Monday 18 January 2016

Wakazi Mkwajuni Wafunga Barabara Kupinga Bomoa Bomoa

Wakazi Mkwajuni Wafunga Barabara Kupinga Bomoa Bomoa

Tarehe January 18, 2016
Jeshi la Polisi likitoa msaada katika barabara iliyotokea vurugu katika Bonde la Mkwajuni leo.
Jeshi la Polisi likitoa msaada katika barabara iliyotokea vurugu katika Bonde la Mkwajuni leo.
Wananchi  ambao makazi yao yamebomolewa  katika Bonde la Mto mkwajuni leo wamefunga barabara ya Kinondoni Kawe katika Bonde la Mkwajuni  na kusababisha usafiri wa daladala na magari mengine kusimama kwa muda.
Kwa mujibu wa wakazi wa Bonde hilo wameiambia Hivisasa kuwa wamechukua hatua  ya kufunga barabara hiyo kufuatia kukerwa na zoezi la Bomoa bomoa lililotekelezwa na serikali na kuwaacha wakiwa hawana mahali pa kwenda.
Licha ya wananchi hao kuzuia barabara hiyo, Jeshi la Polisi Manispaa ya Kinondoni limefika katika eneo  hilo na  kuwazuia wananchi waliokuwa wamechoma matairi ya gari katikati ya barabara.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi  waliamua kukimbia mara baada ya kuona magari ya Jeshi la Polisi katika eneo hilo.

Barabra iliyofungwa na wananchi.
Barabara iliyofungwa na wananchi.
Baadhi ya wananchi wakiangalia kinacho endelea mara baada ya barabara ya kufungwa.
Baadhi ya wananchi wakiangalia kinacho endelea mara baada ya barabara  kufungwa kutokana na Vurugu.

clouds stream