Thursday 26 May 2016

Makandarasi 4,572 Wafutiwa Leseni

Makandarasi 4,572 Wafutiwa Leseni

May 27, 2016

V 1

Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Rhoben Nkhori.

Bodi ya Usajili wa Makandarasi imefuta usajili wa jumla ya makandarasi 4,572 kwa kushindwa kutimiza matakwa ya Sheria ya Usajili wa Makandarasi ya mwaka 1997.

Kaimu Msajili wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi (CRB), Rhoben Nkhori amebainisha hayo wakati wa Mkutano wa Mashauriano wa CRB uliofanyika jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Nkhori amesema kuwa katika jukumu la kuratibu mwenendo wa kazi za makandarasi, Bodi ilikagua miradi 2735. Katika miradi hiyo iliyokaguliwa, miradi 1873 sawa na asilimia 68.5 haikuwa na kasoro.

Ameongeza kuwa miradi mingine ilikuwa na kasoro za kutofanywa na makandarasi waliosajiliwa, kutozingatia usalama wa wafanyakazi, kutokuwa na bango wala uzio na miradi kutosajiliwa. Kwa mujibu wa Bw. Nkhori miradi yote iliyopatikana na upungufu wahusika walichukuliwa hatua mbali mbali kwa mujibu wa sheria.

“Kwa mwaka jana, Bodi ilisajili miradi 3,172 yenye thamani ya shilingi trilioni4.23. Katika miradi hii asilimia 44.4 ilifanywa na Makandarasi wazawa na asilimia 55.6 ilifanywa na makandarasi wa kigeni,” amesema.

Licha ya mafanikio hayo CRD ilikumbana changamoto kadhaa ikiwemo kuwasilisha nyaraka za kugushi wakati wa usajili hususani kadi za magari na mitambo, vyeti vya wataalam, kutumia majina ya makandarasi kwa udanganyifu kwa kuuza vibao, waendelezaji kutotoa taarifa sahihi za umiliki kwa Bodi na baadhi ya makandarasi kushindwa kuwalipa wafanyakazi na vifaa vya ujenzi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa Makandarasi, Bi Consolata Ngimbwa amemwomba Mhe. Rais John Pombe Magufuli kuwapa kipaumbele Makandarasi wa humu nchini ili kuwawezesha kiuchumi. “Mhe. Rais tunaomba utupe kipaumbele kwani sisi tukipata hiyo miradi tutawekeza hapa nchi na kuongeza soko la ajira,”alisema Bi Ngimbwa.

Rais Magufuli amesema serikali yake itawapa kipaumbele makandarasi wazawa lakini akawataka wajipange na kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia maadili ikiwemo kujiepusha na vitendo vya rushwa.

Mrema ‘Amvaa’ Maalim Seif

Mrema ‘Amvaa’ Maalim Seif

 

V 3Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party (TLP), Augustino Mrema.

Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Tanzania Labour Party (TLP), Augustino Mrema,  amelaani hatua ya Katibu Mkuu wa CUF Maalim Seif kutangaza kumwondoa Rais wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein  madarakani kabla ya 2020 huku akiwataka wazanzibar kutoyumbishwa na kauli za mwanasiasa huyo.

Amesema  amani ya Zanzibar ni muhimu kuliko maslahi binafsi hivyo ni vyema kuzitafakari kauli ambazo zinaweza kuleta machafuko na kudai kuwa hakuna mtu aliye juu  ya sheria hivyo kuwepo kwa watu wanaochochea  vurugu  ni kama waahini na kwamba ni vyema hatua zichukuliwe dhidi yao katika kuhakikisha  wananchi wanakuwa salama.

Mrema amesema kwamba amani ya Zanzibar ikiharibika hata bara haiwezi kuwa salama hivyo ni vyema kauli za kuvuruga amani zizingatiwe ili kulinda maslahi ya wananchi wa pande zote mbili.

“Zanzibar ina historia ya kuuawa watu mwaka 2001,kutokana na vurugu za kisiasa hivyo lazma kwa sasa jambo lolote la kiuchochezi liangaliwe kwa macho mawili dhidi ya watu wanaotaka kuvuruga amani katika mazingira hayo,” ameonya.

Amesisitiza  kuwa hakuna chama cha siasa ambacho kinajengwa kwa kususia uchaguzi bali kufanya hivyo ni kuwanyima wapiga kura haki pia ni hatari na kunaweza kusababisha chama kusambaratika kama kulivyotokea kwa baadhi ya vyama mfano, UPC cha Uganda na vinginevyo.

Pamoja na hayo mrema amefafanua kwamba mahakama ya ICC haingalii tu viongozi wa serikali bali hata viongozi wa kisiasa ambao wamesababisha mauaji kutokana na kauli wanazozitoa na kuwataka wahisani kutoingilia mambo ya ndani ya nchi kwani kusitisha misaada kwa hoja ya kufutwa uchaguzi wa Zanzibar na sheria ya mitandao ni kuingilia uhuru wa watanzania.

Vifaranga 5,000 Vyakamatwa Uwanja Wa Ndege


Vifaranga 5,000 Vyakamatwa Uwanja Wa Ndege


Tarehe May 26, 2016airport
Serikali inashikilia jumla ya vifaranga 5,000 vya kuku baada ya kuvikamata vikiingizwa nchini kutokea nchini Malawi kwa kutumia vibali visivyo halali.
Akizungumza na wanahabari katika Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere, Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, ,Maria Mashingo amesema kibali kilichotumika kuingiza vifaranga hivyo vyenye thamani ya milioni 20 ni batili kwani kilitolewa mwaka 2014 kwa mfanyabiashara ambaye aliingiza kuku mama ambao huruhusiwa kisheria.
“Hakuna ruhusa ya kuingiza vifaranga kwani huwa na magonjwa ambayo yanaweza kuambukiza kwa kuku wanaozalishwa hapa kwetu!,” alisema Mashingo.
Mashingo aliongeza kuwa, mbali na magonjwa, endapo vifaranga hao wangefanikiwa kupitishwa katika uwanja huo wangeweza kuua soko la wafanyabiashara wa ndani.
Mwaka 2010 serikali ilipiga marufuku kuingizwa kwa vifaranga nchini ili kuiepusha nchi na ugonjwa wa mafua ya ndege ambao umekuwa ukiripotiwa kulipuka katika nchi mbalimbali.

Serikali: Marufuku Kusafirisha Wanyama Hai

Serikali: Marufuku Kusafirisha Wanyama Hai

Tarehe May 26, 20168-1-1
8-1-1
Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe
Serikali imepiga marufuku kusafirisha wanyamahai wote nje ya nchi kwa miaka mitatu kuanzia leo hadi hapo idara ya wanyamapori itakapokuja na utaratibu mpya wa kuwasafirisha.
Hayo yamesemwa bungeni na Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe wakati akifanya majumuisho ya hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya wizara yake kwa mwaka 2016/17.
“Kuanzia sasa  kwa miaka mitatu serikali imepiga marufuku usafirishaji wa wanyamahai wote kwenda nje ya nchi… Hata chawa za Tanzania hataruhusiwa kusafirishwa nje,” alitangaza Waziri Maghembe.
Maghembe alisema wanyama wengi kutoka Tanzania hupelekwa Hong Kong, Thailand, Ulaya Mashariki na kwingineko duniani jambo linalosababisha ukosefu wa mapato kwa serikali kwani wanyama hao huingizia mapato nchi hizo badala ya Tanzania.

Tozo Daraja La Nyerere Kupitiwa Upya

Tozo Daraja La Nyerere Kupitiwa Upya

Tarehe May 26, 2016
746a05242f0e65acccb45c83318ae029
Kufuatia malalamiko ya watumiaji wa daraja la Nyerere lililopo Kigamboni, serikali inatarajia kufanya mapitio ya viwango vya tozo zinazotumika kwa vyombo vya usafiri vinavyopita kwenye daraja hilo.
Akizungumza na gazeti la serikali la kila siku, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (anayeshughulikia Ujenzi), Joseph Nyamhanga, alisema tangu waanze makusanyo, wamepokea ushauri na maoni na kisha watafanya mapitio ya viwango.
“Kwa sasa bado ni mapema sana, hatuna hata mwezi mmoja toka tuanze kupokea tozo, tunaendelea kupokea ushauri na baada ya mwezi mmoja tutakaa na kufanya mapitio tena kuangalia viwango hivyo,” alisema Nyamhanga.
Aidha alisema Wizara pia itaangalia namna ya kuweka mfumo ambao utawanufaisha zaidi watumiaji wa daraja hilo wa mara kwa mara kuwezesha kuwapo utaratibu wa kulipia tiketi za msimu zitakazotoa nafuu.
“Ushauri wangu kwa wananchi wanaotumia daraja hilo ni kwamba wavute subira wakati tunaangalia hali ikoje, lakini waelewe duniani kote barabara za kulipia na hata madaraja yapo, hii ni mfumo ambao upo duniani kote,” alifafanua.

Tuesday 24 May 2016

Magufuli Ateua Mwanasheria, Mshauri Wa Uchumi


Magufuli Ateua Mwanasheria, Mshauri Wa Uchumi


Tarehe May 24, 2016Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bw. Gerson J. Mdemu kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Kabla ya Uteuzi huo, Bw. Gerson J. Mdemu alikuwa Karani wa Baraza la Mawaziri (Cabinet Clerk).
Bw. Mdemu anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Tulia Ackson ambaye amechuguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Profesa Longinus Rutasitara kuwa Mshauri wa Rais, masuala ya uchumi.
Kabla ya uteuzi huo Profesa Longinus Rutasitara alikuwa Mhadhiri wa Uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es salaam.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi  imeeleza kuwa uteuzi huu unaanza mara moja.

Maalim Seif Matatani Na Jeshi La Polisi Zanzibar

Maalim Seif Matatani Na Jeshi La Polisi Zanzibar

Tarehe May 24, 2016Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad.
Jeshi la Polisi Zanzibar linatarajia kumhoji Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad Ijumaa ya wiki hii kuhusu masuala mbalimbali ambayo hata hivyo, hayakuwekwa wazi.
Kamishna wa Polisi Zanzibar, Hamdani Makame amesema  kuwa  wasaidizi wake ndio watafanya mazungumzo na kiongozi huyo siku ya Ijumaa na kwamba wao ndio wanajua watamhoji nini.
Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar, Salum Msangi naye hakuweka wazi badala yake amesema kuna masuala mengi ambayo ofisi yake inahitaji kuyafahamu kutoka kwa Maalim Seif.
Hii ni mara ya kwanza kwa Maalim Seif kuhojiwa na polisi tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu ambao kwa Zanzibar ulirejewa Machi 20, baada ya ule wa Oktoba 25 mwaka jana kufutwa.
Maalim Seif ambaye kabla ya uchaguzi huo alikuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, alipinga kurudiwa kwa uchaguzi huo msimamo ambao pia ulichukuliwa na chama chake.
Kiongozi huyo amekuwa akitoa matamko kadhaa ya kuwashawishi wananchi kupinga utawala wa Serikali iliyopo madarakani.
Akiwahutubia wafuasi wake huko Pemba hivi karibuni, Maalim Seif alisema Serikali ya CCM imeanza kutikisika kutokana na vikwazo vinavyoendelea kuwekwa na wahisani pamoja na hatua ya chama chake CUF kutowatambua viongozi wake pamoja na Serikali.
“CCM wajue wamekalia kuti kavu, siku yoyote wataanguka… tufanye kazi mpaka haki yetu tuhakikishe imerudi na wenzetu hawana safari ya kudumu,” alisema.
Aliwataka wanachama wake kuonyesha kwa vitendo kutoitambua Serikali ikiwamo kukataa kulipishwa kodi za ovyovyo pamoja na kujitenga na viongozi wa Serikali katika utekelezaji wa majukumu yao.
“Mfano tunaweza kuamua siku fulani kuanzia saa sita, tunasimamisha vyombo vyote vya usafiri na siku nyingine tunaamua kupiga honi Zanzibar nzima kuonyesha hatuitaki Serikali ya CCM,” alisema huku akishangiliwa na umati uliofurika katika ofisi za chama hicho.
Mapema jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa CUF, Shaweji Mketo alisema kuwa amesikia juu ya wito huo lakini hakuwa amepata taarifa rasmi kutoka kwa mkuu wake.
“Nimesikia kama mlivyosikia ninyi,” alisema.
Juzi, wakati akizindua ripoti ya Uvunjifu wa Haki za Binadamu uliofanyika visiwani humo kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, Naibu Katibu Mkuu wa CUF Zanzibar, Nassor Ahmed Mazrui alisema wanazo taarifa za Serikali kutaka kuwakamata viongozi waandamizi wa chama hicho na kuwashikilia.
Alisema wamebaini mpango wa kukamatwa kwao na kuwekwa kwenye Mahakama za bara ili kuwanyamazisha Wazanzibari.

Sakata La Bunge ‘LIVE’: Nape Aumbuka Mwanza

Sakata La Bunge ‘LIVE’: Nape Aumbuka Mwanza

Tarehe May 24, 2016NapePHOTO
NapePHOTO
Waziri wa Habari, Nape Nnauye
Kufuatia kuzuia shughuli za Bunge kuonyeshwa moja kwa moja na vituo vya televisheni, Waziri wa Habari, Nape Nnauye juzi alishindwa kuhutubia wapenzi wa muziki jijini Mwanza baada ya wapenzi hao kumpokea kwa kelele za kudai bunge lioneshwe ‘live’.
Juzi, Nape aliyekuwa mgeni rasmi katika tamasha la Jembeka Festival lililofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, alipokewa na kelele za maneno “Bunge Live” wakati akikaribishwa kuhutubia katika tamasha hilo ambalo lilijumuisha msanii kutoka Marekani, Ne-yo.
“Bunge live, Bunge live, Bunge live,” walipiga kelele mashabiki waliohudhuria tamasha hilo hali iliyosababisha Waziri Nape kushindwa kuhutubia na kulazimika kuketi chini na Mbunge wa Nyamagana, Stanslaus Mabula alisimama kujaribu kuokoa jahazi, lakini naye akakumbana na kimbunga cha sauti za wananchi walioamua kulitaja jina la mbunge wa zamani wa jimbo hilo, Ezekia Wenje.
Akizungumzia tukio hilo, Nape alisema wananchi waliompigia kelele za “Bunge Live” walisukumwa na masuala ya kisiasa, ndiyo maana aliepuka kuendelea kuzungumza ili kutochafua hali ya hewa uwanjani.
“Pale uwanjani tulikwenda kwa ajili ya burudani, sasa baada ya kuona wananchi wanaanza kuleta masuala ya kisiasa nikaona ni busara kuacha kuhutubia. kuepusha shari,” alisema Nape.
Nape alitangaza uamuzi wa kusitisha kurusha moja kwa moja baadhi ya shughuli za Bunge, akisema Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) linashindwa kumudu gharama, lakini wabunge, hasa kutoka vyama vya upinzani wamepinga hatua hiyo wakisema inawanyima wananchi haki yao ya kikatiba ya kupata habari kuhusu chombo chao cha kutunga sheria.

Picha : Mourinho Akihama Kuelekea Man United

Picha : Mourinho Akihama Kuelekea Man United

Tarehe May 24, 2016mourinho anahama
mourinho anahama
Kocha Jose Mourinho ameonekana akisimamia kazi ya kuhama katika eneo la West London jijini London.
 Wakati Mourinho anasimamia zoezi hilo, hakuna ubishi sasa anahamia jijini Manchester kwa ajili ya kuanza kazi mpya.
 Baada ya kocha Louis van Gaal kutupiwa virago licha ya kutwaa Kombe la FA, kocha anayeelezwa anajiunga na Man United ni Jose Mourinho.
348879F300000578-3604976-image-a-74_1464016822981348879F300000578-3604976-image-a-74_1464016822981

Monday 23 May 2016

HOUSE FOR SALE

IMG-20160522-WA004IMG-20160522-WA006HOUSE FOR SALE

LOCATION: Located at Mivumoni, plot size is 900 sqm, 4 ensuites rooms, living room, open kitchen and a dinning. parking and tittle clean 99 yrs. price is 450 milions negotiable.

Contacts: 0652 314 181

V 1IMG-20160522-WA004V 3IMG-20160522-WA006


HOUSE FOR SALE

IMG-20160522-WA005

HOUSE FOR SALE

LOCATION: Located at Mivumoni, plot size is 900 sqm, 3 en-suites rooms, living room, open kitchen and a dinning. parking and tittle clean 99 yrs. price is 450 milions negotiable.

Contacts: 0652 314 181

OFFICE/HOUSE FOR SALE


OFFICE/HOUSE FOR SALE


V 1IMG-20160517-WA021

LOCATION: Located at Mikocheni, opposite Regence Hotel.It hase two halls, five rooms, all are master.It hase a big parking campound, can accomodate 20 cars. price is 3000 USD.

V 1IMG-20160516-WA007V 3IMG-20160517-WA016IMG-20160517-WA021

Contacts: 0652 314 181

Barcelona Watwaa Kombe La Mfalme

Barcelona Watwaa Kombe La Mfalme

Tarehe May 23, 2016Wachezaji wa Barcelona wakishangilia
Wachezaji wa Barcelona wakishangilia
Wachezaji wa Barcelona wakishangilia
Klabu ya soka ya Barcelona imetwaa kombe la Mfalme Hispania, maarufu kama Copa del Rey katika Fainali ya 114.
Wachezaji Jordi Abba na Neymar ndio walio iwezesha Barcelona kutwaa taji hilo katika Fainali iliyopigwa Jijini Madrid kwenye Uwanja wa Atletico Madrid wa Estadio Vicente Calderon.
Hii ni Fainali ya 37 ya kombe la kwa Barcelona huku Barca wakishinda mara ya 28 sasa.
Ikumbukwe Mwaka Jana, Barca walitwaa Kombe hili kwa kuifunga Athletic Bilbao 3-1.

Tanga Kunani Pale?,Timu Mbili Za Shuka Daraja

Tanga Kunani Pale?,Timu Mbili Za Shuka Daraja

Tarehe May 23, 2016Mashabiki wa Coastal Union
Mashabiki wa Coastal Union
Mashabiki wa Coastal Union
Timu nyingine ya Tanga, African Sports imeteremka daraja na kufanya timu mbili za mkoa wa Tanga kuwa zimeteremka daraja kutoka Ligi Kuu Bara hadi daraja la kwanza.
African Sports imepigwa mabao 2-0 na wenyeji wao Mtibwa Sugar hivyo kubaki na pointi 26 zinazowafanya wabaki katika nafasi ya 15 katika timu 16.
Tayari Coastal Union ilishateremka daraja na kuwa timu ya kwanza katika ligi hiyo kuteremka daraja.

Mtoto Wa Rais Atajwa ‘Kusuka Njama’ Za Kumng’oa Kitwanga

Mtoto Wa Rais Atajwa ‘Kusuka Njama’ Za Kumng’oa Kitwanga

Tarehe May 23, 2016Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Charles Kitwanga.
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Charles Kitwanga.
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Charles Kitwanga.
Sakata la kuvuliwa Uwaziri kwa aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga limechukua sura mpya kufuatia Madiwani wa Jimbo la Misungwi pamoja na wakereketwa kujitokeza na kuwataja waliohusika katika kusuka njama za kuhakikisha Waziri huyo anavuliwa madaraka.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es salaam leo Mwakilishi wa Madiwani hao Baraka Kingamkono amesema Waziri Kitwanga hakulewa kama ambavyo imetafsiri sababu ya kumvua uongozi bali alikuwa anatafutwa ili kufanikisha lengo la kumvua madaraka.
Amesema kuondolewa kwake kumesukwa na watu wa Nida hususani waliovuliwa madaraka, Mbunge wa Chalinze Ridhiwani Kikwete, Mfanyabiashara Said Lugumi pamoja na kundi linalodaiwa kutoka NSSF pamoja na Wabunge wa CCM pamoja na wa Upinzani.
Licha ya vigogo hao pia madiwani hao wamesema kundi la wafanyabishara wa Madawa ya Kulevya lenye mtandao mpana serikalini nalo limehusika katika kupanga nguvu kubwa kuhakikisha kuwa Waziri huyo anang’olewa Madarakani.
Kingamkono amesema kilichowashangaza wao kama madiwani waliokuwepo Bungeni hapo ni kuwepo kwa kundi la watu wa NIDA, NSSF na Uhamiaji kufanya sherehe baada ya maamuzi ya Rais kutolewa, jambo lilionesha kuwa wanafurahia kuvuliwa madaraka kwa Mbunge huyo.
Katika Hatua nyingine Mwakilishi wa Madiwani hao amesema Kitwanga alikuwa Mbunge na Naibu Waziri kwa Miaka 10 hakuwahi kuonekana kazini akiwa amelewa.
Madiwani hao pia wamesema hizo ni tuhuma za kupikwa na zinalenga kumchafua Mbunge Kitwanga ambaye alikuwa anaongoza huku akiwa na maadui wengi ndani ya Serikali, CCM na Nje ya CCM pamoja na Mtandao wa Madawa ya Kulevya.

Saturday 21 May 2016

Habari Njema Yanga Pluijm Anza Mazungumzo

Habari Njema Yanga Pluijm Anza Mazungumzo

Tarehe May 21, 2016
Kocha wa Yanga Hans Pluijm akiwa amenyanyua kombe walilokabidhiwa kama washindi wa michuano ya ligi kuu Tanzania bara
Kocha wa Yanga Hans Pluijm akiwa amenyanyua kombe walilokabidhiwa kama washindi wa michuano ya ligi kuu Tanzania bara
Yanga yafungua rasmi mazungumzo na kocha mkuu Hans Van Pluijm kuhusu kandarasi mpya baada ya mkataba wa awali kubaki takribani siku 10 tu.
“Sina wasiwasi kwa hilo, tunaishi vizuri na waajiri wangu kila mtu ana furaha,wana Yanga wananipenda . . Ni matumaini yangu ntaendelea kubaki hapa, najihisi ni sehem ya familia hii” ni maneno ya Hans Van Pluijm.
Uongozi wa Yanga umejibu mapigo kuwa kwa mafanikio haya ya Yanga watampa mkataba mpya mnono Pluijm huku wakidai ataendelea kubaki mpaka achoke mwenyewe.

Majaliwa Abariki ‘Kutumbuliwa’ Kwa Kitwanga

Majaliwa Abariki ‘Kutumbuliwa’ Kwa Kitwanga

Tarehe May 21, 2016
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema uamuzi wa Rais, Dkt. John Magufuli kutengua uteuzi wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga umefuata kanuni za utumishi wa umma ambazo zinakataza kulewa wakati wa kazi.
Majaliwa amesema zipo sheria za utumishi ambapo mtu hutakiwi kunywa pombe na wala hupaswi kulewa ukiwa kazini ili kusudi mtumishi uweze kuwa na akili zako zote timamu zitakazokuwezesha kufanya kazi za Serikali kwa ufanisi.
“Kuna swali aliloulizwa kuhusiana na Wizara yake na kulijibu katika muonekano ulioonyesha kuwa amelewa kiasi cha kupelekea kutojibu swali hilo vizuri na swali hilo litapaswa kurudiwa kuulizwa tena baada ya wabunge kuomba muongozo wa swali hilo,” ameongeza.

Maoni Ya Zitto Kabwe ‘Kutumbuliwa’ Waziri Kitwanga

Maoni Ya Zitto Kabwe ‘Kutumbuliwa’ Waziri Kitwanga

Tarehe May 21, 2016

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe
Mbunge wa Kigoma Mjini na kiongozi wa chama cha ACT Wazalendo Zitto Kabwe ametumia ukurasa wake wa facebook kuelezea   maoni yake  baada ya Rais Magufuli kufanya maamuzi ya kumfuta kazi Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Charles Kitwanga.
Kwa mujibu wa Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu, imebainisha kuwa   Waziri huyo ametolewa madarakani  kufuatia  kuingia bungeni jana asubuhi na kujibu swali lililoelekezwa kwa Wizara yake akiwa amelewa.
“Uamuzi wa Rais kumfukuza kazi Waziri wa Mambo ya Ndani unatuma ujumbe mmoja – hataki mchezo. Rais amethibitisha kuwa anao uwezo wa kutumbua hata aliowateua. Ni maamuzi muhimu sana kwa Kiongozi wa aina yake. Wale vijana waliokuwa wanatumwa kumtetea wasimame kumtetea. Rais kaonyesha Uongozi ‘ no nonsense “Alisema Zitto Kabwe

Monday 16 May 2016

Tutunze Mabasi Ya Mwendokasi Yatutunze-Jaffo

Tutunze Mabasi Ya Mwendokasi Yatutunze-Jaffo

Tarehe May 16, 2016Basi-Darts
Wananchi wametakiwa kutunza miundombinu ya mradi wa Mabasi yaendayo Haraka (DART) pamoja na mabasi yenyewe ili kuufanya mradi huo wa kipekee katika nchi za Ukanda wa Afrika Mashariki kuwa endelevu.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI Seleman Jaffo, na kuongeza kuwa Tanzania itakuwa miongoni mwa nchi zenye maendeleo makubwa baada ya kukamilisha miradi mikubwa iliyo kwenye mpango ya utekelezwaji, ukiwemo ujenzi wa barabara za juu ‘fly over’ kwenye makutano ya Barabara za Nyerere na Mandela ambako harakati za ujenzi zimeanza.
Naibu Waziri huyo amesema maendeleo hayo yataenda sambamba na ukamilishaji wa awamu ya pili ya mradi wa DART utakaohamia Barabara ya Kilwa itakayowaunganisha wakazi wa Mbagala kabla ya mradi wa tatu utakaowahusu wakazi wa Gongo la Mboto.
Amewataka watendaji wa DART kuharakisha mfumo wa ulipaji wa nauli kwa kutumia kadi ili kuepuka upotevu wa mapato unaoweza kusababishwa na watu wasio waaminifu huku akiliagiza Jeshi la Polisi kuimarisha ulinzi kuanzia vituoni.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa UDART David Mgwassa amesema huduma ya mabasi hayo itaanza saa 11:00 alfajili hadi saa 6:00 usiku kwa kutumia mfumo wa tiketi ambazo zitapatikana katika kila kituo huku wakiendelea kukamilisha mfumo wa kadi uanaotarajiwa kuanza kutumika rasmi baada ya siku tano.

Nape Amtaja Aliyezuia Bunge ‘Live’

Nape Amtaja Aliyezuia Bunge ‘Live’

Tarehe May 15, 2016Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema kwamba kuanzishwa kwa studio inayoratibu matangazo ya vikao vya Bunge, vinavyoendelea mjini Dodoma, ni uamuzi uliopitishwa na wabunge wenyewe na hauna mkono wa Serikali, kama inavyodhaniwa na watu wengi.
Nape alisema hayo  wakati akihitimisha mjadala wa bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2016/2017, ambapo jumla ya Sh bilioni 20.33 zilipitishwa.
“Uamuzi wa kuanzisha studio ya Bunge si wa Nape wala Serikali, ulipitishwa na Bunge wakati Nape wala Serikali ya Awamu ya Tano, haijaingia madarakani, walipitisha na bajeti, Kanuni ndo zikasema chombo cha utangazaji kitatangaza mikutano ya Bunge kwa utaratibu na mipango ya Bunge, sasa kuingizwa Serikali kunatoka wapi?” Alihoji.
Alisema Serikali kama wasimamizi wa habari, wapo tayari kusimama kati ya Bunge na wadau wa habari, kuzungumzia upungufu uliopo, ili kupatia ufumbuzi kuhusu studio hiyo na kutorushwa kwa vikao vya Bunge moja kwa moja kama ilivyokuwa zamani.
“Mlikaa wenyewe wabunge mkapanga kuanzishwa kwa studio hii na taratibu zake sio sisi Serikali, tafadhali twendeni taratibu, tusibebeshane mzigo,” alisema.
Aliwataka wabunge kutenda haki na kuacha kusema Tanzania hakuna uhuru wa habari, wakati ripoti ya Shirika la Waandishi wa Habari Wasio na Mipaka, imeonesha katika nchi 180, Tanzania ni ya 11 yenye uhuru wa habari na kwa Afrika Mashariki ni ya kwanza kwa uhuru wa habari.
Alisema katika Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari, wameweka haki zote za wanahabari na utaeleza elimu anayopaswa kuwa nayo mwanahabari ili kuondokana na ‘makanjanja’. Mchakato wa utungaji wa sheria hiyo utakamilika hivi karibuni, hivyo kuanza kutumika.

Friday 13 May 2016

Sakata La ‘Baby’ Bungeni, Wabunge 53 Ukawa Wajitoa TWPG

Sakata La ‘Baby’ Bungeni, Wabunge 53 Ukawa Wajitoa TWPG

Tarehe May 13, 2016Mbunge wa Kawe Halima Mdee.
Mbunge wa Kawe Halima Mdee.
Mbunge wa Kawe Halima Mdee.
Hatimaye Wabunge wanawake 53 wa kambi ya upinzani kutoka vyama vya CUF na Chadema wamejitoa kwenye Umoja wa Wabunge Wanawake (TWPG) kwa madai ya kudhalilishwa na Mbunge wa  Ulanga, Godluck Mlinga (CCM.
Akichangia hoja Bungeni hapo mei 5 mwaka huu Mlinga alisema wabunge hao kutoka Chadema walipata ubunge kwa njia ya mapenzi baada ya kuwa ‘baby’ wa watu.
“Kila mwanamke ndani ya chadema kaingia ubunge kwa sifa yake lakini sifa kubwa ni lazima uwe baby (mpenzi) wa mtu. Ndani ya Chadema kuna wapenzi wa jinsia moja,” alisema Mlinga.
Katika barua yao ya kujitoa jana iliyosainiwa na Mbunge wa Kawe, Halima Mdee kwa niaba ya wabunge wenzake wa kambi ya upinzani na nakala kupewa Spika, Job Ndugai, ilieleza kuwa kauli ya Mlinga inadhalilisha wabunge hao, utu na heshima ya mwanamke.
“Licha ya juhudi zilizofanywa na wabunge wa upinzani za kutaka mbunge husika(Mlinga) afute kauli yake , juhudi hizo hazikuzaa matunda kutokana na Naibu Spika(Tulia Ackson) kupuuza miongozo iliyokuwa ikiombwa.
“Na kikubwa alichokifanya baada ya mbunge (Mlinga) kumaliza kutukana ni kuwataka watu wa hansard wafute kwenye kumbukumbu za Bunge, kitu ambacho ni kinyume na matakwa ya Kanuni za Bunge,”alisema Mdee kwenye barua hiyo iliyosainiwa na wabunge wa CUF 10 na wa Chadema 43.
Alisema wabunge wa upinzani walisononeshwa zaidi na wabunge wenzao wanawake wa CCM, wakiongozwa na aliyekuwa Katibu wa TWPG, Angela Kairuki na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu, Bunge,Vijana, Ulemavu na Ajira, Jenista Mhagama kushangilia udhalilishaji huo.

clouds stream