Wednesday 1 July 2015

Uhaba wa mafuta nchini wachukua sura mpya Bungeni

Uhaba wa mafuta nchini wachukua sura mpya Bungeni


Naibu wazii wa Nishati na Madini Charles Mwijage .
Naibu wazii wa Nishati na Madini Charles Mwijage .
Serikali imesema kwamba  akiba ya Mafuta ya Petrol nchini Tanzania inatoshelea hadi siku 40.Hatua hiyo inafuatia kuwepo kwa madai  kutokea uhaba wa mafuta siku kadhaa zijazo.
Akijibu hoja  ya Mbunge wa Ubungo John Mnyika aliyeomba Bunge hilo kujadili hoja hiyo kwa njia ya dharula kwa kuwa linamaslahi kwa uchumi wa  taifa Naibu wazii wa Nishati na Madini Charles Mwijage amesema mafuta yapo na kuna meli  zipo nje maji  marefu zinakuja nchini zikiwa na shehena ya mafuta.
Amewahakikishia wananchi kuwa nchi haiwezi kuapata tatizo la uhaba wa mafuta huku akisisitiza kuwa  kwa kushirikiana  na TCRA  wanawatafuta waliosambaza taarifa hizo.
Naye Naibu waziri wa Fedha Adam Malima amesema serikali itahakikisha kuwa wananchi wanapata  huduma  ya mafuta   kama  kwaida.

clouds stream