Wednesday 1 July 2015

Ndege ya Jeshi yaangukia nyumba, watu 100 wafariki dunia


Ndege ya Jeshi yaangukia nyumba, watu 100 wafariki dunia


Nyumba na maduka yaliharibiwa katika ajali hiyo.
Nyumba na maduka yaliharibiwa katika ajali hiyo.
Ndege ya kijeshi yaua watu 30 Indonesia .
Ndege ya kijeshi yaua watu 30 Indonesia.
Takriban watu 100 wamefariki  baada ya ndege ya uchukuzi wa kijeshi ya Indonesia kuanguka mapema leo katika maeneo yenye makazi ya watu huko Medan Sumatra.
Maafisa wa kijeshi wanasema kuwa tayari miili 49 imepatikana katika eneo la ajali. Maafisa wa kijeshi nchini Indonesia, wanasema kwamba ndege hiyo ya uchukuzi ya majeshi ya taifa hilo, ilianguka muda mfupi baada ya kupaa angani.
Ndege hiyo ya kubeba mizigo aina ya Hercules 130 ilikuwa na wahudumu 12 na abiria 50 ilipoanguka. Kuna ripoti kuwa watu bado wanasikika wakipiga mayowe katika majengo yaliyoanguka.
Ndege hiyo iliharibu kabisa nyumba ambayo iliangukia katika mji wa Medan, kaskazini mwa jimbo la Sumatra.
Picha za runinga na kwenye mitandao ya kijamii zinaonesha moto unatoka kwenye mabaki ya ndege hiyo.
Msemaji wa jeshi la angani alisema kuwa rubani alikuwa ameomba kurejea katika uwanja wa kambi ya kijeshi kwa sababu ya matatizo ya kimitambo.

clouds stream