Sunday 10 January 2016

Yanga ‘Out’ Mapinduzi Cup,Fainali Ni Mtibwa Sugar Na URA


Yanga ‘Out’ Mapinduzi Cup,Fainali Ni Mtibwa Sugar Na URA


Tarehe January 10, 2016
Winga wa Yanga Simon Msuva
Winga wa Yanga Simon Msuva
Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Young Africans Sports Club wameungana na watani wao wa jadi, Simba Sports Club kuyaaga mashindano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kukubali kichapo mbele ya Uganda Revenue Authority (URA) kwa njia ya matuta 4-3.
Wapigaji penati wa Yanga walikuwa ni Yondani, Msuva na Munishi ambao walufunga, huku Mwashiuya na Bussungu wakipoteza.
Wakati penati za URA zilipigwa na Kulaba, Kiyuyine, Otieno na Bwete ambao walifunga na Sikito akikosa tuta alilopiga.

clouds stream