Sunday 19 July 2015

Urais CCM wapamba Moto

Urais CCM wapamba Moto

Tarehe July 19, 2015

Mgombea Urais CCM akiwasili jijini Mwanza.
Urais umepamba moto CCM ambapo  chama hicho kimeanza mchakato wa kumtambulisha mgombea wake wa urais Dkt. John Pombe Magufuli aliyechaguliwa hivi karibuni.
Mgombea huyo jana amepokelewa  na umati wa wananchi alipowasili mkoani Mwanza  na baadae kuwahutubia wananchi  hao ofisi za CCM mkoa wa Mwanza.
Aidha, mgombea  huyo alitambulishwa jijini Dar es salaam  siku ya jumanne  wiki  iliyopita amejizolea umaarufu kutokana na utendaji wake. Wanananchi mbalimbali jijini Dar es salaam wamekipongeza chama hicho kwa uteuzi huo.


Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM akiwasili kwenye ofisi za CCM mkoa wa Mwanza tayari kwa kuwasalimu wananchi na kujitambulisha.

Msafara wa mgombea Urais CCM jijini Mwanza.

clouds stream