Thursday 8 June 2017

Korea Kaskazini yarusha kombora la kushambulia meli

Korea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012

Korea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012.

Korea kaskazini imerusha makombora kadha ya kushambulia meli mashaiki mwa pwani yake, kwa mujibu wa Korea Kusini

Mamlaka zilisema kwa makombora hayo yaliyorushwa Alhamisi asubuhi karibu na mji wa Wonsan yalikuwa ni ya masafa mafupi.

Makombora hayo yaliruka umbali wa kilomita 20o kabla ya kuanguka baharini.

Majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini mwaka huu yamekiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa.

Wataalamu wana hofu kuwa majaribio hayo na hatua za Korea kutundika silaha za nuklia katika vichwa vya makombora.

Map of North Korea showing Wonsan in east
Ramani ya Korea Kaskazini.

Msemaji wa Jeshi la Korea Kusini amesema kuw majiribio ya hivi punde yalionyesha kuwa Korea Kaskazini ilitaka kuonyesha kuwa ina uwezo wa kulenga meli kubwa baada ya mazoezi ya hivi majuzi kati ya Marekani na vikosi vya Korea Kusini

Makomboa ya kushambulia meli ni makombora ambayo huelekezwa. Mwaka 2012 Korea Kaskazini ilionyesha makomboa kadha kama hayo yanayojulikana kama Styx.

Lakini hapo awali Korea ilijaribu bila mafanikio kufanyia majaribio makombora ya kushambulia meli.

Marekani inaweka mitambo ya kujikinga nchini Korea Kusini
Marekani inaweka mitambo ya kujikinga nchini Korea Kusini.

clouds stream