Tuesday 31 October 2017

Zitto Kabwe Akamatwa Na Polisi Dar


Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe.


Hatimaye, Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo na Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Kabwe, amekamatwa na Jeshi la Polisi asubuhi hii akiwa nyumbani kwake jijini Dar es salaam na amepelekwa kituo cha Polisi Chang’ombe.

Hayo yameibanishwa na Afisa habari wa Chama hicho Abdallah Khamis ambapo amesema sababu za kukamatwa kwake zinawezekana kuwa ni kutokana na hotuba yake aliyoitoa juzi Oktoba 29, 2017 katika kata ya Kijichi, Mbagala Jijini Dar es salaamkatika uzinduzi wa kampeni za uchaguzi wa mdogo wa madiwani kwenye kata 43 nchini.

Hivi karibuni Zitto kabwe amekua akikosoa serikali kuhusiana na hali ya uchumi wa nchi kukua suala ambalo Zitto amesema
haliendani na uhalisia wa maisha ya wananchi

clouds stream