Tuesday 21 July 2015

Pele afanyiwa upasuaji tena


Pele afanyiwa upasuaji tena


Tarehe July 20, 2015
Mwnasoka mkongwe wa Brazil, Pele
Mchezaji mkongwe wa Brazil, Pele amelazimika kurejea tena hospitali kwa matibabu ikiwa ni miezi miwili imepita tangu afanyiwe upasuaji katika kibofu cha haja ndogo.
Vyombo vya habari vya Brazil vimesema Pele (74) alikuwa na maumivu ya misuli na amefanyiwa upasuaji mgongoni katika hospitali ya Albert Einstein, huko Sao Paulo.
Pele, ambaye ametwaa mara tatu kombe la dunia, alikuwa akitibiwa maambukizi ya mfumo wa haja ndogo miezi nane iliyopita baada ya kutolewa mawe kwenye figo yake.

clouds stream