Wednesday 21 June 2017

Zitto Apata Pigo Lingine,Kada ACT-Wazalendo Atimkia CCM

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo.
Kiongozi wa Chama cha ACT­Wazalendo.
IMG-20170426-WA0006

Kada wa chama cha ACT­ Wazalendo mkoani Pwani wilayani Kibaha amehamia Chama cha Mapinduzi (CCM) kwenye mkutano wa Rais Magufuli katika uwanja wa Bwawani wilayani Kibaha leo.

Akizungumza mara baada ya kupewa na nafasi na Msemaji wa Chama Humprey Polepole Kada huyo ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja amesema katika kampeni za urais mwaka 2015 alimpigia kura Rais Dkt.John Magufuli kutokana kile alichosema ni sauti ya Mungu ikimtaka afanye hivyo.

Chama cha ACT­Wazalendo kime endelea kupata pigo kufuatia Vigogo wake kupata shavu katika Serikali ya Rais Magufuli akiwemo Mwenyekiti wa ACT­Wazalendo Anna Mghwira kuteuliwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro na Prof. Kitila Mkumbo kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Majina Umwagiliaji,

clouds stream