Wednesday 1 July 2015

Urais 2015: Watia nia 9 warudisha fomu

Urais 2015: Watia nia 9 warudisha fomu


Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhavi fomu za kuwania Uteuzi wa CCM wa kugombea urais kwenye Ofisi Kuu ya CCM mjini DOdoma Jana.
Waziri Mkuu,Mizengo Pinda akimkabidhi Naibu Katibu Mkuu wa CCM, Rajab Luhavi fomu za kuwania Uteuzi wa CCM wa kugombea urais kwenye Ofisi Kuu ya CCM mjini DOdoma Jana.
Wanasiasa 9 wamerejesha fomu za kuomba ridhaa kuteuliwa kuwa rais makao makuu ya CCM mkoani Dodoma. Wanasiasa hao  ni  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda,  Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, Bernad Membe na Balozi Mahiga.
Wengine ni  Joseph Chaggama, Mbunge wa zamani wa Iringa Mjini, Monica Mbega, Amosi Siyantemi, Dk Mwele Malecela, pamoja na   Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Harrison Mwakyembe.
Baada ya kurudisha fomu hizo wanasiasa hao watasubiri vikao vya uteuzi vitakavyofanyika mapema  mwazoni mwa mwezi julai.
Kwa mujibu wa Ratiba iliyotolewa na chama hicho inaonesha kuwa  vikao vya uchujaji vitakuwa kama ifuatvyo,
Kamati ya usalama na Maadili Zanzibar 4/7/2015
Kamati maalumu ya Halmashauri kuu ya Taifa 5/7/2015
Kamati ya Usalama na Maadili Taifa 8/7/ 2015
Kamati ya Halmashauri kuu ya Taifa 9/7/2015
Halmashauri kuu ya Taifa 10/7/2015
Mkutano mkuu wa Taifa 11-12/7/2015

clouds stream