Sunday 21 May 2017

Kipindupindu chapiga kasi Yemen

Mlipuko wa Kipindupindu Yemen

Mlipuko wa Kipindupindu Yemen
IMG-20170426-WA0006

Shirika la Afya Dunia limeelezea mlipuko wa kipindupindu nchini Yemen ni kama tahadhari kwa sababu unasambaa haraka kuliko ilivyo tarajiwa.

Takriban watu 250 wamefariki dunia kwa ugonjwa huo mwezi uliopita.

Shirika la Save the Children limesema mamia ya watu wanaodhaniwa kuambukizwa ugonjwa huo wanaripotiwa kila siku na kwamba mlipuko huo karibuni utakuwa janga kubwa.

Ugonjwa huo ambao unasambaa kupitia uchafu katika chakula na maji, unaweza kudhibitiwa kirahisi, lakini mfumo wa afya nchini Yemen umevurugika kutokana na mapigano yanayoendelea kati ya waasi wa Ki Houthi na majeshi ya serikali, ambayo yanaungwa mkono na muungano wa majeshi yanayoongozwa na Saud Arabia.

clouds stream