Tuesday 23 May 2017

Yahya Jammeh aliiba dola milioni 50 kutoka kwa serikali

Jammeh alikimbia kuenda nchini Equitorial Guinea baada ya miaka 22 uongozini.

Jammeh alikimbia kuenda nchini Equitorial Guinea baada ya miaka 22 uongozini.
IMG-20170426-WA0006

Aliyekuwa rais wa Gambia Yahya Jammeh aliiba takriban dola milioni 50 kutoka kwa taifa kabla ya kuondoka nchini humo mwezi Januari, kwa mujibu wa waziri wa sheria.

Jammeh analaumiwa kwa kuiba pesa hizo kupitia kwa kampuni ya mawasiliano ya serikali.

Kwa sasa mahakama imeagiza kutwaliwa kwa mali yake yote yaliyosalia nchini Gambia.

Jammeh alikimbia kuenda nchini Equitorial Guinea baada ya miaka 22 uongozini.

Alishindwa kwenye uchaguzi mwezi Disemba na baadaye kukubali kuondoka madarakani baada ya vikosi vya eneo ilo kutishia kumuondoa madarakani.

Magari ya kifahari na bidhaa zingine ziliripotiwa kuingiza kwenye ndege ya mizgo ya Chad wakati Jammeh alikuwa akiondoka nchini humo.

Pesa hizo zilitajwa kuwa dola milioni 11 na waziri wa masuala ya ndani Mai Ahmad Fatty, ambaye wakati huo alikuwa msaidizi wa rais Adama Barrow.

Lakini siku ya Jumatatu waziri wa sheria Abubacarr Tambadou, alisema kuwa bwana Jammeh aliiba dola milioni 50 kati ya mwaka 2006 na 2016.

clouds stream