Thursday 28 January 2016

Baada Ya Kuitandika Everton,Man City Waingia Fainali Na Liverpool


Baada Ya Kuitandika Everton,Man City Waingia Fainali Na Liverpool


Tarehe January 28, 2016
Mshambuliaji wa Manchester City Kun Aguero akishangilia baada ya kuifungia goli timu yake
Mshambuliaji wa Manchester City Kun Aguero akishangilia baada ya kuifungia goli timu yake

Man City imekua timu ya pili kufuzu fainali ya mchezo wa kombe la Capital baada ya kuichapa Everton kwa mabao 3-1.
Everton ndio walikua wa kwanza kuzifumani nyavu za Man city baada ya kiungo Ross Barkley kuifungia timu yake bao la kuongoza katika dakika ya 18 ya mchezo.
Kiungo wa kibrazl Fernandinho akasawazisha bao hilo kwa shuti kali baada ya kutoka piga nikupige kwenye goli la everton katika dakika ya 25.
Kevin De Bruyne akaongeza bao la pili baada ya kunganisha krosi ya kutoaka upande wa kushoto iliyopiga na Raheem Sterling, kina Sergio Aguero kun, akahitimisha kazi kwa bao la tatu.
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika Goodson Park Everton walishindwa kwa ushindi wa mabao 2-1,Man City watachuana na Liverpool katika mchezo wa fainali utaofanyika februari 28 katika dimba la la Wembley.

clouds stream