Wednesday 5 November 2014

KISA FREEMASON MZEE WA UPAKO AMIMINA RISASI MTAANI

KISA FREEMASON MZEE WA UPAKO AMIMINA RISASI MTAANI

.

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo-Kibangu jijini Dar,  Lusekelo Anthony ‘Mzee wa Upako’ usiku wa kuamkia Jumatatu iliyopita  alizua la kuzua kufuatia kumimina risasi kadhaa hadharani kwa madai ya kuwatawanya kundi la vijana waliodaiwa kumvamia na kuziba barabara kwa lengo la kumfanyia kitu mbaya. 
 Ishu hiyo iliyojaa utata mkubwa, ilitokea saa nne usiku maeneo ya Ubungo Kibangu jijini Dar es Salaam kwenye barabara inayotoka barabara kuu kwenda kanisani kwake.
MAELEZO YA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini, tukio lilianza kwa Mzee wa Upako aliyekuwa akipita kwa miguu kukejeliwa na vijana waliomwita Freemason kauli ambayo mtumishi huyo wa Mungu aliiona ni ya kejeli kwake.“Baada ya kuitwa Freemason, yule kijana akiwa na wenzake waliendelea kumkejeli Mzee wa Upako, akawafuata na kuwauliza mbona mnanitukana, nimewakosea nini?”
RISASI ZARINDIMA
“Alipoona wale vijana wanazidi kumkejeli huku wakionesha dalili za kumfanyia fujo ndipo alipotoa bastola yake na kufyatua risasi tatu juu hali iliyowafanya wale vijana kutawanyika huku na kule.
“Baadhi ya watu walikuwa kwenye biashara zao, nao walitimua mbio, wengine waliacha biashara, unajua risasi ni risasi tu, mtu akisikia risasi hawezi kukaa salama hata kama ni mjeshi,” kilisema chanzo hicho.
Moja wapo ya alama zinazoaminiwa kuwa ni za Freemasons
MZEE WA UPAKO ATIMUA MBIO
Ilizidi kudaiwa kwamba, kufuatia kimbiakimbia hiyo, Mzee wa Upako naye alikimbia. Baadaye alirudi eneo la tukio kimachale na kukuta watu wameanza kukusanyika kujua kulikoni.“Mzee wa Upako alipofika aliagiza mtu atakayeokota ‘magazini’ ya risasi alizofyatua angempa shilingi alfu ishirini, vijana wengine wakaingia kazini, wakapata moja, wakapewa chao, Mzee wa Upako akasema mtu akiokota nyingine aipeleke polisi,” kilisema chanzo.
MADAI YA WATU
Kuna madai kwamba, vurugu hizo zilipambwa na kijana mmoja anayeitwa Robert ambapo mtumishi huyo wa Mungu alimkomalia kuwa ndiye aliyekuwa akiongoza wenzake kumtukana na kumkashifu kwamba yeye ni Freemason na si mchungaji wa kiroho kama anavyojiita.
MZEE WA UPAKO NA GAZETI LA AMANI
Kufuatia madai hayo, gazeti hili lilimtafuta Mzee wa Upako kwa njia ya simu na alipoulizwa kuhusiana na tukio hilo, alikiri kutokea na kueleza ‘full’ mkanda.“Ni kweli lilitokea. Ni kwamba, siku hiyo nilipofika eneo lile kuna vijana wa kihuni walinifuata kwa nyuma, wakaanza kupigapiga gari langu, wengine wakizuia njia huku wakidai eti mimi ni Freemason.
Mfano wa silaha ya moto (bastola) kama  ile ya Mzee wa Upako.
“Nilijaribu kuwaambia kwamba mimi ni kiongozi wa kiroho lakini badala yake wakaanza kuniangushia matusi. Ili kujiokoa nilifyatua risasi hewani kuwatawanya,” alisema Mzee wa Upako.
Alipoulizwa kama anaweza kujua sababu za watu hao kumvamia na kumwambia yeye ni Freemason, kiongozi huyo alisema:
“Siwezi kujua, lakini mara baada ya kufyatua risasi na wao kutawanyika mimi niliamua mwenyewe kwenda Kituo cha Polisi Urafiki (Dar) kutoa taarifa.“Mimi siwezi kujua sababu za watu hao kunikashifu na kunitukana labda ukiwapata watakuambia lakini ni watu ambao naamini wametumwa na mtu f’lani ambaye mimi siwezi kukwambia lakini polisi watamjua baada ya upelelezi wao,” alisema.
Alipoulizwa alikuwa anatoka wapi usiku huo, Mzee wa Upako akajibu kwamba alikuwa anawenda kanisani kwake Ubungo Kibangu kwenye shughuli zake za kawaida za kiroho.
MADAI YA ROBERT
Madai ya upande wa Robert anayedaiwa kuongoza vijana wenzake kumfanyia vurugu Mzee wa Upako yanasema kuwa, baada ya mtiti huo wa risasi, yeye alikimbilia Kituo cha Polisi Mbezi, Dar na kufungua malalamiko yenye Kumbukumbu Na. JMD/RB/11099/2014 KUTISHIA KUUA KWA RISASI!Hata hivyo, Robert alipopigiwa simu ili kuulizwa kwa undani hakupokea  licha ya kuita kwa muda mrefu na kutumiwa meseji kwa namba yake ya simu.

clouds stream