Friday 13 January 2017

Biden atokwa na machozi akipewa medali na Obama

Joe Biden na Barack Obama

Bw Biden amesema hakutarajia kutunukiwa medali hiyo
img-20161130-wa0008

Rais wa Marekani Barack Obama amemtunuku makamu wake Joe Biden Medali ya Rais ya Uhuru, ambayo ndiyo nishani ya hadhi ya juu zaidi anayoweza kupewa raia nchini Marekani.

Biden, ambaye alionekana kushangazwa na hatua hiyo, alitokwa na machozi alipokuwa anatunukiwa medali hiyo.

Bw Obama amemsimu makamu huyo wa rais kwa "imani yako katika Wamarekani wenzako, kwa upendo wako kwa taifa na kwa utumishi maisha yako yote."

Tuzo hiyo imetolewa kwa Bw Biden wawili hao wanapojiandaa kuondoka madarakani Donald Trump wa Republican atakapoapishwa kuwa rais mpya tarehe 20 Januari.

Bw Biden amesema anapanga kuendelea kushiriki siasa katika chama cha Democratic.

clouds stream