Monday 27 July 2015

Nkurunziza ashinda kwa kishindo Urais Burundi

Nkurunziza ashinda kwa kishindo Urais Burundi



Rais Nkurunziza ashinda.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza ameshinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika nchini humo, kwa kupata asilimia 69.41 ya kura zote zilizopigwa Jumanne wiki hii.
Taarifa zilizotolewa na AFP jana jioni, zilieleza kuwa Tume ya Uchaguzi ya Burundi, imetoa matokeo hayo yaliyoonesha kuwa amepata ushindi katika awamu ya kwanza ya upigaji kura.
Kwa matokeo hayo, Nkurunziza amewashinda wagombea wanane walioshiriki katika uchaguzi huo na hivyo kupata fursa ya kuongoza nchi hiyo kwa awamu ya tatu, baada ya kushiriki katika uchaguzi wa kidemokrasia mara mbili.

clouds stream