Sunday 29 January 2017

Westham:Payet alikosa nidhamu

Payet alijiunga na Westham akitokea Marseille June 2015

Payet alijiunga na Westham akitokea Marseille June 2015
img-20161130-wa0008

Klabu ya Westham imesema kuwa aliyekuwa kiungo wake Dimitri Payet amekosa nidhamu na upendo kwa timu hiyo baada ya kujiunga na klabu ya Marseille ya Ufaransa kwa Euro milioni 25.

Wagonga nyundo hao wa London wamesema kuwa hawakutaka kumuuza Payet huku mwenyekiti wa klabu hiyo David Sullivan akiongeza kuwa walitamani kuendelea kubaki nae.

Sullivan amesema kuwa sababu ya kumuuza ni ili kutokuondoa umoja wa wachezaji jambo ambalo ni muhimu zaidi.

Payet amejiunga na Marseille kwa mkataba wa miaka minne na nusu.

clouds stream