Monday 27 July 2015

Matukio katika picha: Rais Obama alipowasili nchini Kenya

Matukio katika picha: Rais Obama alipowasili nchini Kenya



Rais wa Marekani Barack Obama akiwasili nchini Kenya.
Rais Barack Obama wa Marekani amewsili nchini Kenya na kupokelewa na mwenyejinwake Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta   kwenye uwanja wa ndege wa wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.
Akiwa nchini Kenya Rais Obama atafungua mkutano wa Kimataifa  wa kibiashara, Ugaidi na haki za binadamu  unaofanyika nchini humo kabla ya kuendelea na ziara yake nchini Ethiopia
Endelea kuwa nasi tutakujulisha kila kinacho endelea katika ziara ya Rais Obama nchini Kenya.
Rais Obama akisalimiana na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta mara baada ya kuwasili nchini Kenya.
Rais wa Marekani Barack Obama akiwa na bibi yake Mama Sarah Obama kushoto na dada yake Auma Obama katika chakula cha jioni na wanandugu wa familia ya Obama nchini Kenya.
Ndege ya Marekani iliyombeba Rais Barack obama.
Rais Barack Obama wa Marekani akipokea shada la maua mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi.

clouds stream