Thursday 15 June 2017

Lema Afunguka Magufuli Kukutana Na Bosi ACACIA

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.
IMG-20170426-WA0006

Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema. Mbunge wa Arusha Mjini Bw.Godbless Lema amefunguka kuhusiana na Rais Magufuli kukutana na Bosi kampuni ya madini ya ACACIA ambaye amekubali kulipa fedha zote kampuni hiyo inazodaiwa toka ianze kuchimba madini hapa nchini.

Kwa mujibu wa Rais Magufuli alisema jana kuwa amefanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton Ikulu jijini Dares salaam.

Baada ya Mazungumzo hayo Prof. John L. Thornton amesema kampuni yake ipo tayari kufanya mazungumzo na Tanzania yatakayozingatia maslahi ya pande zote mbili na pia ipo tayari kulipa fedha zote ambazo inapaswa kulipa kwa Tanzania.

Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii Lema amesema amependa Rais alivyokutana na Bosi wa Acacia na kufanya nae mazungumzo kwa upole na kufikia muafaka wa kuilipa serikali madeni yote.

Screenshot_20170614-235506-768x341 (1)

clouds stream