Thursday 14 January 2016

Real Madrid Na Atletico Madrid Wapigwa Marufuku Kununua Wachezaji

Real Madrid Na Atletico Madrid Wapigwa Marufuku Kununua Wachezaji

Tarehe January 14, 2016
Christiano Ronaldo wa Real Madrid
Christiano Ronaldo wa Real Madrid
Miamba wa Uhispania Real Madrid na Atletico Madrid wamepigwa marufuku kutonunua wachezaji wapya sokoni vipindi viwili.
Klabu hizo zimeadhibiwa na shirikisho la soka duniani Fifa kwa kukiuka sheria za uhamisho wa wachezaji kuhusu kununuliwa kwa wachezaji ambao bado ni watoto.
Marufuku hiyo haitaathiri kipindi cha sasa cha kununua wachezaji, ambacho kinaendelea hadi mwisho wa mwaka huu.
Atletico pia wametozwa faini franka 900,000 za Uswizi ambazo ni sawa na pauni 622,000 za Uingereza, nao Real wakatakiwa kulipa franka 360,000 (£249,000).

clouds stream