Wednesday 1 July 2015

Ghana yaanza kupaa Kimataifa, yazindua gari lake

Ghana yaanza kupaa Kimataifa, yazindua gari lake


Baadhi ya Magari yanayotengenezwa nchini Ghana.
Baadhi ya Magari yanayotengenezwa nchini Ghana.
Gari la Kantanka kutokana nchini Ghana.
Gari la Kantanka kutokana nchini Ghana.
Mafundi wa magari hayo.
Mafundi wa magari hayo.
Nchi ya Ghana imefungua njia kwa nchi  nyingine barani Afrika kufuatia kuanza utengenezaji wa magari aina ya Kantanka ambayo ni pamoja na lile  aina ya 4 by 4 ambalo linatarajiwa kuuzwa kwa takriban pauni 14,000.
Lakini je,kampuni hiyo itaweza kukabiliana na ushindani mkubwa kutoka kwa magari kama vile Toyota,Land Rover na BMW?.
Kwadwo sarfo ni mwana wa mmiliki wa magari hayo. Babaake ni m’bunifu ambaye pia ni kiongozi wa dini. Hupata fedha kutokana na kilimo na uchimbaji.
Magari ya Kantanka yanafananishwa na magari makubwa kama vile Toyota Prado ama MItsubishi Pajero.
Mbele ya gari hilo kuna michoro ya kucha za chui pamoja na nembo ya kampuni hiyo ya nyota ya Afrika.
Kwa mujibu wa mmoaja wa raia nchini humo amesema  watu wanapenda kununua bidhaa kutoka nje kwa hivyo italazimu kufanyika kwa mauzo ya ziada kwa gari hizi za kantanka kukubalika.
Inaonekana kwamba raia wengi kama alivyodai hapo awali Professa wana wasiwasi kuhusu usalama wa gari hilo na kudumu kwake.
Profesa Robert Ebo Hinson ambaye ni mkuu wa kitengo cha mauzo katika chuo kikuu cha Ghana:Nadhani kile kilichotokea hapo awali ni kwamba tumefanywa tuamini kwamba kile kinachotengezwa katika mataifa ya magharibi ni imara.

clouds stream