandamano dhidi ya uchaguzi wa Uhuru Kenyatta akisisitiza kuwa upinzani haumtambui.

Odinga anasema kuwa Nasa haitambui uchaguzi huo kwa kuwa mwenyekiti wa IEBC Wafula Chebukati pamoja na kamishna aliyejiuzulu Roselyn Akombe walithibitisha kwa umma kuwa tume hiyo haiwezi kusimamia uchaguzi ulio huru kutokana na misimamo ya kimapendeleo ya baadhi ya makamishna katika tume hiyo.

Odinga ambaye alikuwa akitoa mwelekeo wa upinzani kwa vyombo vya habari katika jumba la OKoa Kenya jijini Nairobi amesema kuwa ana ushahidi wa kutosha kwamba kulikuwa na uingiliaji na uongezaji wa kura katika ngome za chama tawala cha Jubilee.

Anasema kwamba iwapo uchaguzi huo utaruhusiwa na kutambulika utawavunja moyo Wakenya wengi na hivyobasi kuwafanya kutoshiriki katika uchaguzi mwengine wowote.

Mr Odinga pia amesema kuwa hawezi kuwaruhusu watu wawili wanaojigamba kuwa na uwezo kuharibu uhuru na demokrasia ilipatikana.

Amesema kuwa iwapo uchaguzi wa Uhuru utaruhusiwa kuna uwezekano kwamba ataingilia katiba na kuongeza muhula wa kuongoza.

''Tutaendelea kufanya maandamno kila mara'', alisema Raila Odinga.

Rais Uhuru Kenyatta baada ya kutangazwa mshindiRais Uhuru Kenyatta baada ya kutangazwa mshindi

Bwana Odinga alisusia uchaguzi wa marudio wa urais wiki iliopita kwa sababu anasema kuwa hakuna mabadiliko yaliofanyiwa tume ya uchaguzi ya IEBC baada ya mahakama ya juu kupata makosa na ukiukaji mkubwa wa katiba.

Watu waliojitokeza kupiga kura ni chini ya asilimia 39.

Ametangaza kuwa atazindua bunge la wananchi ambalo litashirikisha jopo litakalochunguza kufeli kwa tume za uchaguzi.

Tuesday 31 October 2017

Nape Akana Taarifa Iliyozagaa Mitandaoni



Mbunge wa Mtama Nape Nnauye.

Baada ya Mbunge Lazaro Nyalandu kujiuzulu na kuhamia chama cha Chadema,Nape amekana taarifa iliyoenea mitandaoni kuwaatazungumza na  Waandishi wa Habari leo.

Kupitia ukurasa wake wa Mitandao ya kijamii Nape amesema hatakuwa na mkutano wowote na vyombo vya habari na kusema
kuwa watu wanatunga hizo taarifa.

“Acheni kupiga ramli juu ya kesho yangu!! Kisa mnatafuta vyeo na hamuwezi kutumia akili kufikiri! Sina ‘press conference’
kesho” aliandika Nape Nnauye.

Zitto Kabwe Akamatwa Na Polisi Dar


Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe.


Hatimaye, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe, amekamatwa na Jeshi la Polisi asubuhi hii akiwa nyumbani kwake jijini Dar es salaam na amepelekwa kituo cha Polisi Chang’ombe.

Hayo yameibanishwa na Afisa habari wa Chama hicho Abdallah Khamis ambapo amesema sababu za kukamatwa kwake zinawezekana kuwa ni kutokana na hotuba yake aliyoitoa juzi Oktoba 29, 2017 katika kata ya Kijichi, Mbagala Jijini Dar es salaamkatika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa mdogo wa madiwani kwenye kata 43 nchini.

Hivi karibuni Zitto kabwe amekua akikosoa serikali kuhusiana na hali ya uchumi wa nchi kukua suala ambalo Zitto amesema
haliendani na uhalisia wa maisha ya wananchi

Kenyatta atangazwa mshindi wa urais Kenya akiwa na kura 7.5m

 Uhuru KenyattaRaisi Uhuru Kenyata

Rais Uhuru Kenyatta ametangazwa mshindi wa urais wa marudio nchini Kenya akiwa na kura 7,483,895 sawa na 98%.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi IEBC Wafula Chebukati amesema kiongozi wa upinzani Raila odinga aliyesusia uchaguzi huo alipata kura 73,228 sawa na asilimia 0.96.

Bw Chebukati amesema jumla ya wapiga kura 7,616,217 kati ya jumla ya wapiga kura 19.6 milioni ambao wamejiandikisha kuwa wapiga kura nchini humo walishiriki uchaguzi huo wa Alhamisi wiki iliyopita.

Hiyo ni asilimia 38.84.

Rais Kenyatta, akihutubu baada ya kutangazwa mshindi, amewashukuru waliompigia kura.

Amesema uchaguzi uliomalizika ni ishara ya uthabiti wa demokrasia na uthabiti wa taasisi za Kenya pamoja na Wakenya wenyewe.

"Agosti 8, na sitachoka, Wakenya walirauka kupiga kura. Na siku hiyo walinichagua bila shaka. Ushindi wangu ulipopingwa Mahakama ya Juu, kwenye hukumu, mahakama haikupinga ushindi wangu wa 54%. Takwimu hazikupingwa. Kilichokosolewa ni utaratibu uliopelekea ushindi wangu," amesema.

Bw Odinga alikuwa ametarajiwa kutangaza mwelekeo kwa wafuasi wake baada ya tangazo la matokeo kufanywa na Bw Chebukati.

Taarifa zinasema ameamua kufanya hivyo hapo kesho.

Matokeo kamili ya wagombea wote kama yalivyotangazwa na Bw Chebukati

MgombeaChamaKuraAsilimia
Uhuru KenyattaJubilee7,483,89598.28
Raila Odinga (Alisusia)ODM73,2280.96
Mohamed Abduba DidaARK14,1070.19
Japheth Kavinga KaluyuMgombea wa kujitegemea8,2610.11
Michael Wainaina MwauraMgombea wa kujitegemea6,0070.08
Joseph Nthiga NyagahMgombea wa kujitegemea5,5540.07
John Ekuru AukotThirdway Alliance21,3330.28
Cyrus JirongoUDP3,8320.05

Bw Chebukati amesema anaamini uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.

Mwenyekiti huyo amesema mambo aliyosema yalihitajika kufanyika kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki yalitimizwa.

Amesema walitaka kuhakikisha kila kitu kilikuwa sawa.

"Hata tulibadilisha tarehe kutoka 17 hadi 26 Oktoba kuhakikisha tuna muda wa kutosha," amesema.

Kadhalika, amesema alikuwa na kundi la kusimamia mradi wa uchaguzi wa urais kuondoa majukumu kutoka kwa makamishna ambao walituhumiwa na baadhi ya wadau.

"Naweza kusema kwa uhakika, kwamba 26 Oktoba kabla ya uchaguzi kuanza, nilikuwa nimeridhika kwamba tulikuwa tumefanya kila kitu kuhakikisha kila Mkenya angetekeleza haki yake kikatiba," amesema.

"Na haki hii mtu anafaa kuitekeleza bila kutishiwa au kuzuiwa."

Bw Chebukati anasema alishangaa kwamba watu waliotafuta wa kushambulia walimwendea yeye.

Hata hivyo, anasema ndani ya tume nao walimwogopa.

"Hatutaweza kufurahisa kila mtu. Nimedumisha na kuheshimu sheria, kama mwanasheria ziwezi kuvunja sheria niliyojitolea kuilinda," amesema.

Matokeo yalivyokuwa uchaguzi wa tarehe 8 Agosti ambao ulifutwa na Mahakama ya Juu

MgombeaChamaKuraAsilimia
Uhuru KenyattaJubilee8,203,29054.27
Raila OdingaODM6,762,22444.74
Mohamed Abduba DidaARK38,0930.25
Japheth Kavinga KaluyuMgombea wa kujitegemea16,4820.08
Michael Wainaina MwauraMgombea wa kujitegemea13,2570.09
Joseph Nthiga NyagahMgombea wa kujitegemea42,2590.28
John Ekuru AukotThirdway Alliance27,3110.18
Cyrus JirongoUDP11,7050.08

Monday 30 October 2017

Mbunge wa CCM Lazaro Nyalandu ajiuzulu Tanzania

Bw Nyalandu

Mbunge wa chama tawala nchini Tanzania CCM Lazaro Nyalandu amejiuzulu wadhifa wake, na kusema kwamba anataka kuhamia chama cha upinzani Chadema.

Bw Nyalandu, Aliyekuwa Waziri wa Mali Asili na Utalii wakati wa serikali ya awamu ya Tano nchini Tanzania amesema kupitia taarifa kwamba amejuzulu nyadhifa zake zote ndani ya chama cha mapinduzi CCM ikiwemo ubunge.

Nyalandu ambaye kabla ya maamuzi hayo ya kujiuzulu alikuwa Mbunge wa Singida Kaskazini amesema amechukua uamuzi huo kutokana na kutokuridhishwa na mwendo wa siasa nchini Tanzania, ukiukwaji wa haki za kibinaadamu, ongezeko la vitendo vya kidhalimu dhidi ya raia na kutokuwepo kwa mipaka baina ya mihimili ya dola - Serikali, Bunge na Mahakama.

Katika taarifa yake ya kujiuzulu aliyoiweka katika ukurasa wake wa Facebook, Nyalandu amesisitiza umuhimu wa nchi hiyo kupata katiba mpya.

"Naamini kwamba bila Tanzania kupata Katiba Mpya Sasa, hakuna namna yeyote ya kuifanya mihimili ya dola isiingiliane na kuwepo kwa ukomo wa wazi na kujitegemea kwa dhahiri kwa mihimili ya Serikali," amesema.

"Nimemua kujiuzulu Kiti cha Ubunge, Jimbo la Singida Kaskazini kuruhusu kufanyika kwa uchaguzi mwingine ili wananchi wapate fursa ya kuchagua itikadi wanayoona inawafaa kwa majira na nyakati hizi zenye changamoto lukuki nchini Tanzania.

"Ni imani yangu, kamwe hayatakuwa ya bure maneno haya, wala uamuzi huu niufanyao mbele ya Watanzania leo."

Nyalandu anaingia katika orodha ya mkururu wa viongozi wa juu wa CCM waliokihama chama hicho na kuhamia chama kikuu cha upinzani nchini humo Chadema tangu mwaka 2015.

clouds stream