Tuesday 31 March 2015

Mwendesha mashtaka kesi ya ugaidi auawa kwa risasi

Mwendesha mashtaka kesi ya ugaidi auawa kwa risasi


kageziss-600x360
Mkurugenzi Msaidizi wa Mashtaka ambaye alikuwa akiongoza upande wa mashtaka katika kesi ya tukio la ugaidi la Jijini Kampala, lililotokea Julai 2010 nchini Uganda ameuawa jana jioni kwa kupigwa risasi.
Kwa  mujibu wa polisi nchini humo wamesema Joan Kagezi, aliuawa saa mbili usiku na watu wenye silaha waliokuwa wakiendesha pikipiki katika eneo la Kiwatule, lililopo nje kidogo ya Jiji la Kampala, wakati akirejea nyumbani.
Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Upelelezi, Grace Akullo, amethibitisha tukio hilo ambapo amesema mwili wa Kagezi, umehifadhiwa kwenye hospitali ya Mulago, na uchunguzi wa mauaji yake unaendelea.

Monday 30 March 2015

HOUSE FOR SALE


HOUSE FOR SALE: House for sle for sale located at Mbezi kwa msuguri, it has 3 bed rooms one of them is a master bed room, sitting room, it has 400 sqm. PRICE is TSH.30 mil.

A HOUSE FOR SALE



HOUSE FOR SALE: A house for sale, located at Mbezi beach Kilongowima street, it has a huge space for car parking and other activities, PRICE is TSH. 600 mil ( negotiable ).

HOUSE FOR SALE


 HOUSE FOR SALE: A house for sale is located at Mwandege, it has 3 bed rooms, sitting room, kitchen, dinning room and enough space  ( 660 sqm ). PRICE is TSH. 15 mil.

Thursday 26 March 2015

Brazil yalipa kisasi, yaichapa Ufaransa 3-1

Brazil yalipa kisasi, yaichapa Ufaransa 3-1


Magoli ya vipindi tofauti ya wachezaji Oscar(40′), Neymar 57′ na Luiz Gustavo 69′ yaliitocha Brazil kulipiza kisasi cha kufungwa na Ufaransa kwenye kombe la Dunia 1998.


Ufaransa ndio walikuwa wa kwanza kupata bao kupitia kwa beki kisiki wa Real Madrid Raphael Varane kwenye dakika ya 21 kwa njia ya kichwa baada ya kutumia kona ya upande wa kushoto iliyopigwa na  Mathieu Valbuena.


Brazil  walitawala muda wote wa mchezo hasa kwa wachezaji wake machachari Neymar na Oscar huku kwa upande wa Ufaransa mshambuliaji wake muhimu Karim Benzema alibana vilivyo, Ushindi wa Brazil unamfanya Dunga kushinda kwa asilimia 100 tangu achukue kikosi hicho mwezi Julai. Mpaka mwisho wa mchezo Brazil wanatoka kifua mbele kwa mabao 3-1.

Rais Kikwete ateua wabunge wawili wapya

Rais Kikwete ateua wabunge wawili wapya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, amewateua wabunge wawili wapya wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Walioteuliwa ni Dkt. Grace Khwaya Puja na Bwana Innocent Sebba ambapo Rais amefanya uteuzi huu kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 66 (I) (e) ambapo amepewa mamlaka ya kuteua wabunge wasiozidi 10.
Uteuzi huu umekamilisha idadi ya wabunge ambao Mheshimiwa Rais amepewa kwa mujibu wa mamlaka aliyonayo Kikatiba ambao waliokwishateuliwa ni Mhe. Profesa Makame Mnyaa Mbarawa, Mhe. Profesa Sospeter Muhongo, Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro, Mhe. Janet Zebedayo Mbene, Mhe. Saada Salum Mkuya, Mhe. Zakhia Hamdani Meghji, Mhe. Shamsi Vuai Nahodha, na Mhe. James Mbatia.

Marekani yabaini mpango wa Al shabaab kuishambulia Uganda

Marekani yabaini mpango wa Al shabaab kuishambulia Uganda

Nchi ya Marekani  kupitia  ubalozi  wa  Marekani nchini Uganda, umesema una taarifa za uwezekano wa kutokea  shambulio la kigaidi nchini humo.
Aidha, taarifa ya ubalozi huo imebainisha kwamba shambulio hilo linaweza kutekelezwa wakati wowote, katika maeneo ambayo raia wa mataifa ya Magharibi na Marekani hukutana.
Katika kipindi kilichopita, kundi la Al-Shaabab lenye makao yake Nchini Somalia, limetekeleza mashambulio Nchini Uganda.
Kwa upande mwingine  nhi ya  Marekani  imetoa tahadhari kwa raia wake wote  waliopo nchini Uganda.

UVCCM yamuonya Nape ‘kumponda’ Lowassa

UVCCM yamuonya Nape ‘kumponda’ Lowassa

Umoja wa Vijana (UVCCM) mkoani Arusha, umemuonya katibu wa itikadi na uenezi Nape Nnauye kuchunga kauli zake kufuatia kauli aliyoitoa dhidi ya Edward lowassa.
Akizungumza na waandishi wa habari mkoani Arusha Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana (UVCCM) MKoani Arusha, Robson Meitinyiki amesema Nape  anapaswa kuelewa chama hicho kilibomoka na  kuwa ni chama cha watu wote na kwa sasa chama kimeanza kuimarika kupitia jitihada za Katibu Mkuu, Abdurahamani Kinana na yeye anaanza kujinyanyua na kutaka kukibomoa.
Ameongeza kuwa  Nape aelewe nyuma ya Lowassa wapo wengi na Arusha wanajipanga kwenda kumshawishi achukue fomu na yeye hapaswi kutoa maneno ya kejeli, kwani kuna kanuni na taratibu za vyama vya kumsimamisha mtu kuwa mgombea, kama ana mgombea wake amtangaze japo lazima apitishwe na chama,siyo mtu mmoja.
Kwa upande wake  Katibu Mwenezi Mkoa wa Arusha, Isack  Joseph, amesema Nape afike mahali achunge kauli zake dhidi ya Lowassa, kwani Lowasa ni mtu mwenye heshima katika nchi hii na alikuwa Waziri Mkuu na kuiletea taifa heshima kubwa.
Kwa upande mwoingine Robson  amesema kama Edward Lowassa anafanya maigizo, ili apendwe na watu, basi wanamshauri mgombea wa Nape afanye maigizo hayo, ili apendwe na watu kwa kufuatwa nyumbani kwake.

Watu 2 Wakamatwa na Mifupa ya Albino Kagera

Watu 2 Wakamatwa na Mifupa ya Albino Kagera


Jeshi la Polisi mkoani Kagera  linawashikilia  watu 2  kwa kosa la kukutwa na viungo mbalimbali vya mwili ikiwemo mifupa mitatu ya mtu mwenye ulemavu wa ngozi (albino).
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Kagera Henry Mwaibambe alisema kuwa tukio hilo limetokea juzi katika kijiji cha Kyota kata ya Kimwani wilayani Muleba mkoani Kagera baada ya jeshi hilo kuweka mtego kwa watuhumiwa hao ambao walikuwa wanatafuta wateja wa viungo hivyo.
Watuhumiwa waliokamatwa  ni James Rutozi (66) mkazi wa Kimwani ambaye ndiye aliyekuwa anahifadhi viungo hivyo na Emanueli Kaloli (50) ambaye pia ni mkazi wa Kimwani aliyekuwa anatafuta mteja wa viungo hivyo.
Jinsi  watuhumiwa hao walivyokamatwa,
Alisema mara baada ya kupata taarifa kuwa kuna watu wanauza viungo hivyo kwa Sh milioni 3 waliweka pesa za mitego na kujifanya wao ni wateja na ndipo walipowakamata watuhumiwa hao wawili ambao walikutwa na mfupa mmoja na walipowabana zaidi ndipo walitoa mifupa miwili.
Mnamo mwaka 2006 katika kijiji cha Rushwa kata ya Mushabago wilayani Muleba, Zeulia Jestus akiwa na miaka 24 mwenye ulemavu wa ngozi (albino) alifariki dunia muda mfupi baada ya kujifungua na ndipo watuhumiwa hao walifukua kaburi hilo mwaka 2008 kwa maelekezo ya mganga wa jadi.
Ameongeza kuwa  walipotaka kujiridhisha jeshi hilo liliomba kibali mahakamani ili kufukua kaburi hilo mnamo Machi 23, mwaka huu lilipofukuliwa liligundulika kuwa viungo hivyo vimetolewa katika mwili wa marehemu huyo.
Kwa upande mwingine jeshi la Polisi linamtafuta mganga wa jadi aitwaye Mutalemwa Revocatus ambaye ametoroka kabla kukamatwa. Mganga huyo   ndiye  anayedaiwa kuwashawishi wafukue hilo kaburi na kuwapa dawa ya kinga ili wasidhurike wakati wanafukua.

Urais 2015: CCM yamuonya Lowassa

Urais 2015: CCM yamuonya Lowassa

Chama cha Mapinduzi CCM kimeibuka na kusema kuwa vitendo vinavyofanywa na Mbunge wa Monduli Edward Lowassa  ni ukiukwaji mkubwa wa kanuni za chama  hicho.
Akizungumzia suala hilo Katibu wa Itikadi na uenezi CCM Nape Nnauye amesema kwamba  vitendo anavyo vifanya Lowassa ni kuvunja kanuni pamoja na kiburi, matendo ya wazi ya kampeni bila shaka. Kupitia matendo hayo yanaweza kumpotezea sifa ya kuwa mgombea katika chama hicho.
Ameongeza kuwa Lowassa ni miongoni mwa waliopewa adhabu na CCM mwaka jana kwa kuanza kampeni kabla ya muda huku akisisitiza bado yupo katika uangalizi.
Katika hatua nyingine Lowassa amekuwa anadaiwa akitumia makundi mbalimbali kufanya kampeni kupitia vikundi mbalimbali, vikundi hivyo ni wajasiriamali jimboni Monduli mkoani Arusha, mashehe 50 kutoka wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani pamoja pamoja   na wachungaji.
Makundi hayo yaalifunga safari hadi nyumbani kwa Lowassa Dodoma kumshawishi achukue fomu ya kugombea urais katika uchaguzi mkuu wa urais utakaofanyika oktoba 2015.

Tuesday 24 March 2015

Ugiriki yakumbwa na mzigo wa Madeni

Ugiriki yakumbwa na mzigo wa Madeni



Viongozi wa Ujerumani na Ugiriki wakutana ujerumani kuinusuru ugiriki dhidi ya mzigo wa madeni, huku waziri mkuu mteule wa Ugiriki akitoa onyo juu ya mahitaji muhimu ya msaada wa haraka wa kifedha.
Aidha,  waziri Alexis Tsipras wa Ugiriki amemweleza kansela wa Ujerumani Angela Merkel kwamba bila msaada mpya wa kifedha kutoka umoja wa ulaya, serikali yake haitaweza kuwa na uwezo wa kulipa madeni yake.
Waziri Tsipras ambaye anafanya ziara yake ya kwanza mjini Berlin alipokelewa na mwenyeji wake kansela Angela Merkel kwa gwaride la kijeshi la katika himaye ya chansela huyo.
Viongozi hao Waziri Mkuu wa Ugiriki na chansela wa Ujerumani wameelezea uhumimu wa nchi zote mbili kufanya kazi pamoja kufuatia mazungumzo ya Berlin kuhusu namna ya kukabiliana na madeni ya Ugiriki.
Kwa upande wake waziri mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras , amesema ni muhimu zaidi kwa Athens na Berlin kufanya mazungumzo ya pamoja kuliko kila mmoja kumzungumzia mwenzake.

Urais 2015: Obama ataka uchaguzi huru Nigeria

Urais 2015: Obama ataka uchaguzi huru Nigeria


Wananchi  nchini Nigeria  wanatarajiwa kupiga kura jumamosi wiki hii baada uchaguzi huo kuhairishwa mwezi uliopita kutokana na mashambulio ya kundi la Boko Haram.
Akizungumzia uchaguzi huo Rais Obama amesema kwamba Nigeria inapaswa kufanya uchaguzi ulio huru na wa haki.
” Wanigeria  wote wanapaswa kupiga kura zao bila ya vitisho ama wasi wasi . Hivyo natoa wito kwa viongozi wote pamoja na wagombea kuzungumza na wapiga kura wao kwamba vurugu hazina nafasi katika uchaguzi wa kidemokrasia,na hawapaswi kuchochea, wasaidie au kujihusisha na vurugu zozote kabla ama baada ya uchaguzi na wakati wa kuhesabu kura.” Alisema Obama
Nina waomba wanaigeria wote kueleza hisia zenu kwa amani na kuwapuuza wote wanaotoao wito wa kufanya vurugu .
Joto la uchaguzi linazidi kupamba moto nchini Nigeria. Mvutano mkali upo kati ya rais Goodluck Jonathan wa chama tawala cha PDP na mgombea wa upinzani Jenerali Muhhamadu Buhari wa APC.

Monday 23 March 2015

HOUSE FOR SALE
















HOUSE FOR SALE: A house located at Tegeta, it is has two floors with six bed rooms, sitting room,dinning room, kitchen,store and enough car parking.Its PRICE is TSH. 600 mil.

Monday 16 March 2015

Yanga noma, yawachakaza wazimbabwe bila huruma

Yanga noma, yawachakaza wazimbabwe bila huruma


Baada ya dakika 90 kumalizika televisheni ya uwanja wa Taifa ilikuwa ikisomeka Yanga 5-1 FC Platinum
Baada ya dakika 90 kumalizika za mchezo wa kombe la shirikisho barani Afrika, televisheni ya uwanja wa Taifa ilikuwa ikisomeka Yanga 5-1 FC Platinum
Yanga wameendeleza ubabe kwa kuutumia vyema uwanja wa nyumbani kwa kuitandika FC Platinum kwa goli 5-1 kwenye mchezo wa raundi ya kwanza ya kombe la shirikisho barani Afrika mchezo uliopigwa leo jioni kwenye uwanja wa Taifa jijini Da es Salaam.
Salum Telela alianza kuifungia Yanga goli la kwanza dakika ya 26 kabla ya Haruna Niyonzima kuongeza bao la pili dakika ya 40 baada ya Amis Tambwe kutandika shuti kali lililotemwa na kipa wa FC Platinum na kumkuta Mnyaruanda huyo aliyeukwamisha mpira wavuni, lakini dakika ya 45 Walter Musona akaipatia FC Platinum goli la kufutia machozi kwa mpira wa adhabu ndogo uliomshinda golikipa wa Yanga Ally Mustafa ‘Bathez’.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi kubwa huku Yanga wakiliandama lango la wapinzani wao kwa muda mwingi kitu kilicho wachanganya FC Platinum. Dakika ya 46 Amis Tambwe akaifungia Yanga goli la tatu akiunganisha krosi safi iliyochongwa na Mrisho Ngassa, goli hilo liliwaamsha Yanga na kuona wanaweza kupata magoli mengi zaidi.
Mrisho Ngassa aliyekuwa msumbufu na mwiba mkali kwenye safu ya ulinzi ya wazimbabwe alifunga goli la nne mnamo dakika ya 52, lakini hakuishia hapo kwani dakika ya 90 alifunga goli lake la pili na la tano kwa upande wa Yanga akimalizia pasi ya Mliberia Kpah Sherman.
Mchezo wa marudio utachezwa jijini Harare, Zimbabwe majuma mawili yajayo, Yanga wanatakiwa kutoridhika na ushindi wao na kubweteka kwani lolote laweza tokea kwenye soka. Mfano mzuri ni wao wenyewe walivyokumbana na upinzani mkali kwenye mechi yao ya marudiano kwenye hatua ya awali dhii ya BDF XI ya Botswana.
Lakini pia Azam wakiwa Sudan walishindwa kutamba na kuzuia kufungwa goli 3-0 mbele ya Al- Merreikh na kutupwa nje ya mashindano, wanachotakiwa ni kuwa na nidhamu ya mchezo na kujiandaa kushinda mechi yao ya pili ili kusonga mbele.

Mashali aendeleza ubabe, amsulubu Dullah Mbabe

Mashali aendeleza ubabe, amsulubu Dullah Mbabe


Thomas Mashali (kulia) akimuadabisha Dullah Mbabe jana usiku, Mashali alishinda kwa pointi za majaji wawili kwa mmoja
Thomas Mashali (kulia) akimuadabisha Dullah Mbabe jana usiku kweye pambano lao la raundi 10, Mashali alishinda kwa pointi za majaji wawili kwa mmoja
Bondia wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali ‘Simba asiyefugika’ jana usiku alimtwanga Abdallah Paazi ‘Dulla Mbabe’ kwa ushindi wa pointi kwenye pambano la raundi 10 ambalo halikuwa la ubingwa lililopigwa kwenye viwanja vya ndani vya Taifa.
Pambano hilo lililokuwa kali na lenye kuvutia, lilianza kwa kasi huku Mashali akianza vyema pambano hilo kwa kumsukumia makonde mazito mpinzani wake kwenye raundi za mapema. Mbabe nae hakuwa nyuma kwani alikuwa akijibu mapigo na kulifanya pambano hilo kuwa la kuvutia zaidi.
Mashali ambaye ni mzoefu kwenye mchezo wa masumbwi, alionekana kuchachamaa kuanzia raundi ya saba na kubadilisha kasi ya mchezo kitu ambacho kilimchanganya Mbabe aliyeonekana kupungua kasi kadri muda ulivyokuwa unayoyoma.
Wakali hao walitambiana kabla ya pambano lao hali iliyopelekea kutaka kuzichapa ‘kavukavu’ siku ya Jumamosi walipokutana kwenye zoezi la kupima uzito kabla ya pambano lao la jana.
Kwenye mapambano mengine ya utangulizi, Japhet Kaseba alikubali kichapo kutoka kwa bondia Said Mbelwa, mpambano uliokuwa wa raundi nane ambapo Mbelwa alishinda kwa pointi za majaji wa wili kwa mmoja.
Pambano jingine la raundi 10 liliwakutanisha Mada Maugo dhidi ya Karama Nyilawila ambapo Maugo aliibuka mshindi kwenye pambano hilo kwa pointi za majaji wawili kwa mmoja na kukata ngebe za nani mkali wa kutupa makonde kati yao.
Pambno jingine la masumbwi la kimataifa litapigwa kati ya Mohamed Matumla ‘Matumla Jr’ dhidi ya Wang Xin Hua kutoka China, pambano hilo litachezwa Machi 27 kwenye ukumbi wa Diamond Jubelee jijini Dar es Salaam.
Pambano hilo litakuwa la uzito wa Super Bantam kuwania nafasi ya kwenda kugombea ubingwa wa taji la dunia la WBF kwenye mapambano ya utangulizi Mei 2 mwaka huu huko Las Vegas Marekani siku ambayo kutakuwa na pambano la Floyd Mayweather dhidi ya Manny Pacquiao.

Moto umezuka hosteli za Mabibo chuo kikuu Dar es salaam (UDSM) asubuhi hii

Moto umezuka hosteli za Mabibo chuo kikuu Dar es salaam (UDSM) asubuhi hii



Taarifa zilizotufikia hivi Punde, kumezuka Moto kwenye Hostel  za Mabibo  za  Chuo  Kikuu Dar es salaam (UDSM). Moto huo bado unaendelea kuwaka  kwenye jengo la Block B.
Chanzo cha moto huo bado hakijafahamika, tutakujulisha zaidi kuhusiana na tukio hili.

Rais wa Zambia afanyiwa upasuaji Afrika Kusini

Rais wa Zambia afanyiwa upasuaji Afrika Kusini


Rais wa Zambia, Edgar Lungu, ameruhusiwa kutoka hospitali ya Afrika Kusini baada ya kufanyiwa upasuaji.
Rais huyo aliyechaguliwa karibuni, ana ugonjwa unaomrejea mara kwa mara, na unao athiri koo yake.
Rais huyo   alilazwa hospitali mjini Pretoria Jumaane mara baada ya  kuzimia katika sherehe za siku ya kimataifa ya wananwake mjini Lusaka.
Kwa upande mwingine Mwezi wa kwanza  alishinda uchaguzi wa rais, na kuchukua nafasi ya Hayati Rais Michael Sata, aliyefariki  dunia oktoba mwaka jana.

Urais 2015: Machinga wajichanga kumchukulia fomu Lowassa



Urais 2015: Machinga wajichanga kumchukulia fomu Lowassa




Wafanya biashara ndogondogo maarufu kama Machinga wamechangisha fedha kiasi cha shilingi Milioni moja na kumkabidhi mbunge wa Monduli Bw. Edward Lowassa ilia aweze kuchukulia fomu ya kugombea urais nchini Tanzania katika uchaguzi mkuu unatakaofanyika mwezi oktoba mwaka huu.
Aidha kiasi hicho cha fedha kimekabidhiwa na wawakilishi wa umoja wa wamachinga nchini Tanzania hivi karibuni nyumbani kwake Ngarash Monduli. iBaada ya kumkabidhi kiasi hicho cha fedha walimkabidhi pia Ngao na Mkuki ambayo wamesema atatumia katika safari yake ya matumaini.
Uchaguzi mkuu wa rais pamoja na wabunge unatarajia  kufanyika mwezi oktoba mwaka 2015 huku wanasiasa  mbalimbali wakitangaza nia ya kutaka kuingia  katika kinyang’anyiro cha hicho.

Mapokezi ya Zitto Kabwe ni Balaa

Mapokezi ya Zitto Kabwe ni Balaa


Wananchi wamempokea kwa shangwe mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe mara baada ya kuwasili  mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi katika jimbo lake.
Maelfu ya wananchi wameminimika barabarani huku kelele za shangwe zikisikika ambazo zinataja jina lake.
Katika hatua nyingine, Chama cha Demkorasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza hivi karibuni kumvua uanachama  Zitto kwa madai ya kufungua kesi inayopinga kujadiliwa katika chama chake hata hivyo alishindwa na kuamriwa  alipe gharama za kuendeshea kesi hiyo katika mahakama Kuu ya Tanzania.

Saturday 14 March 2015

A PLOT FOR SALE








PLOT FOR SALE: A plot with a house located at Kiluvya kwa Komba near RC church, SIZE is 2000 sqm,PRICE is TSH. 40 mil ( negotiable ).

HOUSES FOR SALE




HOUSE FOR SALE: A house for sale located at located at Bunju B, it has 4 bed rooms 2 of them are  masters, kitchen, siting room and dinning room (semi finished ).It take 5 minutes from the main road ( Bagamoyo road) half km, it has a tittle deed and its PRICE is TSH.80 mil ( negotiable ).








A HOUSE FOR SALE: A house for sale located at Kiluvya kwa Komba secondary school,it has 4 bed room one being a master, kitchen, sitting room and dinning room ( semi finished ). Its PRICE is TSH. 40 mil ( negotiable ).

clouds stream